REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

KWA ELIMU BORA ZAIDI

11:56:00 PM Add Comment

Muandalie Mtoto wako Mazingira Bora ya Elimu ya Sekondari. Shule ina walimu waliobobea katika Malezi bora ya Wanafunzi, Maadili yanayokubalika katika Jamii ya Kitanzania na kwingineko.
 Shule ina Mazingira Mazuri kwa ajili ya Wanafunzi Kujisomea, Kupumzika, na kupata Elimu Thabiti.
Huna haja ya kusumbuka, Mpatie mwanao Chaguo Sahihi, nalo ni KASSINGA HIGH SCHOOL.

MKUU WA POLISI CHUPU CHUPU KUUAWA NA WANACHI HUKO UGANDA.

11:06:00 AM Add Comment



  
KAMISHNA WA JESHI LA POLISI KITENGO CHA MAZINGIRA NCHINI UGANDA, amenusurika kuuawa na Wananchi waliokuwa wakiishi katika eneo la KYETINDA WETLAND.

Kamishna huyo, TAIRE IDWEGE, alikumbana na tafrani hiyo ambayo hakuitarajia, alipokwenda kuwaonya Wananchi hao ambao walikuwa wakiishi eneo hilo Kinyume cha Sheria ya Mazingira Nchi Humo

Taarifa zinaeleza kuwa, Kamishna IDWEGE aliponea Chupu chupu kufanyiwa Unyama huo na Wanachi wenye Mapanga makali, ambao tayari walishaanza kumzonga, Baada ya Risasi kadhaa kufyatuliwa Hewani na Jeshi la Polisi liliokuwa Eneo hilo, kwa dhamira ya kuwatawasha na kuwaogopesha

Taarifa zilizidi kumiminika kuwa, wakati Kamishna IDWEGE akitoa tamko la wananchi hao (Wavamizi) hao katika Kando ya Ziwa Viktoria kuondoka, ndipo Mmoja wa Kundi lao alisimama na kupiga kelele 
"Wewe Si una nguvu?, sasa hesabu siku zako huku tukikuonesha sisi ni akina nani"

Aidha kabla tukio hilo halijatokea, Askari wenzake waliingilia kati kuzuia Adha hiyo

KYETINDA WETLAND ni eneo a,balo liko pembezoni mwa Ziwa Victoria, ambalo ni sehemu ya Vyanzo vya maji vinavyosaidia kutiririsha Maji katika Sehemu mbali mbali za Mji wa Kampala

TIMBULO KA-DROP MKATO MPYA WA NYWELE...

10:40:00 AM Add Comment

Tumesikia Mikato kibaaao ya Nywele, na 255 kwa Sasa, Mkato wa Nywele ambao umechukua Title la Kibaba, ni KIDUKU.

 The Bongo Flava Boy, Timbulo himself ameamua kudondosha Style Mpya ya Nywele ambayo ameipa jina la T-STYLE kama ambavyo unachek hapo kwa Picha.

In that case, tufanye kama kuchek endapo Swagg hiyo ya Timbulo goes by the name T-STYLE itabeba Title kama la DUKU....

NEW DROP IN TOWN..RACERS

10:22:00 AM Add Comment

RACERS ni Crew inayojumuisha several youngsters ambao wana vipaji mbali mbali.
Ikiwa pamoja na Rappers pia producers.

Makao makuu ya Racers ni Moro Town na Crew ina miliki studio ya Audio na Video vile vile kwa mahitaji ya graphic designing,cover tracks album covers pia logo designing ni kati ya kazi ambazo Racercs inashghulika nazo kwa sasa.
For the time being kuna product ya tshirts ambazo zinapatikana kwa 15000/= each.For More Info Dia: 0656 650688-0657 659969.

KIONGOZI ATEKWA NYARA......

10:16:00 AM Add Comment



Maafisa kadhaa wa polisi wametumwa katika Wilaya ya Tana Delta, kumtafuta kiongozi wa jamii ya “Wapokomo” aliyetekwa nyara. 

Afisa Mkuu wa polisi eneo hilo, Richard Mukwate, amesema kuwa Abdalla Moyu mwenye umri wa miaka 80 alitekwa nyara na vijana wa jamii ya wa Orma na hadi sasa, hajulikani aliko. 

Aidha Afisa huyo ameongeza kuwa mzee huyo alitekwa nyara alipokuwa akiandamana na wanakijiji wengine ili kutathmini athari za shambulizi la juma lililopita, ambapo zaidi ya watu 40 waliuawa.

POLISI AUWA NA KUCHUKULIWA BUNDUKI YAKE

10:02:00 AM Add Comment



Afisa wa polisi ameuawa kwa kupigwa risasi na bunduki yake kuibwa, katika shambulizi mjini Mandera karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.

Kwa Mujibu wa Taarifa zilizothibitika kutoka Nchini Kenya, imesemekana kuwa Afisa huyo wa Polisi alikuwa katika doria pamoja  na wenzake wakati waliposhambuliwa saa tatu usiku wa alhamisi, huku  mwenzake huyo akipona kuuawa  na pia hakujeruhiwa.

Maafisa wa polisi wanasema ujumbe uliopatikana kutoka kwa wanachama wa kundi hilo unaonyesha kuwa kundi hilo liko tayari kutoa shilingi 890 000 kwa kila mwanamgambo anayemuua afisa mmoja wa usalama wa Kenya.

Zaidi ya maafisa 20 wa usalama katika eneo la Kaskazini Mashariki wameuawa katika mashambulizi yanayoaminika kutekelezwa na wanamgambo wa Al Shabaab.

MWANAFUNZI AKUTWA AMEKUFA GESTI AKIJARIBU KUTOA MIMBA

5:42:00 AM Add Comment



MWANAFUNZI  wa kidato  cha tatu katika shule ya Sekondari ya Tongoni nje kidogo ya jiji la  Tanga,  (jina tunalihifadhi) amekutwa amekufa ndani ya nyumba ya kulala wageni alikopelekwa kutolewa mimba bila mafanikio.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe mwanafunzi huyo alikutwa amekufa juzi katika nyumba ya kulala wageni iliyopo barabara ya 21 jijini Tanga.

Mmoja wa wahudumu wa nyumba hiyo ya kulala wageni ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe alisema kwamba mwanafunzi huyo aliingia saa 4.00 asubuhi siku ya tukio akiwa ameambatana na kijana mmoja wakakodi chumba.

“Baadaye alikuja mwanaume mmoja wa makamo ambaye alituuliza kama wameingia mwanafunzi huyo na mwenzake, tulipomwonyesha chumba  walichoingia naye akakodi chumba cha jirani ndipo tukaona wote wakijifungia kwenye chumba kimoja,” alisema mhudumu.

Mhudumu huyo alisema baada ya muda wa saa moja, mvulana na mzee huyo wakaaga kwamba wanatoka huku wakisema kwamba msichana amebaki chumbani akiwa amepumzika. Akithibitisha habari hizi, Kamanda Massawe alisema taarifa ya tukio hilo ilitolewa na mhudumu wa nyumba hiyo ya kulala wageni katika Kituo cha Polisi cha Chumbageni Jijini Tanga.

“Tatizo ni kwamba nyumba hii ya wageni wahudumu wake hawakuwapa wageni hao daftari ili waorodheshe majina yao hivyo inakuwa vigumu  kuwafahamu,” alisema Kamanda Massawe na kufafanua kuwa alifariki akitolewa mimba ya mwezi mmoja.

Kamanda Massawe alisema mpaka sasa hakuna mtu aliyekamatwa na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini waliohusika na kifo hicho.

Na: Raisa Said, Tanga 

MAKUBWA YAZIDI KUMKUMBA JOSE CHAMELEON

5:31:00 AM Add Comment
 Askari wa jeshi la polisi Uganda wakifanya mahojiano na Jose Chameleone (wa pili kushoto) nje ya nyumba yake.


Askari wa upelelezi akifanya vipimo eneo la tukio, mahali ambapo inasadikika Mvamizi alijichoma moto

NA New Vision, KAMPALA & Frank Joachim
Baba mzazi wa mtu aliyejulikana kama Robert Karamagi ambaye alifariki kutokana na majeraha ya kuungua kwa moto kwa kile kinachoaminika kuchomwa kwa makusudi ndani ya nyumba ya mwanamuziki Jose Chameleone wa Uganda ameibuka na kusema mtoto wake hakujilipua mwenyewe kama inavyodaiwa.

Karamagi aliyekuwa na umri wa miaka 27 alifariki katika hospitali ya Mulago saa chache baada ya kufikishwa hapo na kulazwa.

Matukio yaliyosababisha Karamagi aliyevamia nyumba ya msanii huyo kukumbwa na mkasa huo bado ni kitendawili huko mke wa Chameleone Bi. Daniella akisisitiza kuwa Karamagi alijitia moto mwenyewe alipotaka kujaribi kumchoma bibie huyo.

Lakini baba wa mtu huyo Meja Benedict Kyamanywa amepingana na ripoti kuwa mwanawe alijichoma moto mwenyewe.

Amesisitiza kuwa mwanaye alifungwa kwa kamba na kuchomwa moto ndani ya makazi ya mwanamuziki huyo.

Ameongoza kuwa kabla mwanaye huyo hajakata roho alimuambia kuwa alifungwa kamba na kuchomwa na mafuta ya ndege.

Hata hivyo katika hatua nyingine Meja Kyamanywa ambaye ni daktari msaidizi wa Kakiri Barracks amesema kuwa mtoto wa alikuwa na matatizo ya akili, na kuwa kijiji kizima kilikuwa kinajua akiwemo Chameleone mwenyewe.

PICHA: TUNAJADILI

5:18:00 AM Add Comment

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Amos Makala (Aliyevalia Shati la Kitenge) akiongea na wadau wa tasnia ya filamu kuhusu urasimishaji wa tasnia ya filamu nchini Tanzania

MNADA BANNER