REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

FILAMU YA "FUNGATE" HIYOOOOOO

10:35:00 AM Add Comment
Hivi Ndivyo Flamu ya Fungate ilivyokuwa Ikifanyiwa kazi katika Maandalizi yake. Tunaisubiri Kwa Hama











WANAOENDELEA EPIC BSS 2012 NI HAWA

10:13:00 AM Add Comment
ALWAYS ON MY MIND aliimba Vizuri Sana, Ila Back Vocals za Live Band ziliniboa Kiujumla.Off Course Jamaa ni Mkali ktk Vocal

All The Way From Taarabu hadi Track alioimba Juzi......haikuwa Nzuri, na Kwa Huyu Mrefu kabisa, nahisi Chreography anaifahamu sana...I mean Kucheza. Sina uhakika na Suala La Kuimba

Nashindwa Kuelewa kwaninji katika Simu aliimba Vizuri....But akiwa Live...Huwa Ninadoubt sana...though Majaji wanasema "Ni Mkali".....Sihitaji Mninukuu kivyenu, But Huu ni Mtazama wangu na Wadau Wenzangu tunaopenda MUSIC.

Yes....Jitihada Nzuri sana anazifanya Katika Kucheza...Namkubali kwa Hilo, ila katika Kuimba, Awe Makini Kupita Maelezo...otherwise, atabaki kuwashuhudia Wenzake wakichukua Milioni kadhaa za Ushindi

Thats Why Alidondosha Machozi kabla hajafahamishwa kama anaondoka au Laahh!!... Safari Hii alijitahidi Kiukweli. Vocal Ili9seto haswaa, pindi alipokuwa anaanza Kuimba, ila Mwishoni ilikuwa OVYOOOOOO!!!...Pia nilipenda MIc Control Yake katika Vocal Raising. Anahaki ya Kuwa Kwenye DANGER ZONE
 

Pole Sana Salma...All The Way From Zanzibar. Nilishindwa kuelewa kama GUITAR ndilo lilikuwa linampiga TAFU kipindi cha Mwanzo....Juma hili hakufanya Vizuri sana, kiasi kwamba alidondosha Machozi on Stage hadi nikamuonea Huruma 

Geofrey (Kulia).....ndiye Mkali zaidi Yao. Much Efforts zinahitajika

MHAYA (Kushoto) hakufanya Poa licha ya Kukubalika kwa Majaji. Firstly alikuwa analizaimisha Sauti "VOCAL FORCING" (kitaalam) hasa BASE la Joe Mafela katika Wimbo wa "SHEBELEZA".
Haikuwa Poa sana....but Majaji ndo Washaamua. Kulia, jamaa alifanya Uzuri Pia.

Nilisikia Neno "nimependa Hiyo Tai yako"...then Sikusikia Coment Nyingine iliyoniridhisha

Hosts Wa Shindani Wananifurahisha Sana....Hivi Vanessa ilikuwaje MTV?

HAYA NI MAONI YANGU NA BAADHI YA WADAU WENZANGU......

HIVI NDIVYO DRAKE ALIVYOKUWA OUT

9:20:00 AM Add Comment

Hii Ni Moja ya Picha ambazo "The Champaigne Papi" Drake amepost katika Ukurasa wake wa TWEETER alipokuwa Out au "On Vocation" na Crew yake ya OVO

CONFIRMED : MUUAJI WA GADAFI HUYU HAPA !!!!!

3:45:00 AM Add Comment


Ripoti iliyotolewa na gazeti la Daily Mail linalochapishwa nchini Uingereza imeeleza kwamba dikteta wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi aliuliwa na ajenti wa siri wa Ufaransa kwa amri ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Nicolas Sarkozy. 

Inasemekana kuwa jasusi huyo wa Ufaransa alijipenyeza kwenye kundi moja la vikosi vya wanamapinduzi wa Libya lililomkamata mateka Gaddafi kwenye bomba la majitaka katika mji alikozaliwa wa Sirte na kumpiga risasi.

 Likizinukuu duru za Libya Daily Mail limeandika kuwa ajenti huyo wa Ufaransa aliamriwa na Rais wa zamani wa nchi hiyo Nicholas Sarkozy kumuua Gaddafi ili kumzuia asije akafichua mahusiano yake na Sarkozy endapo angesailiwa. Kabla ya kuuawa na kufuatia mashambulio ya anga yaliyofanywa na shirika la kijeshi la NATO nchini Libya, Muammar Gaddafi alitishia hadharani kwamba angefichua kwa undani uhusiano wake na rais huyo wa zamani wa Ufaransa. 

Sarkozy, ambaye aliwahi kumwita dikteta wa zamani wa Libya 'kiongozi ndugu' wakati alipofanya safari nchini Ufaransa anasemekana kuwa alipokea kutoka kwa Gaddafi kitita cha yuro milioni 50 kusaidia kampeni zake za uchaguzi wa rais wa mwaka 2007. 
Gazeti la Kitaliana la Corriere della Serra nalo pia limeripoti kuwa duru za Libya zimeeleza kwamba muuaji wa kigeni mwenye uraia wa Ufaransa ndiye aliyemuua Gaddafi

TIMU MBILI KUCHUNGUZA KIFO CHA YASSIR ARAFAT

3:36:00 AM Add Comment
Yassir Arrafat


Timu mbili kutoka Ufaransa na Uswisi zinataraji kufanya chunguzi mbili kwa wakati mmoja kuhusiana na kifo cha Yassir Arafat aliyekuwa kiongozi wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO).

 Tangazo hilo lilitolewa hapo jana na maafisa wa Palestina. Timu ya Ufaransa itatekeleza kazi hiyo kwa niaba ya Suha Arafat mke wa Yassir Arafat na timu kutoka Uswisi itatekeleza shughuli hiyo kufuatia mwaliko wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina. 

Chunguzi hizo zitafanywa kwa wakati mmoja lakini na timu mbili tafauti ambazo zitaruhusiwa kulizuru kaburi kwa pamoja na baadaye kuchukua sampuli mara moja pekee. Hayo yamesemwa na Tawfiq Tirawi Mkuu wa Kamati ya Uchunguzi ya Palestina.

HIVI NDIVYO WANANCHI WA IRINGA WALIVYOJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA VIWANJA....

3:28:00 AM Add Comment

MNADA BANNER