REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

"Huruma ya Usher kwenye kifo cha Mtoto Wangu Ni UPUUZI Mtupu!!!- Tameka

6:33:00 AM Add Comment
Marehemu Kile, Mtoto Wa Tameka.

Tameka Raymond, na Usher Rymond.




Na Frank M. Joachim.


Ex- Wife wa Muimbaji machachari katika miondoko ya R&B Usher Rymond, Tameka Rymond , amebainisha kuwa Huruma ya Usher Rymond dhidi ya kifo cha Marehemu mtoto wake kilichotokea Hivi karibuni, Ni UPUUZI na UNAFIKI MTUPU!!!!!!!!!!!!
Bibi huyo ambaye bado kabisa yuko kunako Majonzi ya Mtot wake Mpendwa aliyepata ajali na kuathirika katika sehemu kubwa ya Ubongo, amesema kuwa Kitendo cha Usher kujifanya anahuruma….kinamkwaza saaaana
“Usher ni Mnafiki sana na ni mpuuzi katika hilo. Anazuga kuathirika na kuumia sana dhidi ya Kifo cha Mtoto wangu KILE mbele ya marafiki zake, Mitandao ya Kijamii na Vyombo vya Habari pia".

Mrembo huyo amesema kuwa, Usher  amekuwa akijifanya kuwa na Stress kibao hasa wakati anapokuwa akifanya maintavyuu kibaao

Tameka amefungua Kesi dhidi ya Mkali huyo wa “Dady’s Home” kwa kushirikiana na Mwanasheria wake, ambapo usher mwenyewe aesema kuwa, kesi hiyo haitakuwa na manufaa yoyote kwa Tameka, na italeta matatizo chungu mzima kwa wawili hao na watoto wao wawili ambao bado ni wadogo
“Ukiachana na hayo, Tameka hatapata haki ambayo anaitarajia maanake, mahakama haitokuwa tayari kusikiliza Kesi ambayo imeanzishwa na Mama ambaye bado yupo katika maombolezo.” Alidai Usher

Katika madadi Makuu ya Tameka ni kwamba, Mumewe huyo hakujali hali ya Mtoto wake (Kile) katika Siku za Mwisho alipokuwa katika hali mbaya Hospitali, licha ya Usher kukubali na kujidhatiti kumchukulia kama Mtoito wake baada ya wawili hao kufunga ndoa
“Usher alimtembelea  marehemu mwanangu Kile hospitalini mara moja tu, kati ya siku 15 ambazo mwanangu alikuwa akihangaikiwa kupigania Uhai wake” aliongeza Tameka.

HII SASA KALI!!!!!.....................................

Katika hali ambayo haikutarajiwa, Tameka anongeza kuwa, alimsihi sana Usher aandike katika Ukurasa wake wa TWEETER kuwa “TAFADHARI, MUOMBEENI KILE”, lakini Usher alitia ngumu kabisa, na badala yake, Usher aliweka Picha ya Chai yake katika Ukurasa huo wa TWEETER, huku akiandika chini ya picha hiyo kuwa “CHAI YA WASHINDI”

Floyd Mayweather aachiwa Huru

5:56:00 AM Add Comment




Bondia Floyd Mayweather.


Na Frank M. Joachim

New York, MAREKANI.

The Boxing Champ mwenye Utata Mkubwa, Floyd Mayweather Jr, ameachiwa Huru siku ya Ijamaa Aasubuhi kutoka katika Jela ya Vegas, ambako alitumikia Kifungo cha miezi miwili kati ya Mitatu aliyokuwa amehukumiwa kutokana na ukatili wa Nyumbani
Jembe hilo (Floyd) alihukumiwa kutumikia Kifungo hicho mnamo December  mwaka 2010, baada ya Kushushia Kifinyo mama wa mtoto wake mbele ya Watoto wake, lakini Mpiga Nyundo (Hakimu) alimruhusu kuanaza kutumika Kifungo chake Mwezi June, Tarehe 1, kutokana na Kuwepo kwa Mpambano dhid yake na Miguel Cotto uliopangwa kuchimbika May 05 Mwaka jana, ambapo Floyd alishinda.
Msemaji wa Mpiga Masumbwi huyo, amefafanua kuwa, jombaa alihukumiwa  kifungo cha Miezi 6, baada ya kugundulika kuwa na makosa, sambamba na kuwakung’uta watoto wake katika Tukio hilo.
Jamaa huyo naongeza kuwa Floyd alionesha Tabia nzuri akiwa katika kifungo hicho, ambapo pia alitumikia masaa 100 katika shughuli za Kijamii.
5:32:00 AM Add Comment


Kim Jong Un, Rais wa Korea Kaskazini



Pyongyang, Mji Mkuu wa Korea Kaskazini.

Na Frank M. Joachim & DW

Pyongyang, KOREA KASKAZINI
Korea ya Kaskazini inahitaji msaada wa haraka wa chakula, baada ya mvua kubwa kuuwa idadi kubwa ya watu na kusababisha mafuriko katika maeneo mengi ya kilimo.
Haya yametangazwa na afisa wa Umoja wa Mataifa jana, ambapo  amesema ofisi ya Umoja wa Mataifa katika mji mkuu wa Korea Kaskazini Pyongyang imethibitisha hali hiyo baada ya kuyazuru maeneo yaliyoathirika mwanzoni mwa wiki.
Mvua kubwa iliyonyesha mara mbili iliuwa watu 119 na kuharibu maelfu ya nyumba za watu, hii ikiwa ni kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya Korea Kaskazini. Marekani imesema inatathmini msaada inaoweza kuutoa, ingawa haijapata ombi kutoka kwa Korea Kaskazini. Mvua hizo ambazo zilifuatia kipindi kirefu cha ukame, imezusha wasiwasi juu ya uwezo wa Korea Kaskazini kutosheleza mahitaji ya chakula kwa watu wake.
Mwezi Juni Umoja wa Mataifa ulisema theluthi mbili ya wakazi milioni 24 wa Korea Kaskazini hawana chakula cha kutosha.

Urusi yatuma Meli za Kivita Nchini Syria

5:24:00 AM Add Comment






Moja kati ya Meli Hatari za Kivita za URUSI.


Na Frank M. Joachim & DW


Moscow, URUSI.

Watu wengi wameuawa katika mitaa ya mji wa Hama ulio katikati mwa Syria, ambao umezingirwa na wanajeshi wa serikali.
Ripoti hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kuchunguza Haki za Binadamu la nchini Syria lenye makao yake nchini Uingereza. Shirika hilo halikutaja idadi kamili ya waliokufa, likisema mawasiliano ya simu katika wilaya ya Al-Arbaeen yalikuwa yamekatwa.  Hata hivyo, Kamati ya Kuratibu Shughuli za Wanaharakati imesema waliokufa, ambao ni raia na waasi, hawapungui 50. Hakuna shirika lisiloegemea upande wowote lililothibitisha idadi hiyo.
Msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Syria Hisham Hassan amesema wameondoa wafanyakazi wao kwa kuhofia usalama.  Huku hayo yakiarifiwa, Urusi imetuma meli tatu kubwa za kivita nchini Syria, zenye kubeba nyambizi 120 kila moja.
Shirika la Habari la Urusi limemnukuu afisa wa Urusi akithibitisha kutumwa kwa meli hizo, lakini sababu ya kile zinachokwenda kukifanya haikutajwa. Wakati huo huo tangazo la kujiuzulu kwa mpatanishi wa kimataifa nchini Syria Kofi Annan ifikapo mwishoni mwa mwezi huu, limechukuliwa na wachambuzi kama kutoweka kwa uwezekano wa kupatikana kwa sulihisho la amani katika mzozo wa Syria.

MNADA BANNER