REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

Kristen Stewart alivyomsaliti Mpenzi wake Robert Pattinson na Director wake Rupert Sanders

5:30:00 AM Add Comment
















Na Frank M. Joachim
Yule Baby Mama wa TWILIGHT na SNOW WHITE kwa wale wataalamu wa Movie za Mbele, namzungumzia Bibie Kristen Stewart, amedakwa na wadaku wa hukooooooooooo...akila Maraha ya kimahaba na Director wake katika Movie ya SNOW WHITE na HUNTSMAN kisiri siri
Picha Zenyewe ziko hivi...Kodolea Uone..


Hapa ni Kristen Stewart na Mpenzi wake Robert Pattinsons kabla ya Skendo na Director wake.

Kristen (Katikati), akiwa na Director wake ambaye amefanya naye usaliti, Rupert Sanders, wakti wa kutengeneza Filamu ya "SNOW WHITE"


Kristen Stewart na Rupert Sanders katika Pozi. Hii ilikuwa ni safari ya kuelekea kwenye Uhusiano wao wa kisiri siri...yaani usaliti

Kristen Stewart na Rupert Sanders walipofumwa katika Mgahawa wakila bata....ilikuwa ni dalili ya......
malizia

Hayawi hayawi...yakatimia.Hapa Kristen Stewart akiwa katika Mahaba Mazito ya usaliti na Director wake Rupert Sanders, Baba wa watoto wawili, mwenye watoto wawili na Mke wake mmoja, huku akikabiliwa na Umri wa miaka 41.
Weeeh...Chezea Director wewe?...Hapa Kristen akiwa mule mule katika Maraha ya makopa na Director wake Rupert..Rahaaaa...Utamu...

Hapa wakitoka kwenye Mkoko wao baada ya Kupeana maraha, mazaga zaga na Makachumbari ya Kimahaba.

Ajabu na Kweli...Mahaba yakahamia Nje...hapa Rupert Sanders akiwa amekumbatia Vilivyo Kristen Stewart....
He!...Si yakaanza upya Tena?
(Picha Zote kwa Hisani ya jarida la US WEEKLY)

Director Rupert Sanders akiwa na familia yake (Kabla hajamsaliti mke wake na Kristen Stewart)






UGONJWA WA EBOLA UNAVYOWATESA WANANCHI WA UGANDA

4:13:00 AM Add Comment
Watoa Huduma wakimhudumia Muathirika wa Ugonjwa wa Ebola,
Nchini Uganda.

Raia Mwanamke wa Uganada akiwa Hospitali baada ya Kuambukizwa Ugonjwa Wa Ebola, unaoanza kusambaa Nchini uganda

Rai wa Uganda akiwa na hali mbaya baada ya kuambukizwa ugonjwa wa Ebola ulioibuka Tena Nchini Uganda.

Wahudumu wa Hospitali moja ya Uganda wakiwa na Mgonjwa wa Ebola Nchin humo.

Wataalamu wa Afya Nchini Uganda wakidhibiti Virusi vya Ebola





6 walazwa baada ya kuugua Ugonjwa wa Ebola

3:51:00 AM Add Comment












Mgonjwa Wa Ebola




Rais Wa Uganda, Yoweri Kagutta Museveni






Na Frank M. Joachim




Watu sita zaidi wamelazwa hospitalini kwa kushukiwa kuwa wameambukizwa virusi hatari vya Ebola Magharibi mwa Uganda. Ugonjwa huo hatari ulizuka wiki tatu zilizopita. Inaripotiwa kuwa vijiji vingi katika eneo hilo sasa vimeathirika. Wizara ya Afya ya Uganda na Shirika la Afya Ulimwenguni WHO zilithibitisha mwishoni mwa wiki kuwa virusi hivyo vimewaua watu 14 mwezi huu. Rais wa Uganda Yoweri Museveni jana pia alithibitisha kupitia vyombo vya habari kuwepo ugonjwa huo na kuwataka watu kuepuka kugusana ili kuepukana na hatari ya kuambukizwa. Hakujakuwa na visa vilivyothibitishwa vya maambukizi kuenea katika mji mkuu Kampala. Uganda imewahi kukumbwa na matukio matatu ya kuzuka ugonjwa wa Ebola katika kipindi cha miaka 12 iliyopita. Kisa kibaya zaidi kilikuwa mnamo mwaka wa 2000 ambapo watu 425 waliambukizwa. Zaidi ya nusu yao waliaga dunia. Hakuna chanjo ya kuzuia ugonjwa huo kufikia sasa.




