REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

FREEDOM IS ON THE WAY. 01.06.2014

6:44:00 AM Add Comment

MWEZI JUNI Utakuwa ni Mwezi wa Kupokea Balaa jingine Toka Kwa KENYAN-BORN-RAPPER anayefahamika kwa Jina la JAMAA TU FLANI, Mweny maskani yake Nchini CANADA.

Kwaju hilo ambalo Limepwa Title La FREEDOM, litaanza Kukita Kunako Social Medias na Jumatatu, huku tarehe 02 JUNE, likiachiwa Exclusively Kunako kipindi cha Jam Session Cha 99.4 Metro FM, Mwanza.


FREEDOM ni Wimbo ambao Umepikwa na Producer Deey Classic kutoka Revolution Sound-Mwanza, Huku Vichwa Viwili Kutoka Mwanza, FEMALE MC – NATTY E BRADY na Bibie anayeonea sana kunako R&B na ZOUK –Honeya, ndio waliokamilisha “KOLABO” zito kunako Track Hiyo

OXS- MWEZI WA SITA ITAKUWA NI PROJECT AFTER PROJECT

6:04:00 AM Add Comment

BAADA ya Kutambulisha Mixtape yake ya OXY-GEN, rapper na Producer wa Metro Fm , Mwanza, Abdallah “Oxs” Okelleky, amesema kuwa Mwezi wa Sita Ni “Project After Project”

Akipiga Story na Black Touchez, Oxs amesema Kuwa, Hivi sasa anakamilisha Utafiti wa Soko lake hasa baada ya Kuachia Mixtape yake, na kitakachofuata na Kuanza kupiga Project Moja Baada ya Nyingine na Producers Wa Mwanza.

Pia Oxs ambaye Bado anakita na Kwaju la “PARTY” ambalo ameshirikiana na Juma Nature na Q-The Don, amesema Kuwa Traxx zake Zitashirikisha wasanii Mbali mbali, ambao anaamini wako vizuri katika Music Industry , na wanajua wanachokifanya

“Ninawakubali Wasanii Wote Nchini Tanzania, na Afrika Mashariki Kiujumla. Ila Niko tayari kufanya kazi na wasanii ambao Ninaamini Wanajitambua, na wako serious na Game. Nikishapata Ushauri toka Kwa Meneja wangu kuhusu Msanii ambaye nitafanya naye kazi, basi amini Msiamini, Mwezi wa Sita itakuwa ni PROJECT AFTER PROJECT”


Mixtape ya OXY-GEN ipo Sokoni Hivi sasa, na Inapatikana kwa yeyote anayehitaji

RADIO WA GOODLIFE, UGANDA, AKAMATWA BAADA YA KUKUTWA AMEPANDA BANGI NYUMBANI KWAKE

5:29:00 AM Add Comment
(c) NEW VISION
KAMPALA, Uganda
Inaonekana Kitu BANGI imaeanza kuchukua Sura Mpya katika maisha ya watu maarufu, ikiwa ni baada tu ya WIZ KHALIFA kukamatwa Airport akiwa na Mmea korofi , yaani bangi.

Sasa , Some where in East Afrika, Kwa –abalunji, ba-sssebo, Nazungumzia Uganda, Msanii Kutoka Kundi la Goodlife, Radio, ameingia kunako mbwadidi la hatari baada ya jeswhi la Polisi nchini humo Kubaini Kuwa amepanda mmea wa bangi katika Nyumba ambayo anaishi
(c) NEW VISION-UGANDA

Tukio hilo ambalo limetokea ndani ya Wiki Hii, lilisababishwa na Ugomvi ambao ulitokea katika baa ya CASSABLANKA, ambayo Radio na Weasel hupenda kutembelea, ambapo RADIO aligombana na Msanii AK47, na wasanii wengineo akiwamo SHEEBAH,PALLASO, KING SAHA.
(c) NEW VISION

Data Zinazidi kumiminika Kuwa, ugomvi huo ulidumu kwa Muda Kadhaa, na Kisha Kufika Mpaka Nyumbani kwa Msanii huyo MOZEH RADIO, hali ambayo ilisababisha Uharibifu wa vitu kama Vile madirisha na Vioo Vya gari lake.
(c) NEW VISION

Sasa wakati jeshi la polisi lilipotia Timu Nyumbani Kwa Weasel kwa ajili ya kutuliza Ghasia, Mbwadidi linguine likaibuka, na hatimaye Kukamatwa kwa Mimea kadhaa ya BANGI ambayo radio alikuwa ameipanda katika mazingira ya Nyumba yake.
Hata hivyo bangi hiyo Iling’olewa na Kuchomwa moto kama ilivyo kawaida..

