REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

HUYU NDIYE RAFIKI WA KWELI : THE ROCK HUPENDA KUGAWA MAGARI BURE

2:23:00 AM Add Comment

Na Hezron Munisi  
KAMA itaokea akawepo mtu wa aina hii hapa nchini Tanzania, ambaye ana moyo wa aina hii, na anajitoa kwa njia hii bila kinyongo, basi wabongo tutajiweka naye karibu hasa ukizingatia shobo na udananda ndo mahali petu katika kipindi hiki kigumu kimaisha

DAWYNE JOHNSON a.k.a THE ROCK ambaye ni actor bin Muigizaji wa filamu nchini Marekani, ameweka wazi kuwa tatizo lake kubwa, na ugonjwa wake mkubwa katika maisha yake, ni kugawa magari kwa watu.

Akifafanua kauli yake, The Rock ambaye zamani alikuwa ni mwanamieleka ambaye alijikita katika filamu na kuvutia zaidi katika Filamu kama vile Fast & Furious, Jumanji, na nyinginezo, anadai kuwa chanzo cha hayo yote ni baba Yake, Mzee Rocky Johnson ambaye aliwahi kumtamkia kuwa anahitaji gari la thamani kutoka kwa mwanaye

The Rock alisema kuwa, kuna kipindi baba yake mzazi ambaye pia zamani alikuwa ni mwanamieleka, alipata tatizo katika upande wa Hips moja hivyo ikamlazimu amdanga mtoto wake kuwa daktari ameshauri atumie gari la gharama (jina limehifadhiwa kibiashara) kitu ambacho kilimchekesha sana The Rock lakini akabaini kuwa baba anatamani tu apate gari la hivyo wala sio ushauri wa daktari

Hata hivyo, The Rock hagawi magari kwa watu baki, bali huwa anagawa kwa marafiki, Familia yake, na watu wengine wa karibu zaidi

EXCLUSIVE: DJ KHALED ANAHITAJI KUPUMZIKA

1:37:00 AM Add Comment

Na Rich Sam   
#WATUWAMUNGU wengi tunafahamu kabisa kuwa ili mkono uweze kwenda kinywani, lazima uhakikishe kabisa unapiga kazi kufa na kupona, ikibidi pasipo kulala kabisa ili mambo yako yasogee, na hii imekuwa ikijoptekeza mara kwa mara kwa wasanii mbali mbali kupiga show na kupromote kazi zao pasipo kupumzika.

DJ KHALED ambaye hivi sasa anafanya vizuri na Album yake Mpya "FATHER OF ASAHD" amekuwa katika tours mbali mbali na gigs kadha wa kadha ili kuwashibisha mashabiki wake hasa kupitia Burudani yake ambayo inafurahiwa na watu wengi sana ulimwenguni.

Na tangu ameachia Album yake hiyo, amekuwa akifanya kazi ya kui-promote maeneo mbali mbali pasipo kupumzika vizuri, kitu ambacho kimemfanya achukue uamuzi mwingine sasa hivi

Kupitia instagram account yake, Khaled ameweka wazi kuwa hivi sasa anahitaji kupumzika kwa takriban siku mbili , ili aweze kuilinda afya yake ukizingatia amekuwa akifanya kazi sana bila kupumzika.

Dj Khaled pia ameongeza kuwa, hata Malkia wake (Mama Asahd) ambaye ni mchumba wake, amekuwa akimzuia kupokea simu kwa hivi sasa kwa sababu anahitaji kupumzika ili pia ajijenge kiafya na hata kuwa karibu na familia yake

Tunamnukuu
"Ninahitaji kupumzika. Nimakuwa nikjishughulisha kwa nguvu sana na ninadhani nahitaji siku moja au mbili kupumzika hii , na sababu ambayo inanifanya nipost hili jambo  ni kwamba simu yangu haitoacha kuita kwa sababu malkia wangu ataishia kunizuia nisiongee n mtu kwa sababu nahitaji siku mbili za kupumzika. Sasa, kama mtaona hili jambo, basi niacheni nipumzike, hakuna chochote zaidi ya upendo. Ninahitaji siku mbili kisha nitarejea"