P.Diddy Afunika kwa Utajiri

3:34:00 AM Add Comment








Sean John Combs "P. Diddy"


A new list of hip hop's wealthiest stars has reaffirmed Diddy's status as the world's most valuable rapper. The list of 20 artists and moguls, published by Celebrity Net Worth, places the Bad Boy Records founder at the top with a personal net worth of $500 million. Jay-Z follows closely behind with a net worth of $475 million.

The list echoes the findings of another report published earlier this year by Forbes, which also had Diddy and Jay in the one and two spots. The Celebrity Net Worth list is more extensive, however, and also includes Master P ($350 million), Eminem ($120 million) and Rick Ross ($25 million).

See the full list below:

#20 Rick Ross – Net Worth $25 Million
#19 Tie between T-Pain and T.I – Net Worth $30 Million
#18 Nelly – Net Worth $55 Million
#17 Busta Rhymes – Net Worth $60 Million
#16 Ludacris – Net Worth $65 Million
#15 Beastie Boys – Net Worth $75 Million Each*
#14 Timbaland – Net Worth $75 Million
#13 Pharrell Williams – Net Worth $77.5 Million
#12 Tie between LL Cool J and Akon – Net Worth $80 Million
#11 Kanye West – Net Worth $90 Million
#10 Lil Wayne – Net Worth $95 Million
#9 Ice Cube – Net Worth $100 Million
#8 Snoop Dogg – Net Worth $110 Million
#7 Birdman – Net Worth $115 Million
#6 Eminem – Net Worth $120 Million
#5 50 Cent – Net Worth $250 Million
#4 Dr. Dre – Net Worth $260 Million
#3 Master P – Net Worth $350 Million
#2 Jay-Z – Net Worth $475 Million
#1 Diddy – Net Worth $500 Million

Kanye Plans to propose to kim Kardashian

2:09:00 PM Add Comment





Kim Kardashian na Kanye west



In the latest Kimye news, Kanye West is reportedly planning to propose to Kim Kardashian as soon as her divorce is final.
Now given that Kim’s relationship with Kanye has lasted longer than her 72-day marriage to Kris Humphries, it isn’t clear whether Mr. West’s supposed plan should be congratulated or seen as utterly insane.
But sources said  that he has already asked his personal jeweler to design an engagement ring for Kim, which will incorporate diamonds and rubies from his late mother Donda’s jewelry collection.
If reports are wrong, there have been other clues that also hint to a possible engagement, like the diamond ring West gave Kim back in June and the expensive Lambo that Kim brought him for his birthday.
Now, as crazy as many Hollywood hook-ups go, the Kimye world-wind romance goes right along with the program… of insanity. But to use this space to blast young and, well, ignorant love such as theirs is futile. Whatever’s going to happen will happen whether we scream “DON’T DO IT, KANYE!!!!” or not. So, all that can be said is God speed and good luck.”

"SASA NI ZAMU YA KICHUPA CHA NO SAY"-KACCI

1:29:00 PM Add Comment
 





 Young Rapper anayetamani anayekuja Kwa kasi katika Music Industry hapa Bongo, Aboul Mrisho "Kacci The Town Son'" a.k.a "Kaccilionaire", amedhihirisha kuwa Video ya ngoma yake Mpya kabisaaa yenye Title la "NO SAY" itakuwa Matata ile Balaa
Akipiga stori na Blog hii, Mkali huyo ambaye kwa sasa anakita na Track balaa ya " HOLLA AT YO NIGGAH" iliyepikwa na Producer GQ kutoka Mji kasoro bahari, amesema kuwa watanzania wasubiri mapinduzi ya dhati katika Ngoma hiyo mpya ambayo amemshirikisha mmoja kati ya Memba wa kundi la "Mtu Chee", Country Boy, huku akisisitiza kuwa anaamini Track hiyo itakuwa moja kati ya Headlines kunako Media kibao

"Nafanya video ya nyimbo yangu tarehe kumi na moja ngoma inaitwa NO SAY nimefanya na COUNTRY BOY studio ni DIGITAL VIBES producer GQ na Video Company ni Revolution Videos so niko kwenye maandalizi"

