REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

KAMA ULIKUWA UNASUBIRI MECHI YA SIMBA NA YANGA, KUNA MABADILIKO HAYA

6:42:00 AM Add Comment


Na Dina Ismail, DAR ES SALAAM
MECHI ya watani wa jadi, Simba SC na Yanga SC mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyokuwa ichezwe Oktoba 12, mwaka huu imefutwa na sasa tarehe mpya itatajwa kesho.


Taarifa ya TFF leo imesema kwamba, hiyo iantokana na mchezo wa kirafiki wa kimataifa baina ya Taifa Stars na Benin ambao kwa ujumla utabadilisha ratiba ya Ligi Kuu na marekebisho hayo yatatangazwa kesho (Septemba 26 mwaka huu).

Taifa Stars inashuka uwanjani Oktoba 12 mwaka huu kuikabili Benin katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).


Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Programu ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kwa ajili ya mechi hiyo itatangazwa baadaye na Kocha Mkuu Mart Nooij.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linaendelea na taratibu nyingine kwa ajili ya mechi hiyo ikiwemo usafiri wa Benin kuja nchini, ambapo timu hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Oktoba 10 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 28.
Pambano la Stars na Benin litatanguliwa na mechi ya kudumisha 

upendo kati ya viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu.
Wakati huo huo: Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi anatarajia kufunga mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa vyama vya mpira wa miguu wa wanawake vya mikoa ya Tanzania Bara.

Hafla ya kufunga mafunzo hayo itafanyika kesho (Septemba 26 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya siku tano yalishirikisha viongozi 34 wakiwemo baadhi ya waandishi wa habari na Meneja wa Twiga Stars, na yaliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau.

RAIS KIKWETE ANAHITAJIKA KUTOA USHAHIDI MAHAKAMANI

6:20:00 AM Add Comment

KUTOKA Arusha, TANZANIA 
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa mashahidi wanaotarajiwa kuitwa na walalamikaji katika shauri dhidi ya nchi za Kenya, Uganda na Rwanda linaloendelea katika Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ).

Wakili Jimmy Obeid anayewawakilisha walalamikaji katika shauri namba 9/2013, jana aliieleza Mahakama kuwa miongoni mwa mashahidi watakaoitwa kujenga kesi hiyo ni pamoja na Rais Kikwete.

Shauri hilo lilifungulliwa na Watanzania watatu, Ally Hatib Msangi, David Makatha na John Bwenda wakidai kitendo cha Kenya, Uganda na Rwanda kufanya vikao bila kuzishirikisha Tanzania na Burundi ni ukiukwaji wa mkataba wa kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

Miongoni mwa vifungu vya mkataba wa EAC vinavyodaiwa kukiukwa ni namba 3(3) (c) kinachotaka ushiriki sahihi kuimarisha ushirikiano ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kifungu cha 6 (a) (b) (d) na (f) kinachozitaka nchi wanachama kuzingatia misingi ya kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.

Katika ushahidi wake, Rais Kikwete ataombwa kuthibitisha hotuba yake kwa Taifa aliyoitoa bungeni Novemba 7, mwaka jana ambayo ilielezea jinsi Tanzania na Burundi zilivyotengwa na baadhi ya nchi wanachama wa EAC.

“Kutokana na uzito na majukumu ya Rais Kikwete tunayepanga kumwita kama mmoja wa mashahidi wetu, naiomba Mahakama muda wa mwezi mmoja kuwasilisha orodha ya mashahidi na hati za viapo,” alisema Obeid. Jopo la majaji watano wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Jean-Bosco Butasi, Naibu Jaji Kiongozi, Isaac Lenaola na wengine Faustin Ntezilyayo, Monica Mugenyi na Fakhi Jundu walikubali ombi hilo na kupanga Oktoba 24, mwaka huu wadai kuwasilisha hati ya kiapo na orodha ya mashahidi.

