REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

RIPOTI YA KITENGO CHIMBUA CHIMBUA: MWANAMKE AMEUAWA KIKATILI BAADA YA KUDHANIWA ANATAKA KUWATEKA WANAFUNZI

7:35:00 AM Add Comment

 MKUU WA TTM

Ama Kweli Binadamtunaunyama ambao kijumla hautabiriki.
Mwanamke huyu anaeonekana katika Picha, Ameuawa Kikatili na Wananchi Wenye Hasira kali, baada ya Kutuhumiwa kuwa alitaka kuwateka watoto wadogo waliokuwa Wakienda Shule

MKASA WENYEWE..
Ripoti ya KITENGO CHIMBUA CHIMBUA, imebainisha kuwa., mama Huyo aliwasimamisha watoto wadogo hao waliokuwa na umri unaokadiriwa Kuwa Miaka 7-10, na kuwaambia atawapeleka Shule, huku akiwaambia waongozane

Baada ya Kufikia uamuzi huyo, Mpita njia mmoja aliyemuona, alihisi huenda mama huyo anataka kuwateka watoto hao, na kuanza kupiga kelele za Msaada, na wananchi kuanza kumshughulikia.
Mpaka Mwanamke Huyo anakufa Kikatili, hakuna aliyekuwa na Uhakika kama Mwanamke huyo ni Mtekaji..au Lah 

MWISHO WA RIPOTI:
KICHICHI-Kitengo Chimbua Chimbua, NIGERIA



RIHANNA MCHOKOZI SANA-CHEKI PICHA YA KIGAUNI KILICHOACHA MAKALIO YAKE YAONEKANE

7:23:00 AM Add Comment



TAARIFA NA PICHA KUHUSU BOMU LILILOLIPUKA JIJINI MWANZA

7:16:00 AM Add Comment

MHUDUMU wa nyumba ya kupumzikia wageni wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria, jijijini hapa, amejeruhiwa vibaya baada ya kulipukiwa na bomu lililokuwa limewekwa kwenye korido la nyumba hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana (Jumatatu), kati ya saa 1:45 na saa 2:20 usiku, katika eneo la Makongoro wilayani Ilemela wakati mhudumu huyo Bernadetha  Alfred (25) alipofungua kifurushi cha mzigo alichodhani kimesahaulika kwenye eneo hilo, kabla ya kumlipukia.

Kwa mujibu wa Katibu wa Dayosisi hiyo, Mollel Rogart, kifurushi hicho kilichokuwa kwenye mfuko mweusi wa nailoni, kilikuwa juu ya kreti (tupu) za soda, karibu na eneo la kulia chakula lililopo katika nyumba hiyo.


“Ule mfuko ulikaa pale siku tatu ndiyo usiku huo mhudumu wetu akakichukua kukiangalia akidhani ni mzigo wa mtu umesahaulika.” Alieleza Katibu huyo na kudai kuwa kifurushi hicho kilimlipukia mara tu alipokifungua na kujeruhi vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili.

“Bernadetha kajeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo miguuni na usoni na siwezi kusema kwamba chanzo cha mlipuko huo ni mambo ya kidini japo ulinzi wetu haukuwa mkali kiasi cha kudhibiti watu walioingia na vitu.” Alisema

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Valentino Mlowola akithibitisha tukio hilo, alisema kwamba uchunguzi wa awali uliofanywa na kikosi maalum kutoka Dar es salaam umebaini kuwa bomu hilo limetengenezwa kienyeji.


“Bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili tubaini ni nani kafanya ili kama ni mtu au kikundi kimehusika tuchukue hatua haraka. Natoa wito kwa wananchi kutochukua vitu ambavyo hawa uhakika navyo, wanapoona vitu vya aina hiyo, watoe taarifa kwetu.” Alisema Kamanda Mulowola.

Mlowola alieleza kuwa, Bernadetha aliyejeruhiwa vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili, alikimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya Bugando ambako anaendelea na matibabu.

Kamanda  huyo alieleza kwamba, mabomu (yakiwemo ya kienyeji) yako katika mifumo mbalimbali hivyo wananchi hususan wahudumu wa sehemu za mikusanyiko wawe na tahadhari na vitu vinavyoonekana kusahaulika na wasisite kuwajulisha polisi vinapoonekana hivyo. 