MAAJABU YA WANAWAKE WANNE WALIOZAA NA MWANAUME MMOJA

2:47:00 AM Add Comment

Na Hezron Munisi 
BWANA kama ingekuwa ni hapa Tanzania, lazima tungejiuliza maswali mengi kuwa inawezekanaje tukio hili lifanyike tena kukiwa na amani kabisa ili hali tunafahamu namna ambavyo hali huwa inakuwa pale mkeo ama mzazi mwenzio anapokuja kubaini kuwa imetokea una mtoto mwingine nje

lakini hii imekuwa ni tofauti kabisa kwa wanawake hawa Wanne ambao wamechukua akili za wengi kunako mitandao ya kijamii baada ya kupiga picha ya pamoja na watoto wao ambao wote walizaa na mwanaume mmoja

Wanawake hao hawana mtotro mmoja mmoja kama ilivyo kwa wengine, ila wanawatoto kadhaa na mwanaume mmoja huku wakionekana kufurahia hali hiyo yaani wanapendana haswa kwa tafsiri ya picha hiyo

Kinachowashangaza wengi, ni namna ambavyo wanawake hao wapo karibu sana, wanaonesha kupendana na kuwajali watoto wa mume wao

Cha ajabu zaidi, ni kwamba, wanawake watatu kati ya wale wanne, walipata ujauzito kwa wakati mmoja na kujifungua kwa kupishana kidogo sana

Mume wao pia, anayeitwa CORO INGRAM SR naye hayuko nyuma katika kuhakikisha anajivunia hali hiyo, huku wanaume wengi wakihoji kuwa jamaa kaweza vipi.

MAMBO YA ALBUM : VICTORIA KIMANI KUTOKA NCHINI KENYA NAYE KAACHIA ALBUM

2:35:00 AM Add Comment

Na Joe Mwangi-KENYA 
Watu Wa Mungu Finaly biashara ya Album (EP), inaanza kuchukua nafasi kubwa katika Maisha ya Wasanii hapa Afrika Mashariki.

Ukiachilia mbali Tanzania kuanza kupiga hatua kupitia Album zao baada ya Wasanii VANESSA MDEE, DIAMOND PLATNUMZ, CHIN BEEZ na wengine kujikita katika ulimwengu na soko la albums, Nchini Kenya Victoria Kimani naye katutangazia Album Yake

Kupitia instagram account yake, Kimani ambaye ni Hitmaker wa PROKOTO aliweka wazi kuwa album yake hiyo inaitwa AFROPOLITAN na ina nyimbo Saba

Nyimbo hizo ni pamoja na
  1. WONKA (Produced By Gospel On The Beatz)
  2. SHOULD BE (Produced By Ace Harris & Dj Tag)
  3. HIGHEST CALIBRE (Produced By Ace Harris & Dj Tag)
  4. MY SWEETIE (Produced By Ace Harris & Dj Tag)
  5. BOOM (Produced By Selasi)
  6. FOOL (Produced By Ace Harris & Dj Tag)
  7. NOT FOR SALE (Produced by Gospel On The Beat) 

JAY Z: "NILILIA KWA FURAHA BAADA YA MAMA YANGU KUMKA KUWA ANA HISIA ZA DHATI ZA KIMAPENZI JUU YA MWANAMKE MWENZAKE"

2:21:00 AM Add Comment

Na Baba Juti 
WATU WA MUNGU, hivi unajiskiaje pale ambapo Mama yako Mzazi (Single Mother) anapotamka mbele yako na wadogo zako na wakubwa zako kuwa Anahisi anahisia kali sana za kimapenzi juu ya mtu mwingine tofauti na Baba Yenu?