Wadaiwa katika shauri hilo ni Katibu Mkuu wa EAC, anayewakilishwa na wakili Dk Antony Kafumbe wakati mdaiwa wa pili ni Mwanasheria Mkuu wa Kenya anayewakilishwa na mawakili wawili, Muthoni Kimani na Peter Ngumi, mdaiwa wa tatu ni Mwanasheria Mkuu wa Uganda anayewakilishwa na mawakili watatu, Elisha Bafirawala, Richard Adrole na Maureen Ijang’ na mdaiwa wa nne ni Mwanasheria Mkuu wa Rwanda anayewakilishwa na wakili Malaala Aimable.

Wadaiwa hao watawasilisha majibu kabla ya Novemba 7 mwaka huu na kutoa maelezo ya ziada Novemba 14 mwaka huu kabla ya Mahakama kupanga siku ya shauri hilo kusikilizwa na pande zote zitapewa wito maalumu.

Septemba 2, mwaka huu, wadai waliondoa mahakamani ombi la zuio la muda dhidi ya vikao vya muungano wa wenye nia (coalition of the willing), baada ya Tanzania na Burundi kuanza kushirikishwa kwenye vikao viwili vilivyofanyika Februari 24 na Mei 2, mwaka huu.

LAMBORGHINI YA DHAHABU IMEONEKANA NCHINI UFARANSA..CHEKI PICHA ZAKE HAPA. INAUZWA DOLLA MILIONI 6

5:00:00 AM Add Comment





DAH: MKE WA WIZ KHALIFA, AMBER ROSE, AFUNGUA MADAI YA TALAKA…..INASEMEKANA NICK CANNON NDIYE CHANZO

2:03:00 AM Add Comment

LOS ANGELS, Marekani
BIG News nay a kushtua ni hii ambayo TTM tumekutana nayo ikizunguka kunako Mitandao Mbali mbali ya Kijamii, kuhusu Kuvunjika kwa Ndoa ya Amber Rose na Wiz Khalifa, iliyodumu kwa Muda wa Mwaka 1 na Miezi kadhaa..FULL STORY iko Hivi…

Mpaka Hivi sasa, tayari Amber Rose ameshafungua jalada la Kudai talaka kutoka kwa Mumewe Huyo CAMERON THOMAZ, maarufu kama Wiz Khalifa.

Ingawa Mpka hivi sasa Wiz Khalifa hajatoa Taarifa Maalum kuhusu chanzo cha wawili hao Kutemana, Lakini huwezi amini, tatizo kubwa linaloonekana kuwepo, Ni Usaliti baina ya wanandoa hao wawili, ambapo kila mmoja anamlaumu mwenzake kwa Kujihusisha na UCHEPUKAJI mkubwa.

Licha ya Miezi kuadhaa Amber Rose kupost Picha ya Ndoa yao, wakipongezana kwa Kutimiza Mwaka Mmoja katika Ndoa yao, lakini hivi sasa Ni KWISHA HABARI, hakuna cha Amber Rose , wala Wiz Khalifa Kuhusiana na Ndoa.

·        Ugomvi Ni Mkubwa:
Kama Ilivyokuwa kwa Nick Cannon na Mariah Carey, basi safari hii imekuwa hivyo Hivyo kwa upande wa Wiz Khalifa ambaye anafanya Vema na Albam Yake ya BLACCHOLLYWOOD iliyosheheni mangoma Makali likiwemo la WE DEM BOYS. Chanzo kilicho karibu na wawili hao, kinadai kuwa, Ugomvi ulioko baina ya wanandoa hawa wawili, ni Mkubwa na Mchungu , maana hata ukiangalia Documents za kudai talaka, ni Chungu balaa

·        Nick Cannon Kuhusika Katika Kuvunjika Kwa Ndoa Hiyo.
Hivi majuzi tu, Aliyekuwa Mume wa Mariah Carey, Nick Cannon ambaye nayeye Ndoa yake iliingia katika Noma Kubwa na Madai ya talaka Kufunguliwa, alisikika akisema kuwa, anataka kumfanya Amber Rose awe Maarufu kupitia Televisheni na Huenda akashirikiana naye hasa Kibiashara.
Kauli hiyo iliwafanya wengi wajiulize maswali, hasa ukizingatia inasemekana kuwa Eti, Amber Rose na Nick Cannon wameshawahi kushiriki katika Mkunjuko wa Kimapenzi.
Hali Hiyo ilizua Utata sana, huku wanahabari wakidhani kuwa huenda Nick cannon anazingua, lakini walipomhoji Amber, alikiri kuwa ni Kweli, atafanya kazi na Nick Cannon,

