REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

KIMATAIFA:Israel Yaonywa

5:08:00 AM


Washiriki kwenye kongamano la kimataifa la kuonesha mshikamano na wafungwa wa Kipalestina wanaoshikiliwa na utawala wa Kizayuni wa Israel wameuonya utawala huo ghasibu juu ya ukiukaji wa haki za wafungwa wa Kipalestina na Kiarabu.

Katika sherehe za ufunguzi wa kongamano hilo, Rais Jalal Talabani wa Iraq amesisitiza kuwa, hadi sasa hakuna juhudi zozote zinazofanywa kwa shabaha ya kukomesha machungu na mateso wanayopata wafungwa wa Kipalestina wanaoshikiliwa kwenye jela za Israel na kufichuliwa siasa zisizo za kibinadamu zinazofanywa na utawala huo dhidi ya wananchi wa Palestina. Ameongeza kuwa, kadhia ya Palestina ni kadhia ya ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu tokea  miaka 60 iliyopita na kusisitiza kuwa, kushiriki kwa wingi shakhsia mbalimbali wa kisiasa na kijamii kwenye kongamano hilo kunaonesha jinsi fikra za waliowengi zinavyochukizwa na siasa za ukandamizaji za Israel.

Nabil al Arabi, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema katika kongamano hilo kuwa jinai zinazofanywa na Israel dhidi ya wananchi wa Palestina hazitafumbiwa macho na kusisitiza kwamba viongozi wa Israel wanapaswa kufunguliwa mashtaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa jinai za kivita walizotenda dhidi ya wananchi wa Palestina. Nabil al Arabi amesema kuwa, tokea mwaka 2000 hadi sasa wanajeshi wa utawala wa Israel wametia mbaroni watoto na vijana karibu 2000 wa Kipalestina na jambo hilo linaonesha ukiukaji wa wazi kabisa wa makubaliano ya kimataifa ya kuwalinda watoto.

Kongamano la kimataifa la kuonesha mshikamano kwa Wapalestina limeanza leo mjini Baghdad mji mkuu wa Iraq likihudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi 70 duniani.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

MNADA BANNER