(c) NEW VISION

SSSSSSSSSS..PUFF,,OHOHOHOOO…

CINDY SANYU AMEMCHANA SHABIKI MZEE ALIYEMTUMIA PICHA YA UUME WAKE

5:17:00 AM Add Comment

KAMPALA, Uganda
Within This Week, Vitu Kibao tu Zimetokea ila la Kushangaza ni hili ambalo Limemtokea Cindy, Kitengo Chimbua Chimbua Kinatoa Ripoti…

Hivi majuzi, Sweet baby na muimbaji Mtamu sana Kutoka Nchini Uganda, Cindy Sanyu, aliamua kumlipukia Shabiki ake Mzee ambaye alimtumia Picha ya UUME katika Upande wa Meseji kunako Mtandao wa facebook.

Baada ya Kukutana na Mbwadidi la Mzee huyo kunako Inbox yake, aliamua Kumuanika Mzee huyo katika Wall yake, lakini jambo la kumshukuru mwenyezi mungu ni Kwamba, hakuanika Zile Private Messeges ambazio zilikuwa zimetumwa na Mzee Huyo.

Wakati akimuanika Mzee huyo, Cindy alipost kuwa, badio yuko katika Mshtuko baada ya Kibabu hicho kumtumia Picha ya Uume wake, kwa sababu kwanza hakutarajia kama Mtu Mzima kama huyo anweza kufanya kitu cha kipumbavu, huku akiomba Msaada, ni hatua gani azichukue dhidi yake.


Hata hivyo baada ya kupokea Ushauri mwingi katika Comments, Cindy aliwashukuru fans wake, huku akiamini kuwa, kibabu hicho kitakuwa kimejifunza Heshima nidhamu na Adabu.

HII NDIYO SABABU YA JAY Z NA BEYONCE KUTOKUHUDHURIA NDOA YA KANYE NA KIM.

5:10:00 AM Add Comment

NEW YORK, Marekani.
INFACT Kila mtu atakuwa bado anajiuliza kuhusiana na sababu Kubwa ya msingi ambayo ilimfanya Jay Z na Beyonce washudhurie Ndoa ya Rafiki zao wa karibu, Kanye West na Kim Kardashian iliyofnyika Huko Florencia, Italy.

Baada ya TTM kuzama Rasmi kunako Vyanzo mbali mbali, Finaly tumepata ukweli kuhusu sababu ambayo ilisababisha wawili hao Kutokuhudhuria.

Kwa mujibu wa Info za Kuaminika, inasemekana kuwa, sababu kubwa ambayo inapewa nafasi ya Juu, Ni Kuwepo kwa Mwanamke mmoja anayefahamika RACHEL ROY Katika harusi Hiyo, Sikia sasa Undani Wake.

RACHEL ROY (c) HNH
Rachel Roy, Ni Mwanamke ambaye ndiye alikuwa chanzo cha Ugomvi wa JAY Z na SOLANGE, uliotokea Wiki kadhaa Zilizopita katika Lift ya Hotel ya Standard, wakati Wa MEET GALA AFTER PARTY, ambapo inasemekana kuwa, Jiggah alionekana kuanza Kuwa karibu zaidi na Mwanamke Huyo.

Pia Info zinamiminika Kuwa, RACHEL ROY, ambaye ni EX-WIFE wa rafiki wa Jay Z hasa katika Biashara, alisadikika kutaka kuhudhuria Party ya Rihanna (RIHANNA AFTER PARTY), ambayo Pia JAY Z alitaka Kwenda Bila Beyonce, jambo ambalo SOLANGE hakukubaliana nalo, na Baada ya Muda kadhaa ukatokea Ugomvi huo ambao Hivi sasa Ni Story tu.


Kwa Maana Hiyo, Endapo Jay Z na Beyonce wangehudhuria , basi wangekutana na Kimwana Huyo ambaye alihisiwa kutaka kubiringika na Jay Z, na Ndipo la kuibuka lingeibuka.

