REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

PIMENI KAULI ZENU NA VITENDO VYENU- JK AWAAMBIA VIONGOZI WA DINI NA SIASA

11:07:00 PM Add Comment

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewataka viongozi wa dini na wanasiasa kupima kauli na vitendo vyao ili kuepusha kuligawa taifa kwa misingi ya imani za dini na itikadi za siasa, kama ilivyotaka kujitokeza mwaka 2012.

Katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa Taifa juzi, Rais Kikwete alisema kwa mara ya kwanza mwaka  2012, Tanzania ilifikishwa kwenye hatari ya kutokea mgawanyiko wa Watanzania au hata mapigano kwa misingi ya dini zao.

“Nimeshalisemea jambo hili siku za nyuma na napenda kurudia leo kuwasihi Watanzania wenzangu kupima athari za kauli zetu na matendo yetu kwa mustakabali wa jamii yetu, nchi yetu na watu wake,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Viongozi wa dini, waumini na viongozi wa siasa na wafuasi wao wanao wajibu maalumu wa kuhakikisha kuwa Watanzania wanaendelea kuishi kwa upendo, amani na ushirikiano bila kujali tofauti ya dini zao, makabila yao, rangi zao au maeneo watokako.”

Ingawa Rais Kikwete hakutaja mambo yaliyotaka kuligawa taifa mwaka jana, mwaka huo ulikumbwa na matukio kadhaa yaliyohusishwa na imani za kidini ikiwamo uchomaji wa makanisa katika Miji ya Zanzibar na Dar es Salaam.

Matukio mengine ambayo baadhi ya watu waliyahusisha na imani za dini ni vurugu zilizofanywa na wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Kikundi cha Waislamu wa Taasisi za Jumuiya ya Kiislamu Tanzania ambazo ni pamoja na kuvamia Ofisi za Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Dar es Salaam na uvamizi wa maeneo ya wazi eneo la Temeke. Hata hivyo, watu kadhaa walikamatwa na kufunguliwa mashtaka katika mahakama mbalimbali nchini kwa tuhuma za ama kushiriki au kuongoza vurugu hizo.

EWURA YASHUSHA BEI YA PETROL NA DIESEL

11:03:00 PM Add Comment

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imetangaza bei kikomo cha bidhaa za mafuta kinayoonyesha kuwa petroli, dizeli na mafuta ya taa zimeshuka kuanzia leo.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu imesema bei hizo zimepungua ikilinganishwa na toleo lililopita la Desemba 5, mwaka jana.

“Katika toleo hili, bei za rejareja kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa, zimepungua kwa viwango vifuatavyo: petroli Sh126 kwa lita sawa na asilimia 5.96; dizeli Sh32 kwa lita sawa na asilimia 1.60 na mafuta ya taa Sh50.74 kwa lita sawa na asilimia 2.50,” imeeleza taarifa hiyo.

Kwa punguzo hilo, bei ya rejareja ya petroli katika jiji la Dar es Salaam itauzwa kwa Sh1,993, dizeli Sh1,967 na mafuta ya taa Sh1,973. Arusha petroli ni Sh2,077, dizeli Sh2,051 na mafuta ya taa Sh2,057.

Katika jiji la Mbeya petroli itauzwa kwa Sh2,099, dizeli Sh2,074 na mafuta ya taa Sh2,079 na jijini Mwanza, petroli itauzwa kwa Sh2,142, dizeli Sh2,117 na mafuta ya taa Sh2,122.
Taarifa imefafanua kuwa mbali na kupungua bei hiyo katika uuzaji wa rejareja, bei pia imepungua kwa katika uuzaji wa jumla ikilinganishwa na matoleo mawili yaliyopita.

“Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimepungua kama ifuatavyo: petroli kwa Sh126.10 kwa lita sawa na asilimia 6.17; dizeli kwa Sh32.48 kwa lita sawa na asilimia 1.69 na mafuta ya taa kwa Sh50.74 kwa lita sawa na asilimia 2.6,” alisema.

Mkurugenzi huyo amesema katika taarifa hiyo kuwa mabadiliko hayo ya bei, yametokana na kupungua kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kuimarika kidogo kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania dhidi ya Dola ya Marekani.

Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2008, bei za bidhaa za mafuta ya petroli, zitaendelea kupangwa na soko.

“Ewura itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya uamuzi stahiki kuhusu ununuzi wa bidhaa za mafuta,” alisema Masebu.

Hata hivyo, Masebu alisema pamoja na mpango huo wa Ewura kuweka bei ya kikomo, kampuni za mafuta ziko huru kuuza bidhaa hizo kwa bei ya ushindani, ilimradi ziwe chini ya bei hiyo kikomo.

Alivitaka vituo vya mafuta kuchapisha bei hizo mpya katika mabango yanayoonekana bayana na kuonyesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika.

“Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta kutoka kwenye vituo vinavyouza mafuta kwa bei ndogo zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika,” alisema.

Masebu aliwashauri wanunuzi kuchukua stakabadhi ya malipo inayoonyesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita ili itumike baadaye kama kidhibiti endapo kutajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko ya kikomo au yenye kiwango cha ubora kisichofaa.

CHANZO : MWANANCHI

CONFIRMED :SAJUKI AMETUTOKA

10:37:00 PM Add Comment
 Marehemu Sajuki alipokuwa akipata Matibabu Nchini India

 Marehemu Sajuki (kushoto) alipokuja kutembelewa na Wasanii wenzake. Katikati ni Mkewe Wastara Juma

 Marehemu Sajuki akiwa amembeba Mtoto Wao

Marehemu Sajuki akiwa na Mke wake Wastara Juma

Aliyekuwa Msanii maarufu katika Tasnia ya Filamu nchini Juma Kilowoko almaarufu kama  ’SAJUKI’ ambaye amekuwqa akisumbuliwa na maradhi ya muda mrefu, amefariki Dunia  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Taarifa hizo za Msiba wa Marehemu Sajuki, zimetufikia Rasmi asubuhi hii Majira ya Saa Moja.
Sajuki amekuwa akisumbuliwa na Uvimbe Tumboni kwake, kwa Muda wa miaka Miwili Sasa. Hali hiyo ilimfanya kupelekwa katika Nchi ya India kwa ajili ya Matibabu zaidi, hali ambayo ilimpatia ahueni na Kurudi Nchini Tanzania, kabla Mauti hayajamkuta.
Aidha taarifa za Kuzidiwa kwa Sajuki, zilitolewa mnamo December 2012, baada ya hali yake kuwa Mbaya kwa mara nyingine tena, na hakupata ahueni mpaka Umaiti unamkuta

Joachimjunior inaungana na Familia ya Marehemu Sajuki, katika Msiba huu Mzito, ulioikumbva Tasnia ya Filamu Nchini Tanzania.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu SAJUKI, maqhali Pema peponi , Amina.

TUTAENDELEA KUKULETEA TAARIFA ZAIDI ZA MSIBA WA MPENDWA WETU SAJUKI. ENDELEA KUWA NASI

MNADA BANNER