REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

Hivi Huwa ni Maksudi au Ni Michapio?

Hivi Huwa ni Maksudi au Ni Michapio?

2:27:00 AM Add Comment
1. BELLE 9.
Kwa Jinsi ambavyo huwa nafahamu, Morogoro huwa ni MJI KASORO BAHARI ambapo kwa kkiingereza tunatakiwa kusema "The Town Without Ocean". Lakini bwana Mkubwa huyu "Supa staa" Belle 9 katika Wimbo wake unaokita Fresh Kila Pande za Mitaa "Amerudi"...swahiba wet huyu katupia Intro la "From City Without Ocea", na bado kwny Video Graphics za Maneno zikaja vile vile.
Sasa najiuliza.....Morogoro ni City?...au Kiingereza cha Mji ni City au Town?
Hapana, napata Bonge la Kontradikshen kiukweli...



2. PAUL JAMES "PJ".
Huyu Ni Mtangazaji Muzuri muno (Mzuri Sana) wa Clouds Fm hapa Jijini Dar es Salaam.
Huwa Naenjoy saaana anapokuwa katika Kipindi cha power Breakfast akiwa na Babra Hassa, Gerald Hando pamoja na Bonge.
Leo katika Kipindi hicho hicho nikiwa nasikiliza kwa umakini kama kawaida yangu coz huwa napenda sana Udaku, Nikamskia PJ kwa sauti kabisa na "Konfidensi" kama kawaida yake akitamka maneno "Halafu Then"...Mh, sasa nikajiuliza, alikuwa anamaanisha nini?, Maana Then ni Kiingereza cha neno "Halafu" kwa jinsi ninavyofahamu mie huyu na uelewa wangu Mdogo.
Swali ni "Halafu Then" ni Sahihi?, Mchapio?, Au Swagga.
Kwakweli, ni Full of "Kontradiction Kwangu.

3. STAMINA WA MTU CHEE
Huyu jamaa hapingiki kuwa ni Mkali katika 16 Barz za HIP HOP, na amini usiamini anakamu hadi 100 Barz. Jamaa ni kichwa, lakini sasa, "Born in Here Here the City without Ocean" kweli iko sawa?, mimi niliamnini alimaanisha "Mzaliwa wa Hapa hapa Mji kasoro Bahari"......
Sasa..alikuwa analazimisha Vina...au yuko Sawa?
Full of Kontradikshen kwangu

MNADA BANNER