KUMBU KUMBU YA MWAKA MMOJA TANGIA ALBERT MANGWEA ATUTOKE

5:01:00 AM Add Comment

DAR ES SALAAM, Tanzania
LEO ni Siku ambayo wadau na wapenzi wa Muziki wa Kizazi kipya Nchini, wanakumbuka Kifo cha rapa na Mkali wa Freestyle, Marehem ALBERT MANGWEA- COW WEEZY, tangia ametuachia Simanzi nzito hapo Mwaka jana Tarehe kama Ya Leo, nazungumzia May 28,2013.

Hivyo TTM imezinyaka Info kuwa MASTAA mbalimbali nchini wakiwemo wanamuzik,i wanatarajiwa kushiriki kwenye tukio maalum la kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo cha marehemu Albert Mangwea ‘Ngwair’ , litakalofanyika ndani ya ukumbi wa Nyumbani Park (Samaki samaki Spot) , Kihonda Morogoro mjini.

Mratibu Mtendaji wa tamasha hilo, Kareeem Omary ‘KO’ alisema maandalizi ya tukio hilo litakalokuwa la kila mwaka, limepwa jina la ‘Love Concert – Kumbukumbu ya kifo cha Albert Mangwe’.

Aidha Kareem, aliwaomba wadau kujitokeza kwa wingi kuunga mkono kwenye tukio hilo kwani litakuwa la kipekee na la aina yake ambalo pia litatoa fursa kwa wakazi hao pia mikoa jirani na watu kutoka nje ya Tanzania ambao watahudhuria.

Pia  amewataja wasanii watakaotoa burundani, ni pamoja na kutoka kwa kundi la Wanachemba ambalo pia aliwahi kuwa nalo marehemu Ngwair, JSqueezer, P Funky Majani na Mswaki. Kwa upande wa wasanii kutoka Morogoro ni pamoja na Afande Sele, Team Racers, Mc Koba Chris wa Marya, Belle 9, Samir, Zombie, President Mirrow, Jordan wa Dejavu na wengine wengi.

Kabla ya matukio ya shoo ukumbini, itatanguliwa na ibada mbili maalum ikiwemo ya Kanisani na ile ya nyumbani.

VIWANGO VYA KUBADILI FEDHA ZA KIGENI SIKU YA LEO

2:36:00 AM Add Comment

KATIKA SOKO LA KUBADILISHA FEDHA ZA KIGENI Nchini Tanzania, Kwa Viwango Vilivyowekwa na BENKI YA TANZANIA (BOT), Ni kama Ifuatavyo

FEDHA                                    INANUNULIWA  KWA..    INAUZWA KWA…

SHILINGI YA KENYA                18.71                              18.88
SHILINGI YA UGANDA            0.64                                0.65
DOLLA YA MAREKANI            1626.65                         1642.92
POUND YA UINGEREZA         2728.22                          2755.83
EURO                                       2244.29                          2267.06
YEN YA JAPAN                       15.86                              16.01
RUPIA YA INDIA                      26.62                              26.88
RANDI YA A.KUSINI                153.63                             155.10


UNADHANI MAKAHABA WAKISTAAFU, WANAELEKEA KUISHI WAPI?

2:33:00 AM Add Comment

KUNA Swali ambalo unaweza kujiuliza mpaka sasa, kwamba, Akina dada wanaofanya Biashara ya Ukahaba, wakishazeeka na Kustaafu, Nini hatma yao?

Mpiga Picha Mmoja nchini Ufaransa, maefanikiwa Kugundua mahali ambako makahaba wanaozeeka na Kustaafu Shughuli ya Kuuza Mwili, huko Nchini Mexico.

Katika Jiji la Mexico lililoko Nchi ya Mexico, Imebainika Nyumba Moja kubwa na Nzuri ambako Makahaba Wote wastaafu wanaishi hapo.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyoifikia Ijumaa Mseto, inasemekana Kuwa, Wastaafu wa Ukahaba wanaoingia Katika Eneo hilo, Ni wale tu, wanaoanzia Umri wa Miaka 50 na Kuendelea, na Wanapata Huduma Zote Muhimu sambamba na Vipodozi mbali mbali.


Jumba hilo lilifunguliwa rasmi Mwaka 2006, na mpaka hivi sasa, jumla ya Wazee zaidi ya 250 waliostaafu Ukahaba, wameshapitia eneo hilo.




