REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

ETI HAYA NI YA KWELI JAMANI!!!!?: WAUNGWANA WANADAI KUWA BIBIE HUYU NDIYE TISHIO LAKIM KARDASHIAN KATIKA SEKTA HII..TIZAMA PICHA MWENYEWE !!!!!

8:17:00 AM Add Comment

   Na Baba Juti  
#WatuWaMungu tayari Macho yao yameshaona na hii tunayokuambia ni kwa Mujibu wa Macho ya "Mafisi" hapa Duniani ambao wanafahamu Vizuri kabisa kuwa Yupi ni Mwanamke Mtamu na Yupi ni Mwanamke "kapa"

HUYU Binti anaitwa  LAUREN GOODER na ana Miaka 30, na ndiye ambaye hivi sasa anadaiwa kumtishia amani katika Sekta ya Muonekano wa Kutamanisha Haswa

Waungwana wanadai kuwa Mtu Wa Mungu huyu, Lauren, alifanya kazi nzito sana katika Kuutengeneza Muonekano wake huu ambao ulikuwa ni Kama Ndoto yake na hatimaye amefanikiwa, na Ndio Maana anauanika hadharani bila wasi wasi wowote Ule.

Hebu Tizameni Picha zake kwanza Waungwana....












FULL INTERVIEW: TULICHOJIFUNZA KATIKA INTERVIEW YA COYO ALIPOKUWA KWENYE KIPINDI CHA HIT ZONE (JEMBE FM 93.7-MWANZA)

8:00:00 AM Add Comment

Na Baba Juti & Natty E Brandy (JEMBE FM-Mwanza)
#WatuWaMungu Team HIT ZONE ya 93.7 JEMBE FM-Mwanza (Natty E Brandy & Baba Juti) Tulipata Nafasi ya kupiga "Stori" na Moja kati ya Rappers wa Kutizamwa sana katika Soko la Muziki wa Hip Hop, tunamzungumzia COYO (Zamani Coyo MC) ambaye hivi sasa anafanya Poa sana na Mkwaju wa ZIWAFIKIE

Haikuwa Tabu kwake Kujibu kila Swali ambalo Tulimuuliza, licha ya Kila aina ya Ugumu ambao alikutana nao katika Kujibu Maswali

Kuna Vitu ambavyo Tumefahamu zaidi kupitia Interview ambayo aliifanya. Alimzungumzia KID BWAY kuhusika katika Kazi zake, Track kuonekana haijakubalika zaidi kwa Baadhi ya Watu kama ilivyokuwa Nyma, na Nisher ambaye amhusika kama Director wa Video yake

   IKO HAPA YOTE   

WEEKEND: JUMANNE YA WIKI HII KUTOKA KATIKA KIPINDI CHA HIT ZONE (93.7 JEMBE FM-MWANZA), HIKI KILIFANYIKA PIA

7:22:00 AM Add Comment

   Na JEMBE FM  
#WatuWaMungu Wiki Ndo Hiyo Imekata..... Kama hukupata nafasi ya Kufuatilia kilichotokea Katika Kipindi cha HIT ZONE Kutoka JEMBE 93.7 MHz-Mwanza basi Kitulize Fresh

IMEKAAJE ni Kipengele ambacho Hukusanya Info Mchanganyiko Kutoka Ulimwenguni zote, ikiwa ni za Kuburudani, pamoja na Kijamii

Siku ya JUMANNE, Watangazaji wako NATTY E BRANDY pamoja na BABA JUTI, walishusha Info Kama Ifuatavyo


ETI NI KWELI? : RICH ONE ANADAI KUWA WASANII KUPANDA JUKWAANI WAKIWA NA MATAULO, WALIIGA KUTOKA NJE NA WALA HAKUNA UMUHIMU

7:15:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu tunafahamu Vizuri kabisa kuwa, Kila Ifikapo MEI 25, huwa ni Siku Maalum ya Kuadhimisha Siku ya Taulo Duniani, ikiwa Ni Njia moja wapo ya kumkumbuka na kuheshimu Mchango wa  Mwandishi wa Vitabu, Marehemu DOUGLAS NOEL ADAMS

Siku Hii hufahamika kama "DONT PANIC DAY" ambapo Matumizi ya Taulo hutumika kama Njia ya kujiamini na kuwa na Ujasiri popote pale unapoenda , hasa iwe kazini ama Shuleni, ama kwenye Shughuli Nyingine yoyote

Nchini Tanzani, kumekuwa na Baadhi ya Wasanii ambao walikuwa wakipanda Jukwaani wakiwa na Mataulo yao Begani, kitu ambacho tumeona kimekuwa kikifanyika na Bado kinaendelea kufanyika Kwa wasanii wengi wa Kimataifa