Hicho ndicho kitu ambacho Rapper Jay Z amekiweka wazi hasa namna ambavyo alijihisi mara baada ya mama yake mzazi , Gloria Carter kuweka wazi kuwa anampenda sana mpenzi wake ambaye ni wa jinsia moja

Kama utakuwa unakumbuka katika album ya Jay Z ya 4:44 kulikuwa na wimbo ambao Jay Z aliandika kuhusu mama yake kushiriki mapenzi ya jinsia moja na mwanaume huku akiacha maswali mengi sana kuhusu namna ambavyo alipokea, lakini kwa upande wake anakiri kuwa, siku ambapo anasikia mama yake mazazi anamtamkia kuwa, ana hisia kali na za dhati juu ya partner wake wa kike, miezi kama nane iliyokata, alijisikia furaha mpaka akalia kabisa kwa Furaha

Kilichomfanya Jay afurahi mpaka kulia ama aguswe na tamko la mama yake mpaka kutoa machozi, ni namna ambavyo mama yao mzazi amekuwa akiishi maisha ambayo hastahili kuishi, ili awalinde watoto wake na wala asiwaaaibishe watoto wake, lakini baada ya muda anaamua kuwa huru na kumwambia Jay Z kuwa ana hisia za kimapenzi na mwanamke mwingine

Katika kukazia Zaidi, Jay anasema bada ya mama yake kupata ujasiri huo na kumwambia kuhsu hisia zake, ilimlazimu kesho yake aandike wimbo kuhusu mama yake kushiriki mapenzi ya Jinsia moja

BIRDMAN HAKUTAMANI UGOMVI WAKE NA LIL WAYNE UINGIA KATIKA MAISHA YA WATOTO WAO

1:36:00 AM Add Comment

Na Rich Sam
KUMEKUWA na Taarifa zikizagaa maeneo kadha wa kadha kuwa hatimaye Familia iliyovurugika bila amani, hatimaye imerejea, na hapa tunamzungumzia Lil Wayne pamoja na Birdman ambao kwa pamoja waliingia katika timbwili zito la kudhurumiana mamilioni ya fedha

Sasa, baada ya kuwepo kwa taarifa za muunganiko wao kwa mara nyingine, hatimaye Rapper na Big Boss wa Cash Money Records Label Brian "Birdman" Wiliams ameweka wazi kinachoendelea baina yao huku akifafanua ni nini kiliwasukuma mpaka kufikia uamuzi wa wao kurudisha mahusiano yao.

Birdman anafafanua kuwa, UPENDO na MAISHA ndivyo ambavyo vilifanya muda mwingi sasa atamani kurudisha mahusiano yake na mwanae wa kumlea, Lil Wayne maana hakuwahi kufikiria kama wangeefikia hatua hiyo ambayo imeathiri vitu vingi hasa ukaribu wao na shughuli zao

Tofauti na hilo, Birdman meongeza kuwa hakuwahi kutamani masuala ya Ugomvi wake na mtu yeyote yaathiri ama yaingie katika Familia yake, na ndio maana alijitahidi sasa hali hiyo isije ikaikumba aidha familia ya Weezy au Familiake ukizingatia wana watoto na hakuna kizuri cha kujifunza katika Ugomvi wao

Pia akajazia kuwa, Yeye binafsi alikuwa akiongea vizuri na mtoto wa Lil Wayne (Reginae) na Wayne alikuwa akiongea vema sana na wanapendana sana na Watoto wake (birdman) na ndio maana ikawa ni kazi rahisi kurejesha mahusiano yao

TODAY: 04TH APRIL- WORLD RAT DAY

1:08:00 AM Add Comment

DAYS OF THE YEAR  
Get two things straight right away – rats aren’t dirty, and James Cagney never said it anyway! These are just two of the myths and misconceptions that World Rat Day hopes to dispel as it celebrates the joys of fancy rats.

Anyone who keeps rats as pets or companions is already in on the secret: these animals are friendly, loyal, intelligent, and very endearing. Unfortunately they’ve had a bit of bad press over the years, what with the Black Death, Bubonic Plague and a thousand Pacific islands which have had their native wildlife chewed down to ground level and beyond. But what’s a few environmental and social catastrophes between friends?

Once you get to know rats on a one-to-one basis, then all of their finer qualities will come to the fore. Why not drop in to your local World Rat Day event and discover just how adorably lovable they really are?

MNADA BANNER