REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

SUMATRA - MBEYA :HAKUNA LESENI KWA MAGARI YANAYOBEBA ABIRIA WASIOZIDI 14

3:18:00 AM Add Comment


Mamlaka ya Uthibiti wa Usafiri wa Nchi kavu na majini( Sumatra) Mkoani Mbeya imesitisha  utoaji wa leseni ya kubeba abiria  wa kawaida kwa waombaji wapya wenye magari yenye uwezo wa kubeba abiria  wasio zidi 14.

Aidha  Mamlaka hiyo imesema kuwa endapo wamiliki hao wa magari hayo watahitaji kutoa huduma kwa jamii mamlaka hiyo itatoa  leseni kwa ajili ya kubeba watalii tu .

         
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Mbeya na Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Ndugu Diwani Athumani wakati akizungumza na madereva wa mabasi madogo yaendayo Mji mdogo wa Tunduma Wilayani  kufuatia kuwepo kwa mgomo uliodumu kwa miezi 3 sasa  ambao umefanywa na madereva hao kwa kuto safirisa abiria waendao Tunduma.

 Mgomo huo wa madereva hao umesababishwa na baadhi ya wamiliki wa magari madogo aina ya( Noah) ambayo yamekuwa yakifanya shughuli ya kubeba abiria toka Mbeya hadi Tunduma hali iliyo zua mgogoro mkubwa baina ya wamiliki wa gari hizo Ndogo pamoja na madereva wa Costa ambao ndio wenye leseni za  kusafirisha abiria Toka Mbeya hadi Tunduma.

      
Awali wakati akizungumzana madereva hao Kamanda Diwani amewataka mara moja watu wanaofanya biashara hiyo kuacha mara moja kwani sheria itachukua mkondo wake.

Amesema sababu kubwa ya kusitisa huduma inayo tolewa na magari hayo madogo ni kuzuia majanga ambayo yanaweza kutokea kwani gari hizo hazina madirisha makubwa pamoja na milango yake kuwa midogo ambayo na haina milango ya dharura endapo kunaweza kutokea tatizo lolote.


Kufuatia  hali hiyo Kamanda Diwani amewataka madereva costa ambao wamekuwa wakitoa huduma hiyo kwa muda mrefu kuachana  na mgomo huo badala yake waendelee kutoa huduma kwa  wananchi kama ilivyo kuwa awali.

MBEYA YETU

PICHA: HIYO TUK-TUK IKO POA BHANA

3:10:00 AM Add Comment


Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli, Mh Edward Lowassa amekabidhi pikipiki  nne za miguu mitatu maarufu kama majaji za kubebea mizigo  zenye thamani ya kiasi cha  shilingi millioni 50 kwa umoja wa vijana wilaya ya Monduli, ili kusaidia vijana kukabiliana na tatizo la Ajira.Pichani Mh Lowassa akikabidhi pikipiki hizo kwa mmoja wa viongozi wa matawi ya vijana wilayani hapo, yumbani kwake Ngarash Monduli.

DK SHEIN : TUTAMTAFUTA MUUAJI MPAKA TUMPATE

3:06:00 AM Add Comment



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, amepokea kwa mshtuko mauaji ya Padri Evaristus Mushi na kutoa pole kwa  waumini, ndugu jamaa, marafiki na wananchi wote wa Zanzibar kufuatia kifo hicho.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mhe. Mohamed Aboud ameeleza hayo jana, Jumatatu, Februari 18, 2013 na kusisitiza kwamba   Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi itawasaka hadi kuwatia mikononi na hatimaye kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote waliohusika na mauaji hayo.

Waziri Aboud ameyaeleza hayo wakati alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Vuga, kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kufuatia mauaji ya  Padri Evaristus Mushi wa Kanisa Katoliki  Zanzibar Parokia ya Mtakatifu ST.Joseph, Shangani.

Hapo jana Dkt. Shein alikutana na Askofu Augustino Shao wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Zanzibar, huko katika Ikulu Ndogo Migombani, Zanzibar  na kueleza masikitiko yake kutokana na mauaji hayo ya Padri Mushi wa Kanisa Katoliki la Zanzibar, na kuelezea haja ya kuwepo kwa uvumilivu katika kipindi hichi cha msiba.

Katika mazungumzo na waandishi wa habari,  Waziri Aboud alisema kuwa Serikali imejipanga vizuri  kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha kuwa watu wote waliohusika na mauaji hayo wanakamatwa mara moja .

“Kutokana na jiografia ya Zanzibar,Tunaelewa kwamba zipo sehemu katika kisiwa cha Zanzibar ambazo wahalifu wanaweza kuzitumia, hivyo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo husika vitaziba mianya yote ili kupambana na uhalifu “, alisema Aboud.

Alisema matendo ya uhalifu yanafanywa katika mazingira ya usiri mkubwa kwa hivyo ili wahalifu hao wakamatwe wananchi hawana budi kutoa mashirikiano  kwa Jeshi la Polisi pale wanapohitajika.