Katika Video hiyo ambayo inatarajiwa kufanyiwa "mandingo" mida si mingi, itakuwa chini ya Usimamizi na Uongozaji wa  GEORGE NDUNGURU ambaye yupo katika Kampuni mpya ya REVOLUTION VIDEOS.
Kacci The Town Son still anasababisha Headlines na Ngoma kama Vile Holla At Your Niggah, Haters Going Down, I like That na Butterfly ambazo zote zimetengenezwa haswa na GQ, katika Lebo ya RACERS.
Stay with joachimjunior.blogspot.com ili kujua kila step
Mauaji ya Balozi wa Venezuela Nchini Kenya....Uba

Mauaji ya Balozi wa Venezuela Nchini Kenya....Uba

12:43:00 AM Add Comment
Nyumba ya balozi wa Venezuela mjini nairobi
Ubalozi wa Venezuela Nchini Kenya (Picha na REUTERS)

 Na Frank M. Joachim

Polisi wa Kenya wanasema kuwa wanaendelea na uchunguzi, juu ya mauaji ya balozi mpya wa Venezuela nchini humo, ambaye aliuwawa Ijumaa.
Olga Fonseca, aliyeanza kazi Kenya kati ya mwezi Julai, alikutiakana ameuwawa nyumbani kwake, na watu sita wamekamatwa hadi sasa.
Watu hao sita wamekamatwa siku mbili tu baada ya balozi huyo kupatikana amefariki nyumbani kwake.
Siku ya Ijumaa, polisi walisema kuwa maiti ya Bi Olga Fonseca ilipatikana kitandani mwake lakini sababu za kuuwawa kwake hadi sasa hazijulikani.
Bila ya kutoa maelezo zaidi, polisi wamesema kuwa wanawashikilia watu sita kuhusiana na kifo cha balozi huyo.
 Taarifa kutoka wizara ya maswala ya njee ya Kenya imesema kuwa wafanyikazi katika makaazi ya balozi huyo waliwasilisha malalamiko yao kwa polisi baada ya kufutwa kazi hivi majuzi.
Inadaiwa kuwa bi Fonseca aliwafuta kazi baada ya wao kukataa kuondoa malalamiko kuhusu madai ya kunyanyaswa kijinisia na mtangulizi wa balozi huo.
Hata hivyo polisi wamesema wanachunguza madai hayo

Papa Afungukia Mauaji ya Syria

12:36:00 AM Add Comment




Papa Benedicto XVI
 Na Frank Joachim Kwa Msaada wa DW.

Baba Mtakatifu Benedikto wa 16 amerejea wito wake kwa Jumuiya ya Kimataifa, wa kumaliza machafuko nchini Syria, huku akiyataka mataifa makubwa kutosita katika juhudi za kumaliza mgogoro huo. Baada ya kutoa baraka kwa waumini wake huko Castel Gandolfo, kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani amesema anafuatilia kwa karibu ghasia hizo na ameziomba nchi jirani kuwapokea wakimbizi na kuwapa msaada wote wanaouhitaji. Ameshauri njia ya majadiliano itumike ili kufikia suluhisho la kisiasa kwa amani.   Na taarifa kutoka Jordan, zinasema kuwa serikali hiyo imefungua kambi yake ya kwanza kwa maelfu ya wakimbizi wanaokimbia ghasia nchini Syria. Kambi hiyo ya Zaatari iliyojengwa kwa maturubali iko jangwani, jirani na mji wa Mafraq na ina uwezo wa kuwahifadhi wakimbizi 120,000. Baada ya kuzinduliwa kwa kambi hiyo na serikali ya Jordan na Umoja wa Mataifa, Waziri wa Mambo ya Nje, Nasser Judeh amesema hatua hiyo ni sehemu ya  msaada wa nchi yake kwa Wasyria hao wasio na makazi, ambao wanaingia Jordan kwa makisio ya watu 2,000 kwa siku. 

YANGA MULE MULE

2:31:00 AM Add Comment

wachezaji wa Yanga wakishangilia Goli lao la Kwanza dhid ya APR ya Rwanda, katika Mchezo wa Nusu Fainali katika Uwanja wa Taifa.

