REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

AFYA: MUHIMBILI NA AGA KHAN KUTOA HUDUMA YA UPASUAJI WA MOYO

11:17:00 PM


HUDUMA za matibabu na upasuaji wa moyo zitaanza kupatikana nchini, kutokana na mipango ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na ile ya Aga Khan.

Hatua hiyo itawawezesha wagonjwa wa moyo nchini kutopelekwa kwa wingi nje ya nchi kama ilivyo sasa. Pia itaokoa mamilioni ya fedha ambazo zimekuwa zikitumika kugharimia tiba hiyo nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Huduma za Afya wa Hospitali za Aga Khan Tanzania, Dk Jaffer Dharsee akiwasilisha taarifa kuhusu ongezeko la magonjwa ya moyo nchini katika kongamano la wataalamu wa magonjwa hayo alisema, jitihada kubwa zinafanywa ili kuhakikisha tiba ya moyo inaanza kutolewa nchini.

Alisema Hospitali ya Muhimbili inakusudia kuanza kutoa tiba hiyo katika kipindi cha miezi miwili ijayo baada ya ujenzi wa taasisi yake kukamilika, wakati Hospitali ya Aga Khan itaanza kutoa matibabu hayo mwakani. Kongamano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Hatua ya kuwapo kwa tiba za moyo nchini, itawezesha gharama za tiba kupungua kwa asilimia 57.1, ikilinganishwa na gharama za tiba hizo nje ya nchi.

Dk Dharsee alisema hapa nchini gharama za tiba zitakuwa Dola za Marekani 1,500 sawa na Sh2.4 milioni tofauti na Dola 3,500 (Sh5.6 milioni) zinazotumika kumpeleka mgonjwa kwa ajili ya upasuaji nchi za nje kama India.

Alisema gharama hiyo inatokana na kuwapo kwa gharama kubwa zinazohitajika kuandaa maabara hiyo ambayo ina thamani ya Dola 200 milioni (Sh320 bilioni) bila kuingiza gharama za wataalamu wa kuiendesha na kuhudumia wagonjwa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

MNADA BANNER