Akijibu suali la Mwandishi, Mhe.Aboud alikanusha taarifa zilizozagaa mitaani za kuwepo silaha nyingi mikononi mwa watu wasiohusika na kuwataka wananchi kuondoa hofu.

Sambamba na hayo, Mhe. Aboud amewataka viongozi wa dini mbali mbali  pamoja na waumini wa dini zote  hapa Zanzibar kuwa wastamilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezi.

Aidha, Waziri Aboud alisisitiza haja ya kuwepo uvumilivu kwa waumini wa dini zote ili kuirejesha Zanzibar katika historia yake ya kutokuwa na migongano ya kidini.

MWANAFUNZI AJITEKETEZA KWA MOTO

2:54:00 AM Add Comment


Na John Banda, Dodoma
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Nzuguni iliyopo manispaa ya Dodoma amekufa kwa kujichoma moto baada ya Mjomba wake kumchapa viboko kutokana na kosa la kutomsaidia Bibi yake kuosha vyombo.

Tukio la kifo cha mwanafunzi huyo lilitokea jana jumapili ambapo saa 11 jioni katika hospital Rufaa ya General Dodoma baada ya kulazwa kwa masaa kadhaa

Akisimulia kifo marehemu nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa wa maweni B. mjomba wa marehemu Paul Samwel 21 alisema kuwa siku hiyo ya tukio alitoka kazini kwake mapema akarudi nyumbani na kumkuta  mama yake akiingia jikoni baada ya kutoka kuosha vyombo ndipo alipotaka kujua alipo Catherine kwani siku hiyo ya ijumaa wanawahi kutoka shule

Samwel alisema mama huyo alimjibu kuwa Katherine alipofika alitoka na hajui alipoelekea ndipo alipomsubili mpaka aliporudi akamuuliza kwamba kwanini alimuacha Bibi yake afanye kazi wakati anajua haoni vizuri ndipo akamua kukata fimbo na kuanza kumchapa alipotosheka akamuacha baada ya muda akiwa nyumba jirani alisikia kelele nyumbani.

''ndugu yangu nilikuta mjomba anaungua mwili mzima kuanzia kichwani tuliposaidia na kumpeleka hospital mwili wote haukuwa na kazi bali moyo tu ndiyo ulikuwa ukidunda pekee na jana jumapili saa 11 jioni alikata roho kwa weli ameniuma sana maana ni kama mdogo wangu maana mama yake alimuacha akiwa mdogo sana'', alisema Samwel


Kwa upande wa Wanafunzi wenzake waliofika kuomboleza nyumbani hapo walisema Marehemu alikuwa akilalamika mara kwa mara kuwa alikuwa akiteseka sana nyumbani kiasi cha kila siku kupewa adhabu za vipigo na mjomba wake huku akitaka fedha kwa Babu yake za kunulia vifaa vya shule na mahitaji mengine kama mtoto wa kike alikuwa anachapwa pia.

Wanafunzi hao Desleria Lupembe, Elika Zabron, Maria Paul na Anastadhia Boniface Wote wa kidato cha pili Nzuguni walisema kwa siku zilivyokuwa zinazidi kusogea karibu na kifo chake walikuwa wakimshangaa mwenzao huyo.

''Mara kwa mara alikuwa akituambia wakati wowote atakufa hivyo tumpe picha zetu ili awe anatuangalia na sisi hapa unayetuona tulishampa zetu, lakini alhamis akawa serios sana akasema mambo yamezidi hata jumatatu hatakuja shule na hatutaonana kwasababu siku hiyo alinyimwa hela na Babu yake mzee Samwel pamoja na kuchapwa sana huku akiambiwa amfuate mama yake'', alisema Maria paul [15]

Nae Bibi wa marehemu Juliana Samwel akizungumzia tukio hilo alisema baada ya kuchapwa na mjomba wake Kathe alichukua mafuta ya taa na kujimwagia mwili mzima na mengine akayanywa kisha akijiwasha na njiti ya kiberiti akawaka mwili mzima kiasi cha yeye kushindwa kumsaidia.

mwanangu mtoto aliungua karibu mwili mzima maana alikuwa amejiviringisha kanga toka chini mpaka juu nilipiga kelele majirani wakaja kuzima ule moto na kumbe alishaungua sana hata ngozi ilikuwa ikijichubua yenyewe, mzee Samwel angekueleza mengi lakini kaenda hospital kuuhifadhi mwili maana mama ya mrehema ndiyo leo anatoka Dar hivyo mazishi ni kesho mapema, kuhusu kifo sina cha kufanya imetokea imetokea nitafanyeje'', alisema. mama huyo wa umri kati ya 50/55

Kwa upande wa majirani walisema tukio hilo lilikuwa la kutisha na si la kawaida kuwahi kutokea imeonyesha watoto wa sasa siyo wa kunyanyaswa hovyo, wakatoa ushauri kuwa kila mwenye mtoto akae na mwanae asimuamini mtu ndiyo sababu ya watoto wengi hasa wa kike kuharibikawa kutokana na kukosa uangalizi.

MNADA BANNER