REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

HONGERA SHAKIRA KWA KUJIFUNGUA...HAYA NDIYO ALIYOYASEMA (Samahani laini...kwa Wale tusiojua kuvunja Yai)

11:11:00 PM Add Comment
Shakira na MMe wake Pique kabla ya kujifungua
We are happy to announce the birth of Milan Piqué Mebarak, son of Shakira Mebarak and Gerard Piqué, born January 22nd at 9:36pm, in Barcelona, Spain.

The name Milan (pronounced MEE-lahn), means dear, loving and gracious in Slavic; in Ancient Roman, eager and laborious; and in Sanskrit, unification.

Just like his father, baby Milan became a member of FC Barcelona at birth.

The hospital confirmed that the couple’s first child weighed approximately 6lbs. 6 ounces, and that both mother and child are in excellent health.

BODA BODA WAZUA TAFRANI MWANZA

11:05:00 PM Add Comment
POLISI mkoani Mwanza wamelazimika kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwatawanya waendesha bodaboda waliokuwa wakiwalazimisha askari wawaachie wenzao waliowakamata kwa makosa mbalimbali.
Wakati hayo yakitokea Mwanza, huko Arusha, madereva teksi walipandwa na jazba baada ya kuzuka kwa mzozo kati yao na uongozi wa Hoteli ya Palace kutokana na kile walichoeleza kuwa ni kuondolewa kinyemela katika eneo lao.
Huko Mwanza, ghasia hizo ziliibuka wakati polisi wa usalama barabarani na kikosi maalumu cha ukaguzi wa magari walipofanya doria kukagua leseni na uhalali wa madereva hao wanaofanya shughuli za kusafirisha abiria.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, vurugu hizo zilianza saa 2:46 asubuhi baada ya polisi kuwakamata waendesha bodaboda wapatao 26, ambao walitozwa faini za papo kwa papo kulingana na makosa yao, huku wengine wakiendelea kushikiliwa.
Hatua hiyo iliwafanya waanze kujikusanya kutoka sehemu mbalimbali na kuandamana hadi eneo kulikokuwa limetengwa kwa ukaguzi huo katika Mtaa wa Mission.

Baada ya kufika eneo hilo, walianza kuwarushia mawe askari hao, huku baadhi yao wakiendesha pikipiki kuzunguka eneo hilo na kuzuia magari kupita hali iliyozua tafrani. Baada ya kutokea hivyo, askari hao walilazimika kuwaita askari wengine ili kuwakabili vijana hao.

Vurugu hizo zilizodumu kwa saa tatu, zilisababisha kufungwa kwa barabara iendayo Uwanja wa Ndege na katika eneo la Pasiansi, huku baadhi ya abiria wakilazimika kuteremka katika daladala na kukimbia ovyo na wengine kulala katika mifereji ya maji machafu baada ya milio ya risasi na mabomu ya machozi kuanza kurindima.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alisema jana kwamba polisi hao walikuwa katika ukaguzi wa leseni na vifaa vingine vya usalama kama kofia ngumu ndipo baadhi ya madereva hao wa bodaboda wakaanza kupinga kukamatwa kwa wenzao na kutozwa faini kutokana na makosa waliyokuwa nayo.

Mmoja wa waendesha bodaboda ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini alisema kwamba polisi wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwachukulia leseni zao, huku wakiwabambikiza makosa mbalimbali kwa lengo la kujipatia fedha kinyume cha sheria.
Kamanda Mangu aliwataka waendesha bodaboda hao kutoa taarifa wanaponyanyaswa au kuombwa rushwa na askari hao.
CHANZO : MWANANCHI

MNADA BANNER