REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

#BAABEKI !!: NELLY ANATAKA ALIYEMSINGIZIA KWA KESI YA UNYANYASAJI WA KINGONO AJITOKEZE HADHARANI !!!!!

12:33:00 AM Add Comment

Na Rich Sam 
#WatuWaMungu yule Hitmaker wa Mkwaju wa "Dilemma" , NELLY, bado hajaridhika kabisa na kitendo cha Bibie aliyemsingizia na kumfungulia kesi ya Unyanyasaji wa Kingono, aendelee kujificha, anatakiwa kujitokeza.

JANE DOE, ndiye mwanamke ambaye Mwezi November 2018 aliushangaza ulimwengu kwa kumfungulia Mashtaka Rapper Nelly, akidai kuwa msanii huyo alimdhalilisha kijinsia mnamo mwaka 2017 katika Tamasha ambalo lilifanyika Nchini Uingereza, na Nelly alikuwa ni msanii ambaye alikuwa akishusha show yake katika jukwaa hilo

Katika maelezo yake, Jane alidai kwamba alielekea upande wa "BACKSTAGE" kwa ajili ya kumuona Rapper huyo na kusalimiana nae, lakini alipofika pale, alishangaa kumuona Nelly akianza kumshawishi kingono, kisha akaanza kujichua uume wake, na kisha akamlazimisha JANE kufungua mdomo wake ili Nelly amalizie haja yake kwa  njia ya mdomo

Aidha, Mlalamikaji anadai kuwa, awali hakutoa taarifa kuhusu tukio hilo kutokana na kuwa na hofu kama Jeshi la Polisi lingemuamini.

Sasa Basi, January 24, Rapper Nelly ameiomba mahakama kufutilia mbali mashtaka na malalamiko ya mwanamke huyo, huku akisihi mahakama imuamuru mwanamke huyo kujitokeza mbele ya umma ili watu wamfahamu, pengine huenda ukapatikana ushahidi imara zaidi.


MNADA BANNER