Katika Kuadhimisha Siku ya Taulo, tulichukua nafasi ya Kumtafuta moja kati ya Wasanii wa Kizazi Kipya ambaye pia alikuwa akipanda Jukwaani na Taulo, kutokea TMK WANAUME HALISI, RICH ONE, ambaye alifafanua kwa Uelewa Wake

Rich One alidai kuwa, Haikuwa na umuhimu ama Ulazima wowote kupanda na taulo Jukwaani , ila ilikuwa ni Fashion na kuiga Kwa Wenzetu kutoka Marekani

   MSIKILIZE    

ETI JAMANI !!!! : NI KWELI KIWANGO CHA BECKA TITTLE KIMESHUKA KWA SABABU HII?

3:09:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu kumekuwa na Ukimya na hata Kama anaachia Tracks , Basi Hazivumi kama ilivyokuwa awali, hasa kwa Msanii huyu wa Muziki wa Kizazi Kipya Hapa Nchini Tanzania (Bongo Fleva), BECKA TITTLE

Team Hit Zone tulipata Fununu kuwa kumekuwa na Baadhi ya wadau wa Muziki (Majina tunayaminya) ambao walikuwa wakidai kuwa, Kiwango cha Msanii huyu ambaye pia amewahi kuingia katika Kinyang'anyiro cha Tuzo za KTMA, kimeshuka kwa asilimia kubwa kutokana na kitendo cha yeye kushirikishwa sana na wasanii ambao wanachipukia (Nyie Mnawaitaga UNDERGROUNDS)

Baada ya kuyapata hayo, tukaona haina Ngenje, Wacha Tumsake Bwana Becka Tittle, ili atupe ukweli wa Hali halisi kama Hizo Fununu zina Ukweli Ndani yake, ama lah...
Huyu Hapa Mwenyewe anafafanua kiundani zaidi

KUDADADEKI !!!! : YULE BIBIE ANAYEDAIWA KUCHEPUKA NA T.I YUKO TAYARI KUMPA MTOTO?

2:50:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu Hii sasa ikizidi lazima tuitilie Mshaka kabisa, maana sio kwa kawaida Hii. Hivi Mnamkumbuka Binti anayeitwa BERNICE BURGOS?.....

Yeah !!!, ni Yule ambaye alikuwa akitajwa sana kuwa ndiye Mchepuko wa Rapper T.I , kitu ambacho kiliwafanya Wengi kuanza kujiuliza Maswali kama ni Kweli ama ni Uwongo…

Licha ya T.I kudai kuwa Yule “Mama La Mama” sio Mchepuko wake na wala hakuwa na Mpango naye, Mpya Zimeibuka kuwa Bibie huyo sasa, yuko tayari na anatamani sana kumpa Kumzalia Mtoto T.I

Moja kati ya Rafiki wa Karibu na Mwanamitindo huyo, anadai kuwa, Bernice tayari ana watoto, lakini bado anatamani kuwa na katoto ka kiume kwa hivi sasa

  Tunamnukuu  

“Bernice Burgos anapenda sana kuwa Mama. Unaweza kulibaini hilo hata ukimtizama tu, unagundua kila kitu, ingawa tayari ana watoto wawili ambao wote ni wa Kike. Mara nyingi amekuwa akitamani kuwa na motto wa kike, na kama hivi sasa yuko na T.I , unadhani kinafuata Nini?, any way Ninatania….lakini Mbali na masihala ambayo nimeyafanya, Bado Bernice anatamani  kuwa na motto wa Kiume na T.I, kwa sababu ni baba Bora. Mara Nyingi T.I anawajali watoto wake, na Bernice anadhani ingekuwa Poa zaidi kama angefanyiwa hivyo hasa kwa Mtoto wake wa Kiume”

CRISTIANO RONALDO : ANATARAJIA MTOTO?

2:37:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu Kuna kila dalili za dhati kuwa Msakata Soka kutoka kunako Club ya Real Madrid, CRISTIANO RONALDO na Mpenzi wake GEORGINA RODRIGUEZ wanatarajia Kupata Mtoto

Kwa Mujibu wa Picha ambayo Cristiano Mwenye Miaka 32 aliipost kunako account yake ya Instagram, inaonesha dhahili kuwa Mwanasoka huyo alikuwa ameshika Kitumbo cha Mpenzi wake, kilichokuwa kinaashiria kabisa kuwa lazima kuna kitu ndani yake.

