REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

KENYA: WABUNGE WATISHIA HIVI...

8:34:00 AM Add Comment

Wabunge wametishia kuibandua Tume ya Kuratibu Mishahara ya watumishi wa umma kutokana na hatua yake ya kupunguza mishahara yao.

Tayari mbunge wa Igembe Kusini Mithika Linturi ametangaza kuwasilisha ombi kwa spika wa bunge la taifa, kutoa nafasi kwa hoja ya kuitaka tume hiyo ivunjwe huku akidai kuwa Tume imekwenda kinyume na katiba. Hata hivyo, Wakili Bobby Mukangi ambaye alihusika katika kuandika katiba anasema kwamba bunge halina Mamlaka anayodai Linthuri.

Anasema tume ya kuratibu mishara ya watumishi wa umma ni huru na haiwezi kushinikizwa na yeyote inapotekeleza majukumu yake.

Kwa mujibu wa Katiba tume hiyo ndiyo yenya mamlaka ya kuratibu mishahara ya watumishi wa umma wakiwemo wabunge.

KENYA : UHURU KENYATTA KAFANYA HAYA !!!

8:29:00 AM Add Comment

Rais Uhuru Kenyata amepunguza kiwango cha wizara serikalini kutoka 44 hadi 18.

Kwenye mabadiliko hayo; afisa ya Rais itakuwa na afisi tendaji ya Rais na afisi tendaji ya Naibu Rais ambapo kutakuwa na wizara mbili ambazo ni Wizara ya Masuala ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Taifa na Wizara ya Ugatuzi na Mipango.

Wizara nyingine ni ile ya Ulinzi, Wizara ya Masuala ya Nje, Wizara ya Elimu, itakayokuwa na idara za elimu na ile ya sayansi na teknolojia, Wizara ya Taifa ya Fedha, Wizara ya Afya, Wizara ya Uchukuzi na 
Miundomisingi, itakayokuwa na idara za huduma za usafiri na ile ya miundomisingi.

Aidha kuna Wizara ya Mazingira, Maji na Maliasili, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Miji, Wizara na Habari, Mawasiliano na Teknolojia, Wizara ya Michezo, Utamaduni na Sanaa, Wizara ya Leba, Huduma za Jamii na Usalama, Wizara ya Kawi na Masuala ya Mafuta, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Wizara ya Biashara na Utalii na Wizara ya Uchimbani Majini.

KENYA: 9 WAUAWA MJINI GARRISA KENYA

8:24:00 AM Add Comment

Idadi ya watu walioaga dunia kwenye shambulizi alhamisi usiku mjini Garissa imefikia 9, baada ya wengine watatu kufariki wakikimbizwa hospitalini.

Hii ni baada ya watu wasiojulikana kuvamia hoteli moja mjini humo wakiwa wamejihami kwa bunduki aina ya AK-47 na kuwamiminia risasi wateja waliokuwa ndani ya hoteli hiyo kwa jina 'Kwa Chege'. Mkuu wa polisi mkoa wa kaskazini mashariki Charlton Muriithi amesema kuwa kufikia sasa hawajabaini lengo la mauaji hayo ambayo yamesababisha taharuki kutanda mjini Garissa.

 Ikumbukwe kuwa mapema mwezi huu mwanafunzi aliuawa huku watu wengine watatu wakijeruhiwa baada ya watu waliojihami kutekeleza uvamizi katika kioski kimoja mjini humo.
Vile vile, mwanzoni mwa mwezi Aprili, maafisa wawili wa polisi waliuawa na watu wanaoaminika kuwa wafuasi wa Al Shabaab.

AYAAAAAAA: MADEE TUTAKUWA TUNAONA HII KITU KATIKA VIDEO YAKO YA "SI MIMI"?

8:09:00 AM Add Comment


MEKUZI: MWANAFUNZI HUYU MREMBO, APOKEA KICHAPO KWA WIZI WA........

3:37:00 AM Add Comment
 HURUMA: Binti Murembo akiwa Chini ya Ulinzi wa Wananchi baada ya Kuwiba Viatu....

NGOJA NIMTAFUTE BABY: Akibofya Simu kuwasiliana na Honey wake ili amsaidie kulipa Deni

Tukio la mrembo  huyo  kupokea  kichapo na kuvuliwa  nguo na  kupokonywa  simu yake na mikoba zaidi ya mitano  pamoja na kiasi cha TSh 15,000 ambazo alikuwa amezihifadhi limetokea  jumapili  wiki hii katika  eneo la Miyomboni mjini Iringa.

Akielezea juu ya mkasa  huo  wa aina yake  leo mfanyabiashara   huyo  mama Masawe  alisema kuwa eneo  hilo amekuwa na kawaida ya  kuibiwa  viatu katika  duka  lake la viatu  vya mtumba .....

Mama  huyu  anadai    kuwa  mbali ya  kukamatwa kwa mrembo  huyo  bado amepata  kukamata  vijana  zaidi ya  wawili watanashati ambao  wamekuwa wakifika na kujifanya wakichagua viatu na  kuishia  kuiba na kutoweka .

Binti   huyo ambaye  ni  mwanachuo   alifika  dukani hapo   na  kuanza kuchagua  viatu akijifanya  ni  mteja .....

Baada  ya  kuona  muuza  duka  ameangalia  pembeni, binti  huyo   alichukua  pea  mbili  za   viatu  na  kuzificha  kwapani  asijue  kwamba  pembeni  kulikuwa  na  mtu  mwingine  aliyekuwa  akimwangalia....

Alipoaga na  kutaka  kuondoka ndipo timbwili la  kichapo  lilipoanza kwa mrembo huyo ambae aliomba asipelekwe  polisi  na  asipewe  adhabu  kubwa  kwa  kuwa   ana ujauzito  wa miezi mitatu tumboni.

Alisema  kuwa  kutokana na maombi ya mrembo huyo  kupunguziwa adhabu  hakuweza kumfikisha  polisi  zaidi ya kumpa kichapo  cha kufa mtu na kumpokonya  mali  zote alizokuwa ametoka  kuiba katika maduka ya  Miyomboni mjini hapa pamoja na  simu  yake ya kiganjani .

MNADA BANNER