REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

2 CHAINZ: MIE NI MTU MZIMA/ MSINIKAGUE KIJINGA.

7:17:00 AM Add Comment

  Na Hezron Munis  
RAPPER 2 CHAINS hakufurahishwa na Ukaguzi aliofanyiwa alipokuwa Airport Nchini Dubai huku akidai nkuwa umepitiliza na kumkwa yeye kama mtu mzima ambaye anastahili kuheshimiwa

Tukio limetokea Hivi karibuni ambapo 2 Chainz anadai kuwa, hakukataa kukaguliwa, lakini ule Ukaguzi ulizidi kiwango kiasi kwamba akahisi kusumbuliwa na hata kuingiliwa katika uhuru wake hasa mahali ambapo watu wengine wa kawaida hawakustahili kufika

  PICHA LIKO HIVI     
Kwa Mujibu wa Malalamiko ya 2 Chainz kupitia Instagram account yake, anadai kuwa Wahusika wa ukaguzi katika Airport hiyo, walimkagua mpaka mifukoni mwake na hata katika Begi lake Binafsi wakidhani kuwa huenda amebeba "Bangi" kitu ambacho yeye asingeweza kufanya kwa sababu anajua sheria nzi Nchi hiyo haziruhusu kabisa utaratibu huo wa Bangi.

Tofauti na hilo, 2 Chainz anadai kuwa, Wakaguzi walifikia mpaka hatua ya "Kumnusa" mikononi mwake ili kuthibitisha kuwa hajavuta kabisa hicho kitu kabla hajafika katika uwanja huo wa ndege.

Aidha Rapper Huyo ameongeza, yeye ni mtu mzima na wala hakuna kinachomzuia kuvuta "Bangi" , lakini isfikie hatua wakamkagua kupita kiasi ilihali yeye anafahamu sheria zote

VERA SIDIKA: HUWA SIPENDI NGUMZUNGUMZIA OTILE BROWN/ SIJUTII CHOCHOTE

6:59:00 AM Add Comment

VERA SIDIKA:Amesema kuwa Huwa hazungumzii Mahusiano yake yaliyopita


Na Baba Juti   

SOCIALITE kutokea Nchini Kenya ambaye pia ni msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, VERA SIDIKA maarufu kama "Queen Vee Bosset" ameweka wazi kuwa hajutii kamwe kuachana na aliyekuwa mpenzi Wake OTILE BROWN

Akifanya mahojiano na Kituo cha Redio cha Milele Kilichopo Nchini Kenya, Vera Sidika ambaye hivi sasa ana mahusiano mapya tayari, amesema kuwa mara nyingi hajutii kitu hata kidogo kwa Otile Brown ambaye hawakuachana vizuri, na ndio maana mara kwa mara huwezi kukuta anamzungumzia.

OTILE BROWN


Vera Sidika ambaye pia ni Mjasiriamali kutoka Nchini Kenya, amesema kuwa mara kadhaa amekuwa akisikia baadhi ya "Madongo" na habari nyingine tofauti kuhusu yeye ambazo Otile amrkuwa akizizungumza juu yake, lakini hawezi kujibu kwa sababu ni Takribani Miaka miwili na Ushee sasa imepita Tangu waachane

Pia ameongeza kuwa, huwa hana tabia ya kuzungumzia mambo ambayo yalishapita na hata kutoweka katika maisha yake, hivyo haoni haja ya kuendelea kumzungumzia mtu kama huyo

Kauli hiyo ya Vera Sidika ambaye hivi sasa ana mahusiano ya Kimapenzi na Msanii kutoka Nchini Tanzania JIMMY CHANSA, imetoka baada ya Otile Brown kutembelea Nchini Tanzania na kudai kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo Vera amewahi kumfanyia na hawezi kuyasahau.

Msikilize Hapa
CHANZO: Milele FM-KENYA

MWANDISHI WA HABARI ASIMAMISHWA KAZI KWA KUPOST TUHUMA ZA UBAKAJI ZILIZOKUWA ZIKIMUANDAMA KOBE BRYANT

6:34:00 AM Add Comment

  Na Hezron Munisi   
GAZETI la Washington Post linalochapisha Taarifa za kila Siku kupitia machapisho yake Nchini Marekani, limemsimamisha Kazi mwandishi wake wa Habari kwa kitendo cha "Kutweet" taarifa za Unyanyaaji wa kijinsia kupitia Ubakaji alizowahi kutuhumiwa Marehemu KOBE BRYANT mnamo mwaka 2016

FELICIA SONMEZ alipost "Link" a,bayo ilichapishwa mwaka 2016 kuhusu tuhuma hizo zilizokuwa zikielekezwa kwa Mkongwe huyo wa mpira wa kikapu katika Ligi ya NBA katika kipindi ambacho Mataifa mewngi na wadau wengi wa Marehemu Kobe Bryant wakiwa katika majonzi mazito.

FELICIA SONMEZ: Amesimamishwa Kazi Baada ya Kutweet Kuhus Tuhuma za Ubakaji zilizokuwa zikimuandama Marehemu Kobe Bryan



Uongozi wa Gazeti hilo la Washington Post, umedai kuwa, haikuwa sawa kabisa kwa mwandishi huyo wa Habari kupost kitu kama hicho katika kipindi hiki kigumu hasa kwa familia ambayo mpaka hivi sasa bado ipo katika majonzi makubwa ya Kumpoteza Kobe Bryan na Binti yake Gianna Bryant katika Ajali mbaya ya Helcopter

"Badala ya Kumlinda na kuendelea kumuunga Mkono mwanahabari katika Sura ya Udhalilishaji, Uongozi umemsimamisha kwa kumpa likizo ya Lazima" Barua kutoka katika Idara ya Uhalili ya Gazeti hilo ilinukuliwa hivyo

Tweet Aliyopost Mwandishi Huyo


Felicia Sonmez alitweet taarifa hiyo ambayo ilikuwa ikizungumzia tuhuma za Ubakaji zilizokuwa zikimuhusu Marehemu Kobe Bryant mnamo mwaka 2003, ambazo zilitia Doa kubwa katika Shughuli zake. Tuhuma hizo za ubakaji zilikuwa zikidai kuwa Marehemu Kobe alimbaka Mchezaji mwenzake wa kike aliyekuwa na Umri wa miaka 19 katika Kipindi hicho.

Hata hivyo mwandishi huyo aliondoa Tweet hiyo baada ya kuandamwa sana, huku akidai kuwa alianza kutishiwa kuuwa na baadhi ya watu


MNADA BANNER