REPIN ROCK CITY

REPIN ROCK CITY

TUMA TRACK YAKO

DAVIDO KATIKA MBWADIDI NA MAAFISA WA UHAMIAJI CHINI NIGERIA

3:23:00 AM

SIKU CHACHE ZILIZOKATA, davido aliweza kutweet kupitia account yake ya Twitter, kuwa Maafisa wa Uhamiaji Nchini Nigeria, ambao anadai walimuonea na kumnyanyasa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa MURTALA MOHAMMED, kwa sababu za Kifedha.

Lakini baada tu ya Tweet hiyo kuzagaa kunako Social Networks, Idara Hiyo ya Uhamiaji Nchi Nigeria, imekanusha madai hayo hasa ya kifedha, huku wakiweka bayana kila kitu ili kuepusha Matatizo na Msanii huyo pamoja na wananchi Mbali mbali.

Kwa Mujibu wa taarifa maalumu iliyotolewa na Afisa Habari wa Idara Hiyo ya Uhamiaji, EMEKA OBUA, inasemekana kuwa  davido alimfuata afisa mmoja katika Uwanja huo wa Ndege Siku ya safari, kwa Dhumuni la Kusafiri kwenda Nje ya Nchi, akitumia Passport aliyochukua Nchini marekani, ikiwa na namba 460918874, ambayo ilikatwa Jijini Georgia, DECEMBER 14 209, na inafanya kazi mpaka December 14 2019.

Afisa huyo alizidi kumiminika kuwa, baada ya Afisa husika kuipitia Passport hiyo na kubaini ina tatizo, alimuambia Ukweli Davido kuwa, hawezi Kutoka Nje ya Nchi hiyo kwa sababu Passport hiyo haikuwa na Visa, hivyo ameona ni bora akuonesha passport aliyokatia Nchini Nigeria.


Baada ya Davido Kuambiwa hivyo, inasemekana alimuambia afisa huyo kuwa passport ya Nigeria ameisahau Nyumbani, jambo ambalo Afisa huyo bado hakukubaliana nalo, na kumuambia aelekee nyumbani kuifuata Hiyo passport.

Baada ya Kuambiwa Hivyo, Davido kwa kushirikiana na mabaunsa Wake, walianza kumfokea na Kuanza kuzonga Afisa huyo wa Uhamiaji na kulalamika kuwa inawezekana Vipi ukamzuia Mtu Kusafiri kisa hana Passport ya Nchi Hiyo, na Anapassport Nyingine ambayo haina Shida.

Hata hivyo inasemekana Kuwa, baadaye davido alifuata Taratibu zote, na Kuwakilisha Passport ya Nigeria ambayo ina namba A02227477 iliyochukuliwa  Abuja Mnamo August13, 2010 and na itafanya kazi mpaka August 12, 2015.



Katika kukemea hilo , EMEKA amesema tabia kama za Davido hazifai hasa katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa, na Endapo mtu anahitaji kutumia Passport za aina hiyo, basi huwa kuna Barua maalum ama maandishi maalumu ili kufanikisha safari.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

MNADA BANNER