·        Nick Cannon Amejibu Hivi:
Kwa upande wake Nic Cannon ambaye kwa asilimia kubwa ni HOST katika Vipindi mbali mbali hasa AMERICA HAS GOT TALENT, amesema kuwa yeye hajahusika kwa namna yoyote ile, katika kuvunjika kwa Ndoa ya Wiz khalifa na Amber Rose
Pia Cannon ameongeza ya kwamba, Yeye na Amber Rose, walikubaliana wafanye Mishe za kibiashara tu, na hakuna ushauri wa kudai talaka uliotoka kwake hata Siku moja.

Fahamu Haya Machache:
  • ·        Kipindi cha Awali, Amber Rose amewahi kuwa STRIPPER, yaani Mcheza Utupu/Uchi wa Night Clubs
  • ·        Amewahi kukunjuka na Rapper Kanye West ingawa hawakudumu sana katika Mahusiano yao, huku ikiaminika kuwa Kanye alikuwa akigawa kifinyo kwa Amber Rose
  • ·        Amber Rose aliwahi kumzawadia WIZ KHALIFA saa yenye Thamani kubwa, aliyowahi kupewa na Kanye West wakati wapo Katika mahusiano.
  • ·        Amber Rose anataka apewe haki za malezi na Usimamizi wa Mtoto wao, SEBASTIAN THOMAZ “The Bash”, na anataka Wiz Khalifa awe anamtembelea Tu. Mtoto wao ana Umri wa Mwaka mmoja

“ADAM JUMA ANALIPWA VILE VILE,YAANI ANLIPWA KAWAIDA..ILA TUANGALIE AMETUTOA WAPI”-KAULI YA RIC MAVOKO

1:58:00 AM Add Comment

DAR ES SALAAM, Tanzania
NI KWELI Kipindi cha Nyuma Video kali kama Vile, SHE GOTTA GWAN ya Ngwea, ICE CREAM ya Noorah, CHUNGWA ya Suma-Lee na Nyinginezo kibao, tulikuwa  tunazielewa na kuzipenda sana kupitia mkono wa ADAM JUMA wa VISUAL LAB

SASA, Muimbaji na Mkali wa FOLLOW ME ambaye Soon anaaachia mzigo Mpya wa PACHA WANGU, Rich Mavoko, amewasihi wasanii wa Tanzania kukumbuka Mchango wa Adam Juma hasa pale walipo hivi sasa, na Kiasi wanachomlipa.

Akizungumza kuhusiana na Hilo, MAVOCO amesema kuwa, wasanii hawatakiwi kulalamika juu Adam Juma kuhitaji Mkwanja Mrefu kufanya Video, pasipo kukumbuka Mchango wake katika Video Industry hapa Nchini Tanzania
Hapa Tunamnukuu akisema:

 “Lakini tuangalie pia ametutoa wapi. Movement zake kuhusu music video Adam Juma ameitoa wapi. Tuapreciate kitu ambacho amekifanya. Mimi naweza nika-appreciate media, maDj, na wasanii wenzangu basi tuapreciate pia (Adam J) ametutoa mbali ujue.”

Tofauti na hilo, Rich Mavoco ameongeza kuwa mpaka hivi sasa, kwa asilimia kubwa Adam Juma analipwa Kawaida, na Analipwa Vile Vile.
Aidha kuhusu Video yake hiyo Mpya, mavoko amedai kuwa, adam Juma na Timu yake Nzima, walisafiri Mpaka Cape Town, na wametumia Vifaa vya Kisasa, huku kazi Nzima ikifanyikia huko huko Afrika ya Kusini.