 
Klabu Machachari na Bingwa Mtetezi wa Kombe la CECAFA KAGAME CUP, hatimaye wameonesha ubabe na nia ya kutaka kubakiza ubingwa wao kwa mwaka huu, bada ya kukwangua APR ya Rwanda Bao 1-0
Hamis Kiiza ndiye aliyeinua shangwe za Wanajangwani hao katika dakika 15 za awali za Muda wa Nyongeza, yaani dk 30 za Nyongeza
TAMKO LA IDARA YA USALAMA TAIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAMKO LA IDARA YA USALAMA TAIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

2:19:00 AM Add Comment

Katika siku za hivi karibuni, kumejitokeza taarifa zenye tuhuma kadhaa dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa.

Taarifa hizo zimekuwa zikitolewa kwenye vyombo vya habari zikiihusisha Idara hii na matukio ambayo yanaidhalilisha na kuzua maswali mengi kwa wananchi. Kati ya tuhuma hizo ni tukio la kutekwa kwa Dr. STEPHEN ULIMBOKA, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari na madai ya kufanywa kwa mipango ya kuwadhuru baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Upinzani.

Gazeti moja la kila wiki limekuwa likurudia tuhuma hizo mara kwa mara kwa madai kwamba ni habari za uchunguzi na kuihusisha Idara.

Idara inataka kuwahakikishia wananchi kwamba taarifa hizo ni za UZUSHI NA UONGO ambazo zina nia ya kuharibu jina na sifa ya Idara. Taarifa hizo zimekuwa zikiunganishaunganisha vipande vya taarifa mbalimbali ili kukidhi malengo yaliyokusudiwa na wanaolitumia gazeti hilo. Idara haikuhusika wala haihusiki na matukio yoyote yaliyotajwa katika tuhuma hizo. Hivyo tunawaomba wananchi wazipuuze taarifa hizo.

Matukio yaliyotajwa katika tuhuma hizo yanachunguzwa na Jeshi la Polisi ambacho ndicho Chombo Chenye Dhamana, na kwa Maslahi ya Taifa si vizuri kuachia upotoshaji huo uendelee.

Aidha, tunapenda kuwahakikishia Watanzania kuwa uzushi na tuhuma zinazotolewa dhidi ya Idara hazitatuvunja moyo bali zitatuunganisha na hivyo kutuimarisha katika azma yetu ya kuhakikisha nchi yetu inaendelea kubaki salama kwa kushirikiana na wanachi na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama.

Imetolewa na Idara ya Usalama wa Taifa,

Makao Makuu,

DAR ES SALAAM

ALIYEPANGA KUMUUA MANDELA AFIKISHWA MAHAKAMANI.

2:06:00 AM Add Comment










Mahakama nchini Afrika ya Kusini imemtia hatiani kiongozi wa kundi lenye itikadi kali za ubaguzi wa rangi la Boer Army ya kutaka kuipindua serikali iliyokuwa inaongozwa na Rais wa zamani Nelson Mandela mwaka 2002.
Nelson Mandela


Kiongozi huyo aliyekuwa mhadhiri wa chuo kikuu nchini humo Mike du Toit, alipanga kumuua Mandela kwa mashambulizi ya mabomu kisha aungóe madarakani utawala wa watu weusi. Kesi hiyo imedumu kwa miaka tisa. Hukumu yake inatarajiwa kutolewa mwezi ujao na huenda akakabiliwa na kifungo cha maisha jela.

Wafuasi wengine 21 wa kundi hilo hukumu zao zitatolewa wiki chache zijazo. Jaji Eben Jordan aliyeendesha kesi hiyo amesema kuwa mashahidi wameeleza namna kundi hilo lilivyopanga kufanya mauwaji hayo. Lilipanga pia kuwaua kwa risasi raia weupe wa nchi hiyo wanaounga mkono utawala wa watu weusi.

Swagg Touchez

8:02:00 AM Add Comment
Noorja Ibrahim, among of ma Best friends from RCT, enzi hizo tukiishi Hostel moja na Kusoma Chuo kimoja. I miss those Days.
Lilian Lucian Kikoti. Huwa namkumbuka sana coz she is My best Friend from O Level at St. Anne marie Academy.
Now anakomaa na Life lake kama kawa coz anapenda kuwa Hard working, na aliwahi kunitabilia Makubwa sana in my talents
Thanx alot Lizzle, May Lord bless You
My College Fanz ambao ni moja kati ya Watu ambao huwa nawakubali saaaana wakikaa nyuma ya Mashine...yani Mixer na Mic na Vitu Kibaaaaaaaaao
Kulia ni Cloudian Mchunguzi na Patrick Mengo
Mic u Hommies