HAKUNA KUFANYA MAPENZI MPAKA TUMALIZE WORLD CUP- KOCHA WA MEXICO

2:29:00 AM Add Comment

KOCHA wa Timu ya Taifa ya MEXICO, amewapiga marufuku wachezaji wa Timu yake Kushiriki Tebndo la Ndoa katika kipindi cha mashindano ya Kombe la dunia Mwaka huu Nchini Brazil.

Akizungumza na Gazeti la REFORMA, Kocha Huyo amedaiwa Kuwaagiza wachezaji wake kutokujihusisha na Suala la kufanya mapenzi, na badala yake wanatakiwa kujikita zaidi na kuelekeza Macho yao katika Soka hasa Michuano Hiyo ya Dunia

Aidha Kocha huyo anayetambulika kwa Jina la MIGUEL HERRERA, ameongeza kuwa, kama Mchezaji hatovumilia kutokufanya mapenzi kwa Mwezi Mzima ama Siku 20, basi hajajiandaa kuwa Mchezaji Professional.

Mexico Inatarajia Kukutana na Timu ya Brazili katika Kundi A, pamoja na Coratia na Cameroon

MASE AMPIGA STOP WIFE WAKE, KUINGIA KANISANI, BAADA YA KUKAMATWA KWA KOSA LA KUNYWA POMBE

2:20:00 AM Add Comment

NEW YORK,Marekani.
Nikema Praise The Lord Unasema ..AMEN, hiyo Ndiyo kanuni Yetu watu wa mungu tuliokoka, na kujitolea kumpenda Mungu kwa Nguvu Zote, haijalishi maisha tunayoishi lakini Hebu Sikia Hii Kutoka Kwa Ukaribu.

RAPPA na MCHUNGAJI Mase ambaye hivi majuzi tu Nilikupa Story kuwa anarejea katika game na Albam Mpya, Amempiga Stop Mke wake kuingia, ama kukanyaga, ama kulisogelea kanisa lake, ikiwa ni baada ya kukamatwa akiwa amelewa.

Awali kulikuwa na info kuwa, Baba Mchungaji Mase, pamoja na Mkewe ama mama Mchungaji TAWYLA BETHA walikuwa tayari kupeana Talaka, lakini baadaye ikasemekana kuwa wawili hao wamerudisha mahaba yao.

Mke Wa mase, aka mama Mchungaji, alikamatwa Mwezi uliopita kwa Kosa la Kupiga kilevi na kuendesha gari, jambo ambalo ni Kinyume cha Sheria za nchi ya marekani, na bila Ubishi, mke huyo wa mtumish Wa Mungu alipatikana na hatia.

Chimbua Chimbua katika kutoa Hitimisho, Ilmemimina Info kuwa, Mase aliamua kumpiga Stop Mamito wake huyo, baada ya kuliaibisha kanisa, na kusaliti Imani ya Mwenyezi Mungu.

HALELUYAAAAA

ILLUMINATA ANAHITAJI MENEJA.

2:16:00 AM Add Comment

DAR ES SALAAM, Tanzania,
Back in 255, Area Code ya SAY YES TO BABIES and SAY NO TO UZEE….
Rapa wa kike anayekuja in High Speed with Untouchable Flows, ILLUMINATOR, amemiminika na kusema kuwa Hivi sasa anahitaji Meneja ambaye ataweza kumsimamia katika kaz zake Mbali mbali hasa za Kimuziki, TTM Tushaidaka Kudadadeki.

Akifafanua kuhusu hilo Suala, ILLU ambaye ni best Friend Wa Miss Koi Koi, My Natty E, amesema kuwa Game la Muziki wa Kizazi kipya, Ni Gumu sana, Kiasi kwamba anahitaji kumpata Meneja ili kazi zake ziweze kusimama vilivyo, na aweze kutusua katika Music industry hapa Bongo.

Aidha Iluminator ambaye Remix ya JONI yak wake Yemi alade imemfanya kuwa Tofauti, pia amesema kwamba, watoto wa kike hawatakiwi kuogopa hasa katika Vipaji Vyao, hivyo wanatakiwa kujitokeza kwa Wingi katika Fani Hasa ya Production, ili kuweka heshima kama Zilivyo Nchi Nzima.


