REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

Riyad yupo Jordan

4:55:00 AM Add Comment

Riyad Farid Hijab


Na Frank M. Joachim & DW


AMMAN, Jordan imethibitisha kuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Syria Riyad Hijjab aliyeasi utawala wa Rais Bashar al-Assad yuko nchini humo. Shirika la habari la nchi hiyo, Petra, limemnukuu msemaji wa serikali, Samil al-Mayata akisema kuwa Hijjab na familia yake waliwasili jana jioni. Mayata alikanusha uvumi ulioenea kuwa kiongozi huyo aliingia nchini humo siku ya Jumatatu. Msemaji wa Hijjab , Mohammed Atari amesema kuwa bosi wake alisubiri hadi Jumanne usiku ndipo avuke mpaka kuingia Jordan kutokana na ulinzi mkali uliowekwa kwenye eneo hilo na vikosi vya Syria. Wakati huohuo nchini Syria mapambano ya kuwania mji wa Aleppo yanazidi kupamba moto. Hapo awali vikosi vya serikali vilitangaza kulidhiti eneo la salahidini lakini muda mfupi baada ya taarifa hiyo waasi walikanusha. Hii leo Iran imeandaa mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni kwa ajili ya kuujadili mzozo wa Syria.  Rais Mahmoud Ahmadinejad anajaribu kuzima mtazamo hasi wa mataifa ya magharibi na baadhi ya yale ya kiarabu dhidi ya nchi yake kuhusu mzozo wa Syria.

HATIMAYE LIBYA KIMEELEWEKA

4:50:00 AM Add Comment
Mustafa Abdel Akikabidhiwa Madaraka



Na Frank M. Joachim & DW

Takribani mwaka mmoja tangu kuondolewa madarakani kwa aliyekuwa Rais wa Libya Kanali Muammar Gaddafi, Baraza la Mpito nchini humo limekabidhi madaraka kwa bunge jipya la nchi hiyo. Kwa heshima ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, sherehe za kukabidhi madaraka zilifanyika usiku wa jana. Muda mfupi baada ya tukio hilo, nderemo na vifijo vilisikika kwenye mitaa ya mji mkuu wa Tripoli huku fataki zikirushwa angani. Raia nchini humo wamesikika wakisema kuwa "Libya itakuwa nchi huru na yenye demokrasia siku zote". Bunge hilo lenye wabunge 200 litafanya kazi ya kumchagua Waziri Mkuu ambaye ataunda serikali. Bunge hilo litatunga sheria ambazo zitaiweka Libya kwenye uchaguzi kamili wa bunge baada ya kuandikwa kwa katiba mpya hapo mwakani. Chombo hicho kilichaguliwa mwezi uliopita katika uchaguzi wa kwanza huru na wa haki tangu kuondolewa kwa Gaddafi. Wabunge wanatoka kwenye vyama vya siasa na wabunge wa kujitegemea.

WALEMAVU MOSHI, NEEMA HIYOOOOO

4:45:00 AM Add Comment

MOSHI





MOSHI
Na Edwin Moshi

ZAIDI ya walemavu 200 wanatarajia kunufaika na mafunzo juu ya namna ya kuwa wajasiriamali na namna ya kupambana na virusi vya ukimwi.
Mafunzo hayo ambayo yatawajumuisha walemavu wa viungo yanatarajia kuanza hivi karibuni kwa kuzijumuisha wilaya tatu ikiwemo wilaya ya Rombo,Moshi vijijini na Manispaa ya Moshi.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo hiki ofisini kwake jana,Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Indigo Women Link lenye makao yake makuu jijini Dar es saalam dr.Rosemary Daniel alisema lengo la kutoa mafunzo hayo kwa kundi hilo ni kutokana na kundi la walemavu kusahaulika katika masuala mtambuka.

Dr.Rosemary amesema suala la kumsaidia mlemavu kwa kumpatia mafunzo ya namna ya kujikwamua kiuchumi na kifikra juu ya ugonjwa wa ukimwi na virusi vya ukimwi ambapo kutawawezesha kujikinga na maambukizi mapya.

Ameongeza kuwa,kwa kuwapatia mafunzo hayo,kutawawezesha kujiunga na kuanzisha vikundi vya biashara ndogondogo kwa kuzingatia aina ya ulemavu walionao ili waweze kujipatia kipato.

Aidha amewataka viongozi wa kata na vijiji kutoa ushirikiano kwa kuwapatia taarifa walengwa ili wote waweze kushiriki mafunzo hayo na kuongeza kuwa matarajio yao ni kuwapatia elimu walemavu zaidi ya 400 baada ya mafunzo ya awamu hiyo.

HONGERA SERIKALI KWA HILI!!!

4:42:00 AM Add Comment





Makete
Na Edwin Moshi.

