REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

YANGA MULE MULE

2:31:00 AM Add Comment

wachezaji wa Yanga wakishangilia Goli lao la Kwanza dhid ya APR ya Rwanda, katika Mchezo wa Nusu Fainali katika Uwanja wa Taifa.

 
Klabu Machachari na Bingwa Mtetezi wa Kombe la CECAFA KAGAME CUP, hatimaye wameonesha ubabe na nia ya kutaka kubakiza ubingwa wao kwa mwaka huu, bada ya kukwangua APR ya Rwanda Bao 1-0
Hamis Kiiza ndiye aliyeinua shangwe za Wanajangwani hao katika dakika 15 za awali za Muda wa Nyongeza, yaani dk 30 za Nyongeza
TAMKO LA IDARA YA USALAMA TAIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAMKO LA IDARA YA USALAMA TAIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

2:19:00 AM Add Comment

Katika siku za hivi karibuni, kumejitokeza taarifa zenye tuhuma kadhaa dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa.

Taarifa hizo zimekuwa zikitolewa kwenye vyombo vya habari zikiihusisha Idara hii na matukio ambayo yanaidhalilisha na kuzua maswali mengi kwa wananchi. Kati ya tuhuma hizo ni tukio la kutekwa kwa Dr. STEPHEN ULIMBOKA, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari na madai ya kufanywa kwa mipango ya kuwadhuru baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Upinzani.

Gazeti moja la kila wiki limekuwa likurudia tuhuma hizo mara kwa mara kwa madai kwamba ni habari za uchunguzi na kuihusisha Idara.

Idara inataka kuwahakikishia wananchi kwamba taarifa hizo ni za UZUSHI NA UONGO ambazo zina nia ya kuharibu jina na sifa ya Idara. Taarifa hizo zimekuwa zikiunganishaunganisha vipande vya taarifa mbalimbali ili kukidhi malengo yaliyokusudiwa na wanaolitumia gazeti hilo. Idara haikuhusika wala haihusiki na matukio yoyote yaliyotajwa katika tuhuma hizo. Hivyo tunawaomba wananchi wazipuuze taarifa hizo.

Matukio yaliyotajwa katika tuhuma hizo yanachunguzwa na Jeshi la Polisi ambacho ndicho Chombo Chenye Dhamana, na kwa Maslahi ya Taifa si vizuri kuachia upotoshaji huo uendelee.

Aidha, tunapenda kuwahakikishia Watanzania kuwa uzushi na tuhuma zinazotolewa dhidi ya Idara hazitatuvunja moyo bali zitatuunganisha na hivyo kutuimarisha katika azma yetu ya kuhakikisha nchi yetu inaendelea kubaki salama kwa kushirikiana na wanachi na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama.

Imetolewa na Idara ya Usalama wa Taifa,

Makao Makuu,

DAR ES SALAAM

ALIYEPANGA KUMUUA MANDELA AFIKISHWA MAHAKAMANI.

2:06:00 AM Add Comment










Mahakama nchini Afrika ya Kusini imemtia hatiani kiongozi wa kundi lenye itikadi kali za ubaguzi wa rangi la Boer Army ya kutaka kuipindua serikali iliyokuwa inaongozwa na Rais wa zamani Nelson Mandela mwaka 2002.
Nelson Mandela


Kiongozi huyo aliyekuwa mhadhiri wa chuo kikuu nchini humo Mike du Toit, alipanga kumuua Mandela kwa mashambulizi ya mabomu kisha aungóe madarakani utawala wa watu weusi. Kesi hiyo imedumu kwa miaka tisa. Hukumu yake inatarajiwa kutolewa mwezi ujao na huenda akakabiliwa na kifungo cha maisha jela.

Wafuasi wengine 21 wa kundi hilo hukumu zao zitatolewa wiki chache zijazo. Jaji Eben Jordan aliyeendesha kesi hiyo amesema kuwa mashahidi wameeleza namna kundi hilo lilivyopanga kufanya mauwaji hayo. Lilipanga pia kuwaua kwa risasi raia weupe wa nchi hiyo wanaounga mkono utawala wa watu weusi.

MNADA BANNER