My Brother, Awadh Mnyika. He is the Role Modal to me coz of his kindness, charming, Understanding, and Mostly caring.
Amenisaidia Mambo Mengi sana..na ndo most supporter katika Suala zima la Internet na kubuild this Blog kila siku.
Our Good times ni pale wakati tunapiga Msosi huku tunacheki Muvi...weeeeeh, noumar



Joshua Kibona, From Neema Hostel
Jembe langu la Uhakika....Addicted to movie
Much respect Bro!!
Kuanzia Kulia ni Jombaa Peter Mpaki, Hubert Kiwale, na Patrick Mengo
Mic u Hommies




35 Wafariki kwa Mafuriko Nigeria

1:07:00 AM Add Comment

Mafuriko makubwa yamelikumba eneo la katikati ya Nigeria na kuuwa watu 35. Mvua kubwa ilinyesha kwenye jimbo la Plateau usiku mzima wa jana na kuharibu nyumba 200.

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan


Shirika la msalaba mwekundu kwenye eneo hilo linaripoti kuwa miili hiyo imeshapatikana akiwemo mzee wa miaka 90 pamoja na mtoto wa miezi mitatu. Mkuu wa shirika hilo Manasie Phampe amesema kuwa huenda idadi hiyo ikaongezeka. Mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa pamoja na maji kutoka kwenye bwawa lililofurika yalivisomba vijiji kadhaa kwenye eneo la Jos ambalo ni makao makuu ya jimbo la Plateau. Miili mengine 25 bado inatafutwa huku mingi kati ya hiyo ikiwa ni ya watoto wenye umri wa miezi mitatu hadi miaka 13 ambao walisombwa wakiwa usingizini.

Nigeria kwa sasa iko kwenye msimu wa mvua za mwaka ambazo zimekuwa zikija na madhoruba yanayotoa changamoto kwa maisha ya watu na miundombinu. 

Mmoja wa Waathirika wa Mafuriko katika Nchi ya Nigeria




















Wiki iliyopita watu watatu walikufa kutokana na mafuriko kaskazini mwa Lagos kwenye eneo la Ibadan. Mwaka jana pia watu 120 walikufa kwa mafuriko kwenye eneo hilo.

SYRIA- Ni kweli Tuna Siraha za Kemikali

12:55:00 AM Add Comment






Syria imekiri kwa mara ya kwanza kuwa inamiliki silaha za kemikali na kibaolojia ambazo ingezitumia kama mataifa ya nje yangeivamia kijeshi.

 Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya nchi hiyo Jihaddi al-Makdissi amewaambia waandishi wa habari kwenye mkutano kuwa kamwe silaha hizo haziwezi kutumika dhidi ya waasi lakini zinaweza kuzitumiwa kujibu mashambulizi kutoka nje.

Bashar Al Asad, Rais Wa Syria

 Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Guido Westerwelle amesema kuwa kitendo hicho cha kutishia kutumia silaha kama hizo ni cha kushitua. Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amesema kuwa ana wasiwasi mkubwa kuwa huenda Syria ikashawishika kuzitumia silaha hizo. 

Nchi hiyo haijasaini mkataba wa kimataifa wa mwaka 1992 unaokataza kutengeneza, kutumia au kuwa na shehena ya silaha za kemikali. 

Hapo siku za nyuma, maafisa wa nchi hiyo walikana kuwa na silaha za aina hiyo.  

50 Cents Ageukia Upromota Wa Bondia

12:23:00 AM Add Comment











Mnamo Mwezi April Mwaka Huu, Bondia Maarufu sana Nchini Marekani, Floyd Maywether alichonga na Jarida la XXL la nchini Marekani kuwa Mkali wa Hip Hop na Big Bous Wa G- UNIT, Jackson Cartis goes by tha a.k.a ya 50 Cents, anajaribu kuchumpa kwenye suala zima La Masumbwi maaruf kama Boxing katika Lugha ya Wenzetu
"Katika upande wa Boxing, nahisi Mshikaji utakuwa katika upande wa Upromota"..alinena Maywether
 Sasa Basi....Taarifa zinabainisha kuwa, Mkali huyo wa 'Get Up', ameingiza jina lake katika usajili wa Mapromota
50 Cents akiwa na Maywether


Vyombo mbali mbali vinalipoti kwamba 50 ameanzisha  "TMT Promotions"—kifupisho cha "The Money Team" ambayo tayari ishapata Leseni Jijini New York na yuko kwenye process a kuomba leseni pia katika Jiji la Nevada.

DIAMOND PRIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII MPAKA TAARABU

6:56:00 AM Add Comment








BAADA ya kutamba kwa muda mrefu katika muziki wa kizazi kipya nchini, msanii nyota wa muziki huo, Naseeb Abdul ‘Diamond’ amesema anafikiria kujitosa katika muziki wa taarab.
 

Naseeb Abdul "Diamond Platnum"

Diamond alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, amefikia uamuzi huo kutokana na kuvutiwa na muziki huo wa taarab.
Mshindi huyo wa tuzo mbalimbali za muziki za Kilimanjaro amesema, anajua uamuzi wake huo utawashangaza mashabiki wengi, lakini ni jambo la kawaida kwa msanii.
 

Diamond alisema hadi sasa anaamini hana mpinzani katika muziki wa kizazi kipya na hakuna msanii anayeweza kufikia kiwango chake hapa nchini.
“Najua watu watanishangaa na kuniona mtu wa ajabu, lakini nimefanya hivyo kwa sababu sina mpinzani katika muziki wa kizazi kipya,”alisema.
Diamond alisema ameamua kupiga miondoko tofauti ya muziki kutokana na kipaji alichonacho katika fani hiyo, ambayo imempatia umaarufu mkubwa.
Kutokana na kipaji chake hicho, Diamond alisema hakuna kitu anachoshindwa kukifanya katima muziki.
“Bado sijaanza rasmi kupiga muziki wa taarab, ninachokifanya kwa sasa ni kufanya tathmini ya soko lake ili kuona kama unaweza kuniletea mafanikio kama ilivyo kwa muziki wa bongo fleva,”alisema msanii huyo.
“Naweza kufanya kila aina ya muziki kwa sababu nina kipaji cha kuimba nyimbo aina zote, hivyo endapo nitafikia muafaka, naweza kufanya kitu hicho ingawa mashabiki wangu watashtuka sana,” alisema.
 

Diamond alikiri kuwa, muziki wa kizazi kipya umemfanya ajulikane sehemu nyingi duniani, ikiwa ni pamoja na kupata manufaa mbalimbali kimaisha kwa kuishi kwenye nyumba nzuri na kumiliki magari ya kifahari.
Msanii huyo mwenye haiba ya kuvutia alisema, kwake muziki ni kazi kama zilivyo kazi zingine hivyo amekuwa akifanya kazi zake kwa malengo.
Alisema siri kubwa ya muziki wake kuwateka mashabiki wengi ndani na nje ya nchi ni kufanyakazi zake kwa kujituma na pia kujiwekea malengo.
"Sifanyi muziki kwa ajili ya kujifurahisha, kutafuta pesa na kuwaacha mashabiki wangu wabaki na kiu ya burudani,”alisema Diamond.
“Ninapofanya muziki nahakikisha kuwa, nakata kiu ya mashabiki wangu kwa kuwapa burudani wanayoihitaji,”aliongeza.
Katika kufanikisha hilo, Diamond alisema amekuwa na utaratibu wa kushirikiana na watu mbali mbali kwa vile anaamini sio rahisi kuweza kufanya kila kitu peke yake.
Pia Diamond Ameongeza Kuwa miongoni mwa watu, ambao wamekuwa wakimpa ushirikiano mkubwa katika kazi zake ni wacheza shoo kwa vile wamekuwa wakibuni vionjo vipya kila kukicha.
"Siwezi kuwa na ubahili ninapofanya kazi na hili ndilo lililonifanya nizidi kusonga mbele katika kazi ya muziki. Ili upate ni lazima utoe na ili uwafurahishe mashabiki wako ni lazima uzingatie kanuni hizo,”alisema.

UBAYA UBAYA ya DJ. Nas Yafanyika...

6:49:00 AM Add Comment









DJ Maarufu mkoani Iringa Nickson Sanga ari maarufu DJ NAS  wa Iringa ameanza zoezi la kurekodi video yake inayokwenda kwa jina la Ubaya ubaya.
Mzigo huo unasimamiwa fresh na Kampuni ya Show Biz Difine inayomilikiwa na msanii Mike Mwakatundu a.k.a Mike T.
 
 
.














 
 
Dj Nasi akiwa na Video Modals wakati wa Making te Video

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 Dj. Nasi Katika Mzigo.......

MNADA BANNER