REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

FROM MY FACEBOOK PAGE : HII Minato ya Wiki hii...Duuuh

12:14:00 PM Add Comment
 Hahahahahaaaaa.....Usinirenge, but...oooooh My God, hiyo ishara unafahamu ni ya nini?, au ulitia Swagg tu?..Haya bhana

 Kama wewe ni Mtoto wa Kiume na Utotoni hujagusa kitu hiki, basi we ulikuwa wa kishua na Geti kali kinoma....Ilikuwa ni balaaa enzi zangu wakati nafukuzia Foward pale kati, nilikuwa naua kinoma noma

 Haya bhana....wewe ndo Mweko Mwenyewe....sijapata kukuona ukiwa ndani ya Mkato huo aisee...

 What a guuuuud Pouz, ingawa sjafahamu ilikuwa Wapi.. Thats my Beautiful Girl, Jamila on the Left Side alongside Dora Rodrick...I like dem smiles

Yah...yah...yah..Tru dat. Tufanye Magumashi, Mbwembwe, Michakato, Mishe na kila aina ya Swaggz, but when it comez to church...aaaah...jamani, lazima tumkumbuke Mwenyezi Mungu... Thats my Young Sister Ashy Racka

KALAMU YA NANDONDE WIKI HII : MWANAMKE ATANDIKWA MIJAREDI MPAKA KUTOLEWA JICHO na MUME WAKE

11:53:00 AM Add Comment


 Na Ahmad James Nandonde, MUSOMA
Mwanamke mmoja Christina Fabian mwenye umri wa miaka (27) ametandikwa na mijaredi na anayedaiwa kuwa mmewake maginga kisiri na kupelekea kutolewa jicho moja la upande wa kulia

Akizungumzia tukio hilo mbele ya waandishi wa habari mapema leo hii mwanamke kuyo amesema January mosi aliondoka nyumbani kwake anapoishi katika kijiji cha baranga wilayani tarime kwa lengo la kwenda kumwogesha mama mkwe anayeishi katika kijiji hicho ambaye ni mgonjwa na aliporudi ndipo alikutana na adha ya kipigo kutoka kwa mume wake

Amesema aliporudi nyumbani majira ya jioni ya siku hiyo alimkuta mume wake amesharudi nyumbani na kumuuliza sababu za kuchelewa nyumbani akiwa anamjibu kilichopelekea kuchelewa kurudi ndipo akaanza kumchapa sehem mbalimbali za mwili kwa kutumia mjeredi ndipo alipofikia mpaka kwenye jicho la kulia

Aliendelea kusema baaada ya kuona amempasua jicho alimuacha na asubuhi yake alimchukua na kumpeleka hospitali ya mkoa wa mara kwa ajili ya matibabu lakini walishindwa kumtibu hadi atakapo peleka pf3 kutoka polisi ndipo atibiwe

Hata hivyo wakiwa njiani kwenda polisi mume wake alimwonya kuwa asiseme kama yeye ndiye aliyempiga na aseme wamevamiwa na majambazi na kupelekea Bi Christina kusema hivyo walipofika polisi

Akizungumzia tukio hilo mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la ABC Foundation Bw. Robert Moro amesema jamii haina budi kubadilika kutokana na kujichukulia uamuzi wa kupiga katika suala ambalo linaweza kuzungumzika.

MARA MILK WAINGIA HASARA YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 8

11:47:00 AM Add Comment



Na Ahmad James Nandonde, MUSOMA
KIWANDA CHA MAZIWA CHA MARA (MARA MILK) MUSOMA KIMEPATA HASARA
ZAIDI YA SHILLINGI MILIONI 8 ILIYOSABABISHWA NA ITILAFU YA UMEME ILIYOTOKEA JANUARI 9 MWAKA HUU.

AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI OFISINI KWAKE LEO HII MKURUGENZI MTENDAJI WA KIWANDA HICHO JAMES MATHAYO AMESEMA KUWA KIWANDA HICHO KIMESIMAMA KWA MUDA WA SIKU MBILI KUTOKANA NA UHARIBIFU WA BAADHI YA VIFAA VYA KIWANDA HICHO

AMESEMA KUWA BAADA YA ITILAFU YA UMEME KUTOKEA VIFAA VIWILI VYA MOTO VILIUNGUA AMBAVYO ALIVITAJA KUWA NI HEATER ELEMENT YENYE GHARAMA YA SHILINGI 3.6 NA PAMPU YAKUPOOZA MAJI CHILLER MACHINE YENYE THAMANI YA SHILINGI MILLIONI 1.2. NA KWAMBA VINAPATIKANA NCHI JIRANI YA KENYA NAITAWALAZIMU KUVINUNUA.

NAYE KAIMU MENEJA WA KIWANDA HICHO AMBAYE PIA NI PLAN ENGENEER WA TANESCO MKOA WA MARA AMEKIRI KUWEPO KWA TATIZO HILO NA AMESEMA KUWA WANATAMBUA MCHANGO WA KIWANDA HICHO KWA SHIRIKA LA UMEME MKOANI HUMO NA WAMEOMBA RADHI KWA USUMBUFU HUO NA KWAMBA WANAENDELEA KULITAFUTIA UFUMBUZI.