Licha ya Wengi kumpongeza Cristiano kwa kuweka hadharani mahusiano yake Mapya na Georgina, bado kuna watu wenye “Jicho Korofi” waligundua kabisa kuwa bibie huyo ameshajazwa, na kuanza kushusha Comments za kuhoji kuhusu kile ambacho wanakiona kwa macho yao hayo Makali



Ronaldo na Georgina walikutana kwa Mara ya Kwanza Kule Central Madrid na ilikuwa ni June, wakati mwanasoka huyo akifanya Shopping katika Duka Kubwa la Bidhaa za GUCCI. Walianza kuonekana Hadharani November Mwaka Jana, kabla ya kuonesha dhahiri kuwa ni Wapenzi kupitia RED CARPET ya Tuzo za FIFA zilizofanyika ZURICH mnamo January Mwaka Huu

INASEMEKANA : MARIAH CAREY KUFUNGA NDOA KWA MARA YA PILI NA NICK CANNON.... HARUSI YAO SASA !!!

2:22:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu Lisemwalo lipo, na kama halipo basi Liko Njiani Ndukiiii, linakuja !!!!. Kuna taarifa kuwa Mariah Carey na Nick Cannon , wanandoa waliopeana Talaka Kipindi cha Nyuma, Wanapanga Kufunga Ndoa Nyingine tena Upya..katika Msimu  Wa Joto.

Mapema Ndani ya Mwezi huu, kuliibuka Taarifa kuwa  wawilio hao wamerudisha mahusiano yao Mapya ikiwa ni baada ya Mariah Carey kupigana Chini na “Mkata Viuno” wake Bryan Tanaka

Moja kati ya watu wa karibu kunako familia hiyo kimedai kuwa Ni kweli wawili hao wanatarajia kufunga Ndoa Kwa mara ya Pili ikiwa ni baada ya ile ya kwanza kuisha na talaka na itakuwa na Harusi kubwa sana

   Tunamnukuu  
“ Mariah atakuwa na Party huko ST. TROPEZ, ufaransa ama Italy katika eneo la Ukanda wa AMALFI. Harusi itaalika watu 500, akiwemo BEYONCE, Sir ELTON JOHN. Pia wanatarajia kuwa na Vinywaji Vingi ambavyo vitagharimu kuanzia USD 1000 kwa kila Chupa, pamoja na Keki kubwa itakayokuwa na Muonekano wa Dhahabu Original Kabisa “

Ukiachilia mbali vitu hivyo, Pia inasemekana Mariah Carey atavalia gauni lotakalogharimu USD 250,000 na litakuwa na Muonekano wa Madini ya Diamonds.

Na kama haitoshi, yeye mwenyewe atawaimbia Wageni Waalikwa .


Pia Mhabarishaji huyo aliongeza kuwa, Mariah Carey alidhihirisha kuwa anahitaji kuolewa tena na Nick Cannon ambaye ni Baba wa Watoto wao Mapacha.

USINIAMBIE !!!!: DRAKE AMEPEWA MASAA HAYA KUKIRI KUWA NI BABA HALALI WA MCHEZA NGONO HUYU

1:37:00 AM Add Comment

  Na Baba Juti  
#WatuWaMungu RAPPER  Drake yuko katika hati hati za kupandishwa Mahakamani endapo hatokubali kuwa Yeye ni baba Halali wa Mtoto wa Mwanamke Mcheza Ngono maarufu aliyestaafu, SOPHIE  BRUSSAUX.

Taarifa Mpya ambazo Team Hit Zone tumezinyaka Mpaka Hivi sasa, Drake amepewa Muda Mchache sana ili kukubali na kukiri kuwa yeye ni baba halali wa Mtoto na atatoa Mahitaji Maalum ya Mtoto kitu ambacho ni muhimu kuliko yote sababu yeye ni moja kati ya wahusika wakubwa katika Ujauzito alioupata Bibie huyo


Mpaka Hivi sasa, Sophie ameshatangaza Rasmi mwanasheria ambaye atasimama naye katika kuhakikisha kuwa Drake anafikishwa Mahakamani kama atakana kitu amcho kinaonekana Dhahiri kabisa kuwa motto huyo ni mali halali ya Drake

Mwanasheria huyo anatambulika kwa jina la RAOUL FELDER.


Ukiachilia mbali taarifa mpya hizi ambazo tunazimimina kwako, Drake aliwahi kuzungumziwa sana hasa kwa Kuwa Karibu na Sophie kipindi ambacho amepigana Chini na Mwanamama J-Lo, hali ambayo inathibitisha kuwa inawezekana kabisa Drake akawa alikunjuka na Mwanamama Huyu


Tofauti na Hilo, Sophie alianika wazi Mesej ambazo zilikuwa zikimuonesha Drake akimlazimisha Bibie huyo kutoa Mimba Yake, kitu ambacho Sophie hakukifanya hata Kidogo

MNADA BANNER