REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

MEKUZI: MWANAFUNZI HUYU MREMBO, APOKEA KICHAPO KWA WIZI WA........

3:37:00 AM
 HURUMA: Binti Murembo akiwa Chini ya Ulinzi wa Wananchi baada ya Kuwiba Viatu....

NGOJA NIMTAFUTE BABY: Akibofya Simu kuwasiliana na Honey wake ili amsaidie kulipa Deni

Tukio la mrembo  huyo  kupokea  kichapo na kuvuliwa  nguo na  kupokonywa  simu yake na mikoba zaidi ya mitano  pamoja na kiasi cha TSh 15,000 ambazo alikuwa amezihifadhi limetokea  jumapili  wiki hii katika  eneo la Miyomboni mjini Iringa.

Akielezea juu ya mkasa  huo  wa aina yake  leo mfanyabiashara   huyo  mama Masawe  alisema kuwa eneo  hilo amekuwa na kawaida ya  kuibiwa  viatu katika  duka  lake la viatu  vya mtumba .....

Mama  huyu  anadai    kuwa  mbali ya  kukamatwa kwa mrembo  huyo  bado amepata  kukamata  vijana  zaidi ya  wawili watanashati ambao  wamekuwa wakifika na kujifanya wakichagua viatu na  kuishia  kuiba na kutoweka .

Binti   huyo ambaye  ni  mwanachuo   alifika  dukani hapo   na  kuanza kuchagua  viatu akijifanya  ni  mteja .....

Baada  ya  kuona  muuza  duka  ameangalia  pembeni, binti  huyo   alichukua  pea  mbili  za   viatu  na  kuzificha  kwapani  asijue  kwamba  pembeni  kulikuwa  na  mtu  mwingine  aliyekuwa  akimwangalia....

Alipoaga na  kutaka  kuondoka ndipo timbwili la  kichapo  lilipoanza kwa mrembo huyo ambae aliomba asipelekwe  polisi  na  asipewe  adhabu  kubwa  kwa  kuwa   ana ujauzito  wa miezi mitatu tumboni.

Alisema  kuwa  kutokana na maombi ya mrembo huyo  kupunguziwa adhabu  hakuweza kumfikisha  polisi  zaidi ya kumpa kichapo  cha kufa mtu na kumpokonya  mali  zote alizokuwa ametoka  kuiba katika maduka ya  Miyomboni mjini hapa pamoja na  simu  yake ya kiganjani .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

MNADA BANNER