Adam Juma amewahi Kutengeneza Hit Songs za wasanii wa Muziki wa Kizazi kipya ambao Hivi sasa wamekimbilia Production za Kimataifa kama Vile OMMY DIMPOZ (Nai Nai & Baadaye) pamoja na DAIMONDS ( Kamwambie , Mawazo,Mbagala , nitarejea & Moyo wangu)

SHAVU KWA SHAVU: DIAMONDZ PLATNUMZ APATA UBALOZI, YOUNG DEE APATA UBALOZI..

1:47:00 AM Add Comment

DAR ES SALAAM, Tanzania
WAKATI Diamonds akitoa tamko Rasmi kuhusu Kuwa balozi wa Application ya MZIIK hasa kunako SMART PHONES, Muda huo Huo pia tukapata Info kuwa YOUNG DEE naye karamba Ubalozi wa Channel moja hivi ya kampuni ya STAR TIMES..sasa Hii ni Kupitia Account zao za Instagram

·        Kwa Upande Wa Diamondz “Dangote”
“Chibu Dangote” ama Nasib Abdul alikutana na Shavu la kutosha kwa Kuwa Balozi wa Application Mpya ya Simu za aina ya Smart Phones, inayoitwa MZIIKI.
Hapa tunanukuu Kauli yake
“Ningependa kukutaarifu Shabiki yangu Mpendwa kuwa, Kijana Wako sasa Ni balozi wa Application Mpya iitwayo #MZIIKI
Akamaliza Chib dangote huku kwa Chini akiitafsiri kwa Lugha ya Kiingereza kwa wale wasiofahamu Kiswahili

·        Kwa Upande Wa Young Dee
Naye rapper Young Dee ambaye hivi sasa anafanya Poa na Mkwaju mpya wa SIO MCHOYO, naye alitoa Mtonyo kuwa ni Baalozi wa Channel ya Q-YOU ya Star Times….hapa tunamnukuu

“Thanks #StarTimes for Such a Deal…..New Ambassador of #Qyou Chanel….. Its Official Now
Kwa Upande wetu TTM, tunawatakia kazi Njema, hasa katika kutangaza Bidhaa walizokabidhiwa. Ameeen


10 Healthy and Delicious Avocado Recipes

8:10:00 AM Add Comment

PURHIYA Mahmoud
Last year it was made the first homemade bread from one of the favourite banana recipes. It was so delicious! And now, Now, its better  we show you how to make the first avocado recipe with walnut bread. we like avocados and some of people like walnuts, so we believe it’ll be perfect dish for us.
Ingredients:
  • 1 cup organic white, unbleached spelt flour
  • 3/4 cup organic whole spelt flour
  • 1 tsp baking powder
  • 1/2 tsp bicarbonate of soda
  • pinch of salt
  • 4 large free-range eggs
  • 1/2 cup organic fat-free yoghurt
  • 1 avocado, mashed
  • 3 tbsp walnut oil
  • 1 cup walnuts, chopped

Directions:
Preheat oven to 1800 C and prepare a standard size loaf tin.
In a medium bowl, sift together the flours, baking powder, bicarbonate of soda and salt. Beat the eggs in another bowl and beat in the yoghurt avocado and oil. Fold the dry ingredients into the egg mixture, add the walnuts and fold to combine. Bake for 45 minutes or until a skewer inserted in the middle comes out clean.


Wonton cups with avocado and smoked salmon would be a perfect appetizer during the party or holiday dinner. Bake this little wonton cups inside mini muffin trays. When won ton cups come out of the oven, they’ll have perfect little form to hold the ingredients of this delicious avocado recipe.
Ingredients:
  • 24 square won ton or shumai (dumpling) wrappers
  • 2 tablespoons unsalted butter, melted
  • 2 teaspoons white sesame seeds
  • 4 ounces hot-smoked salmon (see Notes), flaked into small pieces
  • 1/2 cup finely sliced green onions, including tops
  • 1/4 cup finely chopped fresh cilantro
  • 1 tablespoon lime juice
  • 2 teaspoons grated fresh ginger
  • 1/2 teaspoon kosher salt
  • 1 small avocado, finely diced
Directions:
Preheat oven to 350° C. Lay 12 won ton wrappers flat and, using about half the butter, brush both sides. Press into mini muffin cups (2 tbsp. size), pleating each to form a small cup. Sprinkle wrappers with half the sesame seeds. Bake until golden brown (watching carefully; they can burn easily), 7 to 9 minutes. Loosen from cups with a small spatula and put on a cooling rack. Repeat with remaining 12 won ton wrappers, butter, and sesame seeds.
In a small bowl, combine salmon, green onions, cilantro, lime juice, ginger, and salt; mix well. Add avocado and toss very gently until well combined. Put a generous spoonful in each won ton cup. Serve immediately.