AMESEMA KUWA ITILAFU HIYO IMETOKEA KUTOKANA NA KUANGUKA KWA TRANSFOMA INAYOHUDUMIA KIWANDA HICHO NA TAYARI WAMEKWISHA BADILISHA NA KUWEKA TRANSFOMA NYINGINE.

KIWANDA CHA MAZIWA MARA MILK KINAZALISHA MAZIWA YA MTINDI, YOGATI, NA MAJI YA KUNYWA AINA YA SUPER WATER.

MKWAJU MPYA : CLOSER - VANESSA MDEE

11:30:00 AM Add Comment
AUDIO TRACK : CLOSER
ARTIST : VANESSA MDEE
AUDIO PRODUCER : HERMY B & PANCHO LATINO
STUDIO : B HITZ

MKWAJU MPYA : Wazo La Leo - Stamina Ft. Fid Q

11:26:00 AM Add Comment

 AUDIO TRACK : WAZO LA LEO
ARTISTS : STAMINA FEAT. FID Q
AUDIO PRODUCER : P-FUNK
STUDIO : BONGO RECORDS

CHEMUNDUGWAO : "Asilimia 95 ya Wasanii wa Filamu, Hawajitambui "

11:08:00 AM Add Comment


MWANAMUZIKI mahiri wa muziki wa asili hapa nchini, Che Mugundugwao amewaeleza wasanii wa filamu kuwa wanakabiliwa na tatizo kubwa la kutojitambua.

Amesema kutojitambua huko kunapelekea wasanii kuwa chachu ya mauzo ya magazeti ya udaku kutokana na skendo zao.

“Asilimia 95 ya wasanii hawajitambui na bila wao kujijua, wamekuwa ni watengeneza habari hususan zile zinazowadhalilisha

“Nadhani hawajui hilo lakini kama wanajua basi hawapo sawa kiakili, jambo litakalozidi kuifanya tasnia ya filamu kukosa nidhamu na kuonekana kama fani ya wahuni”, alisema Chemundugwao.

Che Mundugwao alienda mbali zaidi pale aliposema kuwa wasanii kuandamwa na kashifa kumewasababishia hata baadhi ya wasanii wa kike kuchelewa kuolewa.

NA SALUTI 5

ALIYPIGA PICHA NA LEMA, MIAKA MINNE JELA

10:46:00 AM Add Comment


Na: Daniel Mjema-Moshi
MTU aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema akiwa amevalia sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela. Abubakari Kikulu (29), alipiga picha na mbunge huyo Desemba 23 mwaka jana, baada ya Lema kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara eneo la Mererani, ikiwa ni sehemu ya mikutano aliyoifanya kutokana na Mahakama ya Rufani Tanzania kumrejeshea ubunge wake.

Mbali na kupiga picha hiyo na Lema pamoja na Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari, kijana huyo alionekana katika picha hiyo akionyesha vidole viwili, ambayo ni alama ya Chadema.
 
Hata hivyo, baada ya picha hiyo, JWTZ lilimtilia shaka kijana huyo na kutangaza rasmi kumsaka, ili lijiridhishe kama ni mmoja wa wanajeshi wake.
Baada ya kumsaka kwa takriban siku 12, kijana huyo alikamatwa Januari 13, katika Mji wa Bomang’ombe wilayani Hai na baada ya kupekuliwa alikutwa na sare hizo.

 Jana, Kikulu alifikishwa mahakamani mjini Moshi, akiwa chini ya ulinzi wa polisi na kusomewa mashtaka mawili, ambayo yote alikiri kuyafanya kama ilivyodaiwa mahakamani.
Baada ya kukiri kosa hilo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Kilimanjaro, alimhukumu kifungo cha miaka minne jela, ili iwe fundisho wa wakosaji wengine wa aina hiyo.

Kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alimsomea mshtakiwa huyo mashitaka yake mawili, likiwamo la kujifanya Ofisa wa Jeshi, wakati akijua ni uongo.
Wakili huyo alidai mahakamani kuwa Januari 3, mwaka huu katika eneo la Bomang’ombe wilayani Hai, mtuhumiwa huyo alijitambulisha kama mtumishi wa umma.

 Katika shtaka la pili, wakili huyo alidai siku hiyo hiyo katika Mtaa wa Msikitini, eneo hilo la Bomang’ombe, mtuhumiwa alipatikana na sare za JWTZ kinyume cha sheria.

 Sare hizo ni pamoja na suruali moja, mashati mawili na kofia mbili, vyote vikiwa na alama za Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Baada ya Hakimu Kobelo kumuuliza mshtakiwa kama ni kweli alitenda makosa anayoshitakiwa, mshtakiwa huyo alikiri makosa yake katika hali ambayo haikutarajiwa.

 Kutokana na kukiri kwake makosa hayo, Hakimu Kobelo alimhukumu kifungo cha miaka miwili kwa kosa la kwanza la kujifanya Ofisa wa JWTZ na miaka mingine miwili kwa kosa la pili.
Hata hivyo, Hakimu Kobelo alisema kuwa kwa kuwa adhabu hizo zinakwenda kwa pamoja (concurrent), mshtakiwa huyo atatumikia kifungo cha miaka miwili jela.

Kwa mujibu wa hakimu huyo, kosa alilolifanya mtuhumiwa huyo ni baya na linastahili adhabu kali, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaotumia vibaya sare za majeshi nchini.

MNADA BANNER