Mlipuko huo uliozusha hofu kwa waumini mbalimbali wakiwemo wa Kanisa hilo, umetokea ikiwa ni wiki moja baada ya maadhimisho ya ‘Huduma ya Mtoto’ kwa makanisa mbalimbali ya Kikristu jijini hapa yaliyofanyika kwenye kanisa hilo, yakitanguliwa na maandamano kutoka uwanja wa furahisha hadi KKKT.




HIVI NDIVYO UNAVYOTAKIWA KUISHI NA RAFIKI HUYU

7:07:00 AM Add Comment

MARAFIKI ni watu Muhimu sana katika maisha ya kawaida. Kuna muda huwa tunakutana na watu mbali mbali ambao huwa tunawafanya kuwa marafiki kulingana na Muonekano, tabia, Historia za Kimaisha, na mengineyo.

Kuna ukweli kwamba, kuna marafiki ambao huwa wanakubali kile ambacho unakifanya, na hata kujivunia kuwa karibu na Wewe, ili kufanikisha Suala hilo, ama Kukupa Ushauri mzuri na hatimaye kufikia pazuri.

Lakini Pia kuna marafiki ambao huwa hawatabiriki. Leo anakupenda, kesho anakuchukia, Wiki ijayo anapenda ushirikiano wako, Wiki nyngine hataki umuingilie katika mambo yake, lakini kuna muda hataki hata kukusikia.

Lakini ukweli utabaki pale pale kwamba huyo bado ni rafiki ako, na unatakiwa ufanye yafuatayo:
  • ·        Muamini katika kila anachokifanya
  • ·        Mpongeze katika mafanikio anayofikia.
  • ·        Mkumbushe mambo ya Msingi ambayo huenda ameyasahau.
  • ·        Kuwa Mstari wa Mbele katika kufanikisha Kazi yake, Yaaluma, Kipaji, na hata Shughuli zake
  • ·        Kumbuka Kujishusha Chini unapobaini hayuko katika Mood Nzuri
  • ·        Mshirikishe katika Baadhi ya mambo yako ya Msingi hata kama hatofurahishwa nayo

  • ·        Kubali ushauri wake, na kuuboresha Kama Una mapungufu.
  • ·        Mheshimu, na uthamini utu wake, huku ukiepuka Kuhisi Mambo mabaya Juu yake.
  • ·        Kuwa wa Kwanza Kumuombea kwa Mungu ili awe na maisha Bora
  • ·        Mfanyie Kitu Kizuri ambacho hakiamini kama unaweza kukifanya.
  • ·        Kubali na Pokea Lawama, Matusi, hasira, Chuki na Mengine, kutoka kwake dhidi yako.
  • ·        Onyesha Furaha kila siku unapokutana naye, na epuka kumlaumu pindi asipozingatia Salamu yako, Ushauri wako, na hata anapokuona huna mchango wowote katika Maisha yake

#BRING BACK OUR GIRLS..BOKO HARAMU BADO WANAZIDI KUTEKA WANAFUNZI

6:56:00 AM Add Comment

Habari kutoka Nigeria zinasema kuwa, watu wanaoaminika kuwa wanamgambo wa Boko Haram wamewateka nyara wasichana 8 katika kijiji cha Warabe kilichoko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. 

Habari zaidi zinasema kuwa, wasichana hao wenye umri wa kati ya miaka 12 na 15 walitekwa nyara wakati watu hao wenye silaha walipovamia kijiji hicho na kupora mifugo pamoja na vyakula. Tukio hilo limejiri siku moja baada ya Boko Haram kutangaza kwamba linawashikilia zaidi ya yanafunzi wa kike 200 waliotekwa nyara katika shule moja mjini Chibok mwezi uliopita. Kiongozi wa Boko Haram, 
Abubakar Shekau ametishia kuwauza wasichana hao ndani na nje ya Nigeria.

Umoja wa Mataifa umeonya kundi la Boko Haram ukisema kuwauza wanafunzi hao wa kike ni kinyume cha sheria za kimataifa zinazopinga biashara ya utumwa na hatua hiyo itapelekea wanachama wa kundi hilo kutafutwa kwa kosa la kutenda jinai dhidi ya binadamu.


Siku ya Jumapili Rais Goodluck Jonathan alisema serikali yake inafanya juhudi zote kuwatafuta na kuwaokoa wasichana hao na akaziomba baadhi ya nchi za Magharibi kuisaidia serikali yake katika suala hilo.

MNADA BANNER