HIVI NDIVYO FEDHA ZINAVYOMGONGANISHA SAMUEL SITTA NA KATIBU WAKE

7:53:00 AM Add Comment

Dodoma.TANZANIA 
Kauli ya Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel  Sitta kwamba fedha ambazo zitakuwa zimeokolewa katika siku 60 za uendeshaji wa Bunge hilo hazitarejeshwa serikalini, bali zitatafutiwa utaratibu wa namna ya kuzitumia, imemgonganisha na katibu wake, Yahya Khamis Hamad ambaye amesema “hilo ni jambo la ajabu”.

Sitta alitoa kauli hiyo juzi usiku wakati akiahirisha Bunge hilo lenye wajumbe 500 baada ya wajumbe 130 wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kulisusia tangu Aprili 16, mwaka huu.

Wajumbe hao wamekuwa wakilipwa posho ya Sh300,000 kwa siku sawa na Sh150 milioni kwa siku kwa wajumbe wote, huku Serikali ikiwa imetenga Sh20 bilioni kwa ajili ya siku 60 za uendeshaji wa Bunge hilo.

Kauli hiyo ya Sitta kuwa fedha zitakazookolewa zitatafutiwa utaratibu badala ya kurudishwa zilikotoka, iliwafanya wajumbe wa Bunge hilo kulipuka kwa furaha na kugonga meza.

Hata hivyo, katibu wa Bunge, Yahya Khamis Hamad alishangazwa na kauli hiyo ya Sitta akisema: “Mimi hayo niliyasikia lakini kwangu pia ni ya ajabu kwa sababu fedha tulizonazo hazitoshi, sasa hizo za kubaki mimi sijui.”

Katibu huyo alisema kwa sasa, Wizara ya Fedha inawapa kiasi cha fedha kwa kile tu ambacho kinahitajika na yeye anatoa taarifa serikalini kwa kiasi kilichotumika. “Mimi sijui labda yeye anajua sitaki kumsemea,” alisema.

Sitta pia aliwaeleza wajumbe hao kuwa baada ya kukabidhi Katiba inayopendekezwa, wote watakabidhiwa cheti na Rais Jakaya Kikwete.
“Cheti hicho kitakuwa na sahihi ya Rais mwenyewe kwa hiyo tutakaa kidogo kusubirisubiri Katiba iliyokamilika, haiwezi kuwa ya ovyo ovyo tu lazima iwe na viwango vizuri,” alisema Sitta na kuongeza:
“Tutachapisha nakala nyingi kila mmoja aende na waraka huo wa kihistoria nyumbani na itakuwa ni Katiba bora sana hapa Afrika na Kusini mwa Sahara.”

Mwenyekiti huyo aliwapiga vijembe viongozi wa Ukawa na makundi mengine yanayopaza sauti kutaka Bunge hilo lisitishwe ili kuokoa pesa
“Tutamaliza zoezi hilo Oktoba 3, mwaka huu ili tutoke na Katiba inayopendekezwa kinyume na wale wanaopiga kelele ovyo bila kuwa na sayansi kichwani eti unaokoa gharama kwa kusitisha mchakato.
“Mchakato huu ungesitishwa ina maana utawala ujao, rais ajaye ingembidi kuanza upya na Tume na aingie tena kwenye Bunge Maalumu la Katiba,” alisema Sitta.


NI SHEEEEEDAAAH: TIZAMA PICHA ZA MADARAJA YA KWANZA KWA NDEGE KALI ZA KIMATAIFA

7:45:00 AM Add Comment


















MNADA BANNER