REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

FAHAMU MTU AMBAYE, ETI ANAFANANA MDOMO NA MTOTO WA DIAMOND PLATNUMZ.

7:04:00 AM Add Comment

BAADHI ya sehemu za Mwili za Mtoto wa Diamond Platnumz na Zari, zinanza kuoneshwa kwa kificho, na huku watu wakizidi kusubiri kwa hamu kumuona.

Lakini wadaku na hata wale wataalam wa Kufananisha Vitu, wameshaanza kuzungumza kuhusu nani anafanana na Mtoto huyo katika baadhi ya Viungo, kati ya Zari na Diamond.


Katika Picha Moja wapo Ya Latiffah, ambayo ilionesha Mkono, na Mdomo kwa Mbali, basi imewafanya Followers watambue kuwa, unafanana na Mdomo wa nani kati ya watu hao wawili.

Followers zaidi ya Mmoja, walicomment na kuamini kuwa, Mdomo wa Mtoto huyo, unafanana na Mdomo wa mama Yake, yaani  ZARI THE BOS LADY

Followers hao walicomment Hivi:

maggiepetersangkaThe baby totally Zari. U got strong bood
mamamudy11kabisaaa

sheria_mwana_va_sembilinyiJamani mtoto bado mchanga rangi ake bado haijajulikana ila mdomo km wa zari(afadhali)

noszraVyote vya zari...ila mbegu ya dimond

miss_lourine@judieyni10094 lips za mama si baba. Bette


KWA Upande wako, unasemaje kuhusu Hili?

WIZI WACHANGIA KUANGUKA UCHUMI WA TAIFA

6:39:00 AM Add Comment

Imeelezwa kuwa moja ya mambo yanayochangia kuanguka kwa uchumi wa Taifa ni tabia ya wizi wa fedha za umma unaofanywa na watumishi wa Serikali kupitia njia ya manunuzi.

Hali hiyo imebainishwa juzi na Askofu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga, Askofu John Nkola katika ibada ya sherehe za kumpongeza Mchungaji Amos Ndaki kwa kutimiza miaka 21 ya utumishi wake ndani ya kanisa hilo.

Askofu Nkola amesema kuporomoka kwa uchumi wa Taifa mara nyingi kunachangiwa na watumishi wasio waaminifu ndani ya Serikali ambao huiba fedha za Serikali kwa kutumia njia ya kudanganya kwenye manunuzi mbalimbali ya umma, hivyo kuisababishia hasara Serikali.

Akifafanua amesema vitendo hivyo vimekuwa vikifanywa na watumishi wasiokuwa na hofu ya Mwenyezi Mungu ndani ya mioyo yao, hivyo kwao dhambi ya kuiba huona ni jambo la kawaida bila kuelewa wizi wanaoufanya una athari kubwa kwa walipakodi na wananchi kwa ujumla.

MNYAA APIGWA CHINI ZANZIBAR

6:33:00 AM Add Comment

Chama cha Wananchi (CUF) kimetangaza wagombea wa nafasi ya ubunge na uwakilishi kwa majimbo 54 ya uchaguzi kwa nafasi na uwakilishi na majimbo 50 kwa nafasi ya ubunge huku kikimtema kigogo wake, Muhammed Habibu Mnyaa (pichani), baada ya jimbo lake la Mkanyageni kufutwa na Tume ya Uchaguzi (Zec).

 Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Omar Ali Shehe, alisema baada ya Zec kufanya mabadiliko ya mgawanyo wa majimbo na kuongeza majimbo manne mapya, chama hicho kililazimika kufanya mabadiliko ya wagombea wa majimbo.

 Alisema baadhi ya wagombea waliogombea majimbo ya zamani na sasa yamebadilishwa majina wamewapa majimbo hayo yaliobadilishwa majina na kuwaongeza wagombea wanne kwa majimbo mapya kwa nafasi za uwakilishi.

 Mnyaa alikataliwa na wananchi katika kura za maoni, lakini baadaye Baraza Kuu la Uongozi likapitisha jina lake kugombea nafasi hiyo, hatua iliyoibua malalamiko kutoka kwa wanachama wa CUF kwa madai ya kuwa hakuwa chaguo lao.

 Baraza Kuu la CUF lilirejesha jina la Mnyaa kabla ya Zec kutoa ripoti ya mapitio na mgawanyo wa majimbo na baada ya kumaliza kazi hiyo tume ililifuta jimbo la Mkanyageni alilokuwa akiliongoza.

 Shehe alisema jana kuwa utaratibu uliotumika katika kuwapata wagombea wa majimbo mapya wamefuata katiba ya chama ambayo inaruhusu kufanya mabadiliko katika hali ya dharura.

 Aidha, CUF imemrejesha Naibu Naziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati, Haji Makame Mwadini ambaye alibwagwa katika kura za maoni kutetea nafasi yake  ya uwakilishi kwa jimbo la Nungwi na jina lake halikurejeshwa na Baraza Kuu la chama hicho, lakini sasa amepewa kugombea jimbo la Kijini.

 Waliobadilishwa majimbo baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kutaja majina mapya kwa baadhi ya majimbo ni Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu (sasa Malindi) wakati ni Ali Saleh aliyekuwa anagombea ubunge Mji Mkongwe (sasa Malindi).

Wengine ni mwakilishi wa jimbo la Mtoni, Nassor Ahmed Mazrui amepelekwa  jimbo la Mtopepo, Mansour Yussuf Himid uwakilishi jimbo la Chukwani badala ya Kiembe Samaki na Abdillahi Jihadi Hassan uwakilishi jimbo la Mwanakwerekwe badala ya Magogoni


MNADA BANNER