Tofauti na Kurap, Iluminator ni PRODUCER, ambaye huwa anafanya kazi zake Mwenyewe katika Studio zake za SWAHILI SWAGGZ RECORDS

JOH MAKINI IS COMING MAZEE

2:14:00 AM Add Comment

DAR ES SALAAM, Tanzania
Msanii wa rap nchini John Saimon aka Joh Makini Mwamba wa kaskazini kwa sasa anampango wa Video ya  wimbo wake unaofahamika kwa Jina la ‘I See You’ hivi karibuni …TTM, tumenyaka Infoz Pia.

Akimiminika Kuhusiana na Hiyo Ishu, Joh makini amesema kuwa, Mkwaju huo Mpya Utakita kunako Hewa Muda Si Mrefu, na umepikwa na Producer Nahreel.

Aidha Joh ambaye aliweza kuvibratisha Hisia za wadau wa Muziki wake kupitia kwaju la KILIMANJARO MOUNTAIN na BYE BYE pamoja na NIKUMBATIE, amesema Hivi sasa anasubiri Muda wa kushusha Noma hilo Ufike, ili aweze kutimiza kile ambacho watu roho inataka.


Pia Akizungumzia Kuhusu Video ya NIKUMBATIE, Makin maesema kuwa, Kwaju hilo ni Kali sana, Hivyo Video yake haitakiwi Kuwa ya Kitoto. So kwa hivi sasa Yuko anapepesa macho kumpata Director Mkali atakayesimamia Mzigo..

FLAVIANA MATATA NA AY, WAMEUNGANA NA WATANZANIA WOTE WALIOPOTEZA NDUGU ZAO KATIKA AJALI YA MV BUKOBA

7:56:00 AM Add Comment

Jana Ilikuwa ni kumbu kumbu ya Kuzama kwa Meli ya MV Bukoba iliyotokea May 21 Mwaka 1996 Mkoani Mwanza ikitokea Bukoba Mkoani Kagera.

Balozi Mstaafu wa Tanzania nchini Uingereza na Marekani Mwanaidi Majaar jana ameongoza zoezi la Kuweka Mashada katika Makaburi ya Kumbukumbu ya Watu waliopoteza Maisha katika ajali hiyo.

Flavian Matata ambae katika ajali hiyo alimpoteza mama yake mzazi sanjari na binamu yake, amewashukuru watu wote waliohudhuria katika kumbukumbu hiyo ya Ajali ya Mv.Bukoba ambapo amesisitiza kwamba jambo kubwa zaidi ni kuwaombea wale wote waliopoteza maisha wapumzike kwa amani.


Ambwene Yessaya (AY) alikuwepo siku ya jana katika maeneo hayo, na Hiki Ndicho Walichokizungumza

WILL SMITH NA MKEWE JADA PINKETI, WANACHUNGUZWA KUHUSU PICHA YA MTOTO WAO, WILLOW.

7:52:00 AM Add Comment

LOS ANGELS,Marekani
KITENGO cha Huduma kwa Watoto na Familia kutoka jijini Los Angels, kimesadikika kuanzisha Uchunguzi dhidi ya wazazi wawili, Will Smith na Jada Pinket, hasa kuhusu Picha ya Mtoto wao wa Kike Willow Smith, iliyomuonesha akiwa kitandani na Muigizaji MOISES ARIAS.

Kwa mujibu wa Mishe za Chimbua Chimbua, inasemekana Kitengo Hicho kimeamua kufanya Uchunguzi huo haraka Iwezekanavyo , ikiwa ni baada ya Picha ya Willow mwenye Miaka 13 akiwa kitandani na MOISES mwenye Miaka 20, huku kukiwa na mazingira tatanishi , Baada ya jamaa huyo kuonekana akiwa kifua wazi.

Kwa Mujibu wa Chanzo kimoja ambacho kipo karibu na familia Hiyo, kilifunguka kama Sio kumiminika kuwa, Upelelezi ama Uchunguzi Huo, Ulianza Juma lililopta, yaani wiki iliyopita Kuhusu Ishu Hiyo.

Hata Hivyo bado Chanzo hicho kimezidi kumiminika kuwa, Will Smith pamoja na Mke wake Jada Pinket, wameonekana kutoa ushirikiano Mzuri kuhusu Uchunguzi huo, ambao Kiujumla unadhamira ya kufahamu kilichokuwa kikiendelea baina ya watoto hao wawili.


Kama Utarudisha kumbu kumbu zako, TTM tuliwahi kukupa Mtonyo kuwa, mama Mzazi wa Willow, Jada, alisema kuwa Picha hiyo haikumaanisha Kile ambacho Wengi wanakidhania.

JAMAA AJITOKEZA KUMSHTAKI DR.DRE KUHUSU BEATS ELECTRONIC

7:50:00 AM Add Comment

Ukiskia Good Things Gone Baad, mchakato Ndo unaanzia Hapa, Zima TTM tukukatie Mtonyo fasta.

Jamaa Mmoja anayefahamika kwa jina la STEVEN LAMAR ambaye ni Meneja wa ONE-TIME-HEDGE-FUND, amejitokeza na kudai kuwa, amefungua mashitaka ya madai dhidi ya Dr. Dre na Jimmy Lovine hasa Kuhusu Beats By Dre na Beats Electronic ambayo itapigwa Bei Kwa Kampuni ya APPLE kwa Mkwanja Mrefu haswa.

LAMAR anawatuhumu wamiliki hao wa BEATS ELECTRONICS kwa kukiuka makubaliano yao ambayo pia yalikuwa Ndani ya Mkataba, hasa ikiwa ni baada ya Kuuza pasipo kumpa taarifa, huku akihitaji malipo ya Asilimia akadhaa kwa kuwa na Mchango katika Kufanikisha Beats By Dre.

Pia data Zinaeleza kuwa Miaka 8 Iliyopita, yaani Kuanzia Mwaka 2006, Dr. Dre na Jimy Lovine, waliwahi kumshtaki Lamar na washirika wake, ikiwemo kampuni aliyokuwa akiifanyia kazi kipindi hicho, kwa madai kuwa alikuwa akitengeza Bidhaa Nyingine iliyokuwa na Mfumo wa kampuni ya BEATS ELECTRONIC, jambo ambalo lilikuwa ni Nje ya Mkataba wao.


Hata hivyo Lamar bado anadai Kuwa, anahitaji kulipwa Asilimia 20, kwa Ushirikano alioutoa mpaka Dre na Lovin wanakutana na kutengeneza kitu Kimoja, pamoja na kila alichokichangia katika Kampuni hiyo

NICKI MINAJI NA FORBES, WANA JAMBO

7:47:00 AM Add Comment

Muda Kidogo hivi umepita baada ya Jarida la FORBES kuchapisha habari yenye Kichwa Cha habari kuwa, HIP HOP INASHIKILIWA NA MWANAMKE MWEUPE, MWENYE NYWELE NYEUPE KUTOKA AUSTRALIA, ambaye bila Shaka alikuwa Ni IGGY AZAELA

Tofauti na Hilo, jarida hilo bado lilidai kuwa NICKI MINAJI Hivi sasa ni kama ameshuka baada ya kukaa Kimya Kwa Muda mrefu bila Kutoa ngoma Yoyote Mpya, jambo ambalo si Kweli, kwani Nicki ameshaachia Mikwaju kadhaa ya HIP HOP, ikiwemo L.A.N (Na Usitake Nitaje kirefu Chake).

Lakini baada ya watu Kibao kulalamikia Ishu hiyo hasa Tittle la jarida hilo, baadaye Forbes walibadili TITTLE na kuandika. MSANII MPYA ASIYELINGANISHWA NA WENGINE: MWEUPE, MWENYE NYWELE NYEUPE, TOKEA AUSTRALIA

Sasa Kunako Moja ya interview baada ya kuulizwa kuhusu Ishu Hiyo kunako Moja ya interview Nchini marekani, Nicki Minaj alijibu kwa Kucheka, huku akisema kwamba, Kampuni ya FORBES kiujumla, inatakiwa  kuwa na Hofu kuhusu Mkwanja atakaoupata atakaoupata, pindi atakapouza Kinywaji chake cha MYX FUSSION kwa Dollari za Kimarekani MILIONI 250.

Aidha Minaji ambaye hivi sasa ameshaachia Track yake ya PILLS & POTIONS imeshaachiwa rasmi, amesema kuwa kila Mtandao unauwezo wa Kuandika Chochote kile kuhusu Hip Hop, na hakuna tatizo juu ya hilo, Lakini kwaSuala la Iggy Azaela, Hakuna Kitu kama Hiyo.


Hata Mie Pia Ntakubali Kwaaa Kweli.

PICHA: MUONEKANO WA KIM KARDASHIAN KABLA YA SIKU YA NDOA, NA MAHALI AMBAKO ATAFUNGIA NDOA

7:15:00 AM Add Comment





















MNADA BANNER