Baadhi ya wakazi wa Makete mjini wameipongeza serikali kwa kufanya ukarabati wa barabara za mitaa huku wengine wakiukosoa uamuzi huo wa serikali

Wakizungumza na mwandishi wetu wakazi hao wamesema zoezi hilo la ukarabati wa barabara hizo umekuja wakati muafaka kani barabara hizo zimesahaulika kwa kutofanyiwa matengenezo kwa muda mrefu hali iliyosababisha mitaro ya barabara hizo kuziba na maji kupita juu ya barabara hizo wakati wa masika na kusababisha uharibifu mkubwa

Mmoja ya mkazi wa makete mjini aliyejitambulisha kwa jina Obeth Sanga amesema kutokana na barabara hizo kutofanyiwa matengenezo ya muda mrefu kumepelekea baadhi ya wakazi wa makete mjini kumwaga vifaa vya ujenzi kwenye mitaro ya barabara hizo na kuviacha kwa muda mrefu hali inayoharibu barabara hizo

“Hebu fikiria mtu unaleta mchanga au mawe ya kujenga halafu unaviacha kweye mitaro kwa muda mrefu, mvua zikianza maji yanakosa pa kwenda yanapita juu ya barabara na kuziharibu halafu wao wao wanaanza lawama kwa serikali” amesema Sanga

Katika hatua nyingine wakazi hao wameilaumu serikali kwa ukarabati huo na kusema umekuja wakati ambao kuna vumbi hivyo zoezi hilo linazidi kuongeza vumbi

Monica Mahenge ambaye ni mkazi wa Makete amesema ujenzi huo kwa hivi sasa hauna tatizo isipokuwa baada ya wiki moja vumbi litazidi hivyo kuongeza adha kwa wananchi, hivyo ameshari ujenzi huo ungesubiri angalau mwezi Novemba ambapo ni karibu na msimu wa mvua

“sawa wanamwaga maji kwenye hizi barabara na vumbi linaondoka kabisa lakini baada ya wiki moja vumbi linajaa kama mwanzoni, yaani ni bora wangesubiri karibu na masimu wa mvua ndio wajenge, halafu kwa sasa magari mengi yanapita huku hayapiti kule kwenye barabara kuu kwani wanakwepa matuta, yaani vumbi litatumaliza” alisema Bi. Monica

Halmashauri ya wilaya ya Makete ipo kwenye utekelezaji wa kukarabati barabara za mitaa ambazo zimesahaulika kwa mda mrefu, kama ilivyokuwa ikilalamikiwa na wananchi wengi kuwa barabara hizo ni mbovu

MARUFUKU VIONGOZI KUWASUMBUA WANANCHI KWA MICHANGO KTK SENSA- RC IRINGA

4:41:00 AM Add Comment


MKUU WA MKOA WA IRINGA, DR. CHRISTINE ISHENGOMA



Iringa
Na Edwin Moshi

WAKATI maandalizi ya sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika usiku wa Agosti 25 kuamkia Agosti 26 mwaka huu yakiendelea kuchukua kasi hapa nchini , mkuu wa mkoa (RC) wa Iringa Dkt Christine Ishengoma amepiga marufuku viongozi kuwa kuwasumbua wananchi kwa michango kwa kipindi hiki cha kuelekea katika zoezi la Sensa ya watu na makazi.

Pia atangaza kumchukulia hatua kali ya kisheria kiongozi yeyote ambaye atabainika kuomba fedha kutoka kwa wananchi pindi anapokuwa katika majukumu yake ya kuhamasisha zoezi la sensa .

Dkt Ishengoma alitoa agizo hilo leo alipozungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake na kudai kuwa ili kufanikisha zoezi hilo la Sensa ya watu na makazi katika mkoa wa Iringa amelazimika kusimamisha michango yote ya maendeleo kwa wananchi ili kuwaondoa na hofu mbali mbali juu ya michango hiyo na badala yake kujiandaa kwa kuhesabiwa pekee.

Hatua ya mkuu huyo wa mkoa wa Iringa kupiga marufuku viongozi kuchangisha wananchi michango mbali mbali ya kimaendeleo imekuja baada ya kuibuka kwa vitendo vya baadhi ya viongozi kuidaiwa kupita kwa wananchi na kukusanya michango ya maendeleo huku baadhi ya wananchi wakianza kuingiwa na hofu kuwa yawezekana viongozi hao wakatumia siku hiyo ya sense kuwakamata kwa kushindwa kulipa michango.

Alisema kuwa ni vema kwa kipindi hiki cha kuelekea katika zoezi hilo la sensa viongozi wa vijiji,mitaa kata na wilaya kuachana na mpango wa kupita kwa wananchi kuchangisha michango hiyo ama kuhamasisha juu ya wananchi kuchangia miradi ya maendeleo ili kuwafanya wananchi hao kujiandaa kwa kuhesabiwa pekee.

MNADA BANNER