REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

KENYA: NAULI YA Kshs 20 Yaua Abiria

3:50:00 AM Add Comment


Mwanamume amefariki baada ya kutupwa nje ya Gari aina ya matatu kufuatia ugomvi kuhusu nauli ya shilingi 20 katika barabara ya Juja hapa Nairobi. 

Polisi wanasema kwamba mwanamume huyo alizozana na kondakta wa matatu hiyo kabla ya kusukumwa nje ya matatu hiyo mwendo wa saa tano jana usiku. Polisi wanawasaka wahudumu wa matatu hiyo walitoweka kwa gari hilo, mara tu baada ya tukio hilo.Kisa hiki kimetokea mwezi mmoja tu baada ya tukio sawa na hilo kutokea mtaani Kawangware ambako mwanamke mmoja aliskumwa nje ya basi kufuatia ugomvi kati ya na kondakta kuhusu nauli ya shilingi 10.

ISTA-FATHER

3:45:00 AM Add Comment

Picha ya Wizzy Khalifa ambayo aliipost katika Mtandao wa Instagram "Ready to Be a Fathere" wakati wa hati hati za Amber Kujifungua.

Hongera za Dhati kwa Amber Rose na Wizzy Kahlifa kwa kupata Dume..

PICHA : RAIS KIBAKI ALIPOTEMBELEA KIWANDA CHA MAGEREZA-UKONGA

3:35:00 AM Add Comment
  
TWENDE TUKAJIONEE: Rais wa Kenya, Mwai Kibaki (wapili kutoka kulia) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wa pili kutoka kushoto),  Mkuu wa Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kulia) pamoja na maofisa mbalimbali kutoka nchini na Kenya, wakiingia ndani ya kiwanda hicho.


 SALAM YA KENYA NA TANZANIA: Rais wa Kenya, Mwai Kibaki (kushoto) akimsalimia Mkuu wa Jeshi la Magareza nchini, Kamishna Jenerali John Minja kabla ya kuingia ndani ya  Kiwanda cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Wa pili kutoka kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, anayefuata ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima.

KITI CHA WAPENDANAO: Rais Mwai Kibaki (wa kwanza kutoka kulia aliyevaa tai) akiwafurahia Askari Magereza na ofisa kutoka nchini Kenya wakiwa wamekaa kwenye kiti cha wapendanao kilichotengenezwa na wafungwa kiwandani humo.

ITASAIDIA SANA KATIKA AJALI: Mshauri Mtaalamu wa Mradi wa Kiwanda cha kutengeneza kofia ngumu katika Jeshi la Magereza, Alpherio Moris (kulia) akimuonyesha Rais Mwai Kibaki moja ya kofia ngumu (Helmet) ambayo inatarajiwa kutengenezwa na kiwanda cha magereza Ukonga hivi karibuni.

POKEA KIDOGO TULICHO NACHO Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jeneral John Minja (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum ya kiti Rais Mwai Kibaki wa Kenya.

PAMOJA: Rais Mwai Kibaki akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali nchini pamoja na maofisa kutoka nchini Kenya.


HAKIKA NIMEJIONEA MWENYEWE: Rais Mwai Kibaki (wa pili kushoto) akiwa na maofisa mbalimbali wakiondoka Kiwanda cha Magereza Ukonga baada ya kumaliza kuangalia vifaa mbalimbali vinavyotengenezwa na kiwanda hicho.




PICHA ZOTE NA
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

TANZANIA YANG'ARA LONDON

3:18:00 AM Add Comment




CHANZO: Urban Pulse na Freddy Macha
Jumapili mchana  wilaya ya Westminster jijini  London ilikuwa na mashindano ya ubunifu na urembo katika maonyesho  ya kimataifa ya London Fashion Week. Mashindano haya yalifanyika jumba la Somerset lililosimama imara  kwenye upembe wa  kaskazi ya mto Thames.

Maonyesho ya London Fashion Week, bado yanaendelea jumba hili  la Somerset toka tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. Magwiji na mapapa wa mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda.  Wote hukutana katika maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa biashara.

Siku hii Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na British Council na LFW kushiriki kwenye mashindano  ya kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo.  Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na  Christine Mhando ndio wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka 27 sasa.

Katika kuunga mkono maendeleo ya Tanzania na Watanzania,  Ubalozi wetu  Uingereza na Bodi ya Utalii Tanzania, nao pia walichukua nafasi hii kuwasaidia wananchi hawa kufanikisha mahitaji yao ya ushindani. Ubalozi umetoa Ukumbi wa Nyumba Ya Tanzania ulioko Bond Street ili wasanii hao waweze kuonyesha nguo na sanaa zao kwa juma zima kama sheria za London Fashion Week zinavyoamuru. Vile vile Bodi ya Utalii ya Tanzania imesaidia katika mchango  wa mali ghafi zilizotumika katika shughuli hizi  ili kuiuza Tanzania kimataifa.

Mshindi wa tukio alikua Estonia. Ingawa  Tanzania haikuwa mshindi wa mwanzo- ilichaguliwa kati ya Kumi Bora jambo ambalo limetikisa nyoyo na vichwa vya  waandaaji, wabunifu,wafanya biashara na watafuta vipaji vya kimataifa. Hii ni mara ya kwanza kwa taifa letu kushiriki katika shughuli na  wote wameguswa na kupumbazwa na usanii wa hali ya juu ulioonyeshwa na wasanii  watatu wa Kitanzania.   Lukindo, Mhando na Kibacha wamechukua nafasi waliyopewa kwa mikono miwili na wote wameisogeza Tanzania hatua moja zaidi ndani ya ulingo wa kimataifa na katika biashara hii ya mavazi na urembo ambayo inasemekana ina thamani ya  Pauni Billioni 10  ama  shilingi Trillion 25 za Tanzania.


UJANGIRI TENA

3:15:00 AM Add Comment



Na Hamza Mashole  wa  Songea
Kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA kwa kushirikiana askari wanyamapori wa Selou na Askari wa vijiji vinavyozunguka pori la Akiba la Selou wamefanikiwa kukamata meno ya tembo 15 yenye thamani ya milion miambili, Risasi 9, Bunduki moja aina ya RIFFLE 458 na Gobole moja ambavyo hutumika kuulia wanyama .

Doria hiyo imechukua takribani siku tatu katika pori la Akiba la Selou ikiwa ni sehemu ya kuwatafuta majangili wanaofanya mauaji ya wanyamapori katika pori hilo,
Akizungumza na mwandishi wetu Bw. Mohamed Mpapa ambaye ni mwakilishi wa kampuni hiyo ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA, Amesema kuwa hiyo ni kujituma kutokana na motisha ya fedha anayoitoa mwezeshaji wa kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA ndio chachu ya mafanikio ya kukamata meno,bunduki na risasi.

 Akiendelea kuzungumzia tukio hilo Bw. Mohamed Mpapa amesmea baada ya majangili kuwaona Game Frontiers Tanzania wakiwa katika doria ndani ya pori hilo huku wakiwa wamekamilika kimapigano majangili hao waliweza kukimbia na kuacha nyara hizo baada ya kuona nguvu yao ni ndogo katika kupambana na kundi la doria.

Ameongezea kwa kusema Kampuni yake imefurahishwa na mafanikio na ushirikiano uliopo kati yao, Serikali na wanavijiji kukabiliana na ujangili unaoendelea kuwamaliza tembo katika Pori la Akiba la Selou pia ametoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano katika kuwafichua majangili.

Nae Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kusini Magharibi ya Pori la Akiba la Selou Bw. Bernald Lijaji amesema Pembe zilizokamatwa ni 15 pamoja na Bunduki aina ya RIFLE 458,Gobole moja na Risasi 9 aina ya 458 vimekamatwa katika Doria iliyofadhiriwa na Mwekezaji wa Kